< Ezra 6 >

1 Thus King Darius ordered that a search be made of the archives that were housed in the treasury of Babylon.
Kisha Mfalme Dario alitoa amri, nao wakafanya uchunguzi katika kumbukumbu zilizohifadhiwa katika hazina huko Babeli.
2 But it was actually in the fortress of Ecbatana, in the province of Media, that a scroll was found, recording the following:
Karatasi moja ndefu ya maandishi ilipatikana huko Ekbatana katika jimbo la Umedi. Haya ndiyo yaliyokuwa yameandikwa humo: Kumbukumbu:
3 In the first year of King Cyrus, he issued a decree regarding God's Temple in Jerusalem: Let the Temple be rebuilt as a place where sacrifices are offered, and make sure it has strong foundations are firm. Make it sixty cubits high and sixty cubits wide,
Katika mwaka wa kwanza wa kutawala Mfalme Koreshi, mfalme alitoa amri kuhusu Hekalu la Mungu katika Yerusalemu: Hekalu na lijengwe tena mahali palepale Wayahudi walipokuwa wakitoa dhabihu, kwenye msingi ule ule. Iwe na kimo cha mikono sitini, upana wa mikono sitini,
4 with three layers of stone blocks and one of timber. Expenses are to be paid from the royal treasury.
kuta zijengwe kwa safu tatu za mawe makubwa kisha ifuate safu moja ya mbao. Gharama zitalipwa kutoka hazina ya mfalme.
5 In addition, the gold and silver items of God's Temple, which Nebuchadnezzar took from the Temple in Jerusalem and brought to Babylon, must also be returned to the Temple in Jerusalem and placed there.
Pia, vyombo vya dhahabu na vya fedha vya nyumba ya Mungu, ambavyo Nebukadneza alivichukua kutoka kwenye Hekalu huko Yerusalemu akavileta Babeli, yapasa virudishwe mahali pake ndani ya Hekalu huko Yerusalemu, yapasa viwekwe ndani ya nyumba ya Mungu.
6 These are my instructions to you, Tattenai, governor of the province west of the Euphrates, Shethar-bozenai, and your fellow officials, and officials of the province: Stay far away from there!
Sasa basi, Tatenai, mtawala wa Ngʼambo ya Mto Frati na Shethar-Bozenai pamoja na ninyi, maafisa wenzao wa jimbo hilo kaeni mbali na mahali hapo.
7 This work on God's Temple—leave it alone! Let the governor and leaders of the Jews continue with rebuilding this Temple of God on its original site.
Msiingilie kazi ya Hekalu hili la Mungu. Mwacheni mtawala wa Wayahudi na viongozi Wayahudi wajenge upya nyumba hii ya Mungu mahali pake.
8 Furthermore, this is my decree as to what you are to do for these Jewish leaders regarding the rebuilding of this Temple of God. The full expense involved is to be paid from royal income, the tribute of the province west of the Euphrates, so that the work will not be delayed.
Zaidi ya hayo, hapa natoa amri kuhusu mtakalofanya kwa ajili ya wazee wa Wayahudi katika ujenzi wa nyumba hii ya Mungu: Gharama za watu hawa zitalipwa kikamilifu kutoka hazina ya mfalme, kutoka kwenye mapato ya Ngʼambo ya Mto Frati, ili ujenzi usisimame.
9 Provide whatever is needed by the priests in Jerusalem: young bulls, rams, and lambs for burnt offerings to the God of heaven, and wheat, salt, wine, and olive oil. Make sure to give them this each day without fail.
Chochote kinachohitajika kama mafahali wachanga, kondoo dume, wana-kondoo kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa kwa Mungu wa mbinguni, ngano, chumvi, divai na mafuta kama vitakavyohitajika na makuhani huko Yerusalemu, lazima wapewe kila siku pasipo kukosa,
10 In this way they can offer sacrifices that are acceptable to the God of heaven, and pray for the lives of the king and his sons.
ili waweze kutoa dhabihu inayompendeza Mungu wa mbinguni na kumwombea mfalme na wanawe hali njema.
11 Further I declare that if any man interferes with this decree, a beam is to be ripped from his house and set in the ground, and he is to be impaled on top of it. His own house shall be turned into a pile of rubble for disobeying this decree.
Zaidi ya hayo, ninaamuru kwamba mtu yeyote atakayebadilisha amri hii, boriti itangʼolewa kutoka nyumba yake, ichongwe upande mmoja na atumbuliwe nayo. Kwa ajili ya kosa hili nyumba yake ifanywe lundo la taka.
