< Ezekiel 46 >
1 This is what the Lord God says: “The east gate of the inner court is to be kept shut during the six working days, but it shall be opened on the Sabbath and on the day of the New Moon
“‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Lango la ukumbi wa ndani linaloelekea upande wa mashariki litakuwa linafungwa kwa siku sita za juma, ila siku ya Sabato na siku ya Mwezi Mwandamo litafunguliwa.
2 The prince must come through the gateway porch from outside and he will stand by the gatepost, and the priests will sacrifice his burnt offerings and peace offerings. He is to bow in respect at the gate's threshold of the gate and leave, but the gate is not to be shut until evening.
Mkuu anayetawala ataingia kupitia baraza ya njia ya lango la ukumbi na kusimama karibu na nguzo ya lango. Makuhani watatoa sadaka za mkuu anayetawala za kuteketezwa na sadaka za amani. Mkuu anayetawala atasujudu kwenye kizingiti cha njia ya lango, kisha atatoka nje, lakini lango halitafungwa mpaka jioni.
3 The people of Israel will also bow before the Lord at the gateway entrance on Sabbaths and New Moons.
Siku za Sabato na za Mwezi mwandamo watu wote wa nchi wataabudu mbele za Bwana penye lile ingilio la ile njia.
4 The burnt offering that the prince is to offer to the Lord on the Sabbath day shall be six male lambs and a ram, all without defects.
Sadaka ya kuteketezwa aletazo mkuu anayetawala kwa Bwana siku ya Sabato itakuwa ni wana-kondoo sita na kondoo dume mmoja, wote wasiwe na dosari.
5 The grain offering to accompany the ram shall be one ephah, and the grain offering with the lambs shall be as much as he chooses, together with a hin of olive oil for every ephah of grain.
Sadaka ya nafaka inayotolewa pamoja na huyo kondoo dume itakuwa efa moja na sadaka ya nafaka inayotolewa na hao wana-kondoo itakuwa kiasi apendacho mtu pamoja na hini ya mafuta kwa kila efa.
6 On the day of the New Moon he is to offer a young bull, six lambs, and a ram. They are all to be without defects.
Siku ya mwezi mwandamo atatoa fahali mchanga, wana-kondoo sita na kondoo dume, wote wasiwe na dosari.
7 He is also to provide a grain offering of an ephah with the bull, an ephah with the ram, and as much as he is chooses with the lambs, together with a hin of olive oil for every ephah of grain.
Atatoa kuwa sadaka ya nafaka efa moja pamoja na fahali mmoja, efa moja na kondoo dume mmoja na pamoja na wana-kondoo kama atakavyo kutoa, pamoja na hini ya mafuta kwa kila efa.
8 When the prince enters, he is to come in through the gateway porch, and leave the same way.
Wakati mkuu anayetawala aingiapo, atapitia kwenye baraza ya njia ya lango, naye atatoka nje kwa njia hiyo hiyo.
9 When the people of Israel gather before the Lord at the regular religious festivals, anyone who enters through the north gate to worship has to leave through the south gate, and anyone who enters through the south gate leave through the north gate. No one is allowed to go back through the same gate through which they entered. Everyone must leave by the opposite gate.
“‘Wakati watu wa nchi wanapokuja mbele za Bwana katika sikukuu zilizoamriwa, yeyote aingiaye kwa lango la kaskazini kuabudu atatoka nje kwa lango la kusini na yeyote aingiaye kwa lango la kusini atatoka nje kwa lango la kaskazini. Hakuna mtu yeyote atakayerudi kwa kupitia lango lile aliloingilia, lakini kila mmoja atatoka nje kwa lango linalokabili lile aliloingilia.
10 The prince is to enter when the people do; and leave when they leave.
Mkuu anayetawala atakuwa miongoni mwao, akiingia nao ndani wanapoingia, naye atatoka nao nje wanapotoka.
11 At the religious festivals and regular meetings, the grain offering will be an ephah with a bull, an ephah with a ram, and as much as people choose with the lambs, together with a hin of olive oil for every ephah of grain.
“‘Kwenye sikukuu na kwenye sikukuu zilizoamriwa, sadaka ya nafaka itakuwa efa moja pamoja na fahali mmoja, efa moja pamoja na kondoo dume mmoja, pamoja na idadi ya wana-kondoo kama mtu apendavyo kutoa, pamoja na hini ya mafuta kwa kila efa