12 May God who chose the city of Jerusalem as the place where he would be honored, destroy any king or people who try to alter what I have said or who destroy this Temple. I, Darius, issue this decree. Let it be faithfully carried out.
Naye Mungu, aliyeliweka Jina lake huko, amwangushe mfalme yeyote au watu watakaoinua mikono kubadili amri hii au kuharibu Hekalu hili lililoko Yerusalemu. Mimi Dario nimetoa amri hii. Nayo itekelezwe kwa bidii na kwa makini.
13 Tattenai, the governor of the province west of the Euphrates, Shethar-bozenai, and their fellow officials faithfully carried out what King Darius had decreed.
Kwa sababu ya amri aliyotoa Mfalme Dario, Tatenai mtawala wa Ngʼambo ya Mto Frati na Shethar-Bozenai na wenzao wakaitekeleza kwa bidii na kwa makini.
14 As a result the Jewish leaders continued building, and they were encouraged by the messages from Haggai the prophet and Zechariah, son of Iddo. They completed building the Temple following the command of the God of Israel, and the decrees of Cyrus, Darius, and Artaxerxes, kings of Persia.
Hivyo wazee wa Wayahudi waliendelea kujenga na kustawi kutokana na mahubiri ya manabii Hagai na Zekaria, mwana wa Ido. Wakakamilisha ujenzi wa Hekalu kulingana na agizo la Mungu wa Israeli na amri ya Koreshi, Dario na Artashasta wafalme wa Uajemi.
15 The Temple was completed on the third day of the month of Adar, in the sixth year of the reign of King Darius.
Hekalu lilikamilika siku ya kumi na mbili ya mwezi wa Adari, ndio mwezi wa tatu, katika mwaka wa sita wa utawala wa Mfalme Dario.
16 Then the people of Israel, the priests, the Levites, and the rest of those who had returned from exile, all joyfully celebrated the dedication of the God's Temple.
Kisha watu wa Israeli: makuhani, Walawi na wengine wote waliohamishwa, wakaadhimisha kule kuwekwa wakfu nyumba ya Mungu kwa shangwe.
17 To dedicate God's Temple they sacrificed one hundred bulls, two hundred rams, four hundred lambs, and a sin offering for the whole of Israel comprising twelve male goats, one for each Israelite tribe.
Kwa ajili ya kuwekwa wakfu nyumba hii ya Mungu walitoa mafahali mia moja, kondoo dume mia mbili, wana-kondoo mia nne, sadaka kwa ajili ya dhambi ya Israeli yote walitoa mbuzi dume kumi na wawili, mmoja kwa ajili ya kila kabila la Israeli.
18 They organized the priests and Levites by their divisions to serve God in the Temple at Jerusalem, in accordance with the Book of Moses.
Wakawaweka makuhani katika nafasi zao na Walawi wakawekwa katika makundi yao ya huduma kwa Mungu huko Yerusalemu, kulingana na ilivyoandikwa katika Kitabu cha Mose.
19 The exiles who had returned observed the Passover on the fourteenth day of the first month.
Katika siku ya kumi na nne ya mwezi wa kwanza, waliorudi kutoka uhamishoni wakaadhimisha Pasaka.
20 The priests and Levites had all purified themselves so that they were clean according to the ceremonial law. So they killed the Passover lamb for all the exiles who had returned, for their fellow priests, and for themselves.
Makuhani na Walawi walikuwa wamekwisha kujitakasa nao wamekuwa safi kwa kufuata kawaida za ibada. Walawi wakachinja kondoo wa Pasaka kwa ajili ya wana wa waliorudi kutoka utumwani uhamishoni, kwa ajili ya ndugu zao makuhani na wao wenyewe.
21 The Passover was eaten by the people of Israel who had returned from exile, and by those who had joined them and had rejected the pagan practices of the peoples of the land in order to worship the Lord, the God of Israel.
Hivyo Waisraeli waliokuwa wamerudi kutoka utumwani uhamishoni wakaila Pasaka, pamoja na wale waliokuwa wamejitenga na matendo ya unajisi wa Mataifa ya jirani ili kumtafuta Bwana, Mungu wa Israeli.
22 Then they observed the Festival of Unleavened Bread for seven days. Everyone throughout the land was so happy because the Lord had made the king of Assyria favorable to them, helping them to rebuild the Temple of God, the God of Israel.
Kwa muda wa siku saba waliiadhimisha Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu kwa furaha, kwa sababu Bwana alikuwa amewajaza furaha kwa kubadilisha nia ya mfalme wa Ashuru kwamba awasaidie ujenzi wa nyumba ya Mungu, Mungu wa Israeli.

< Ezra 6 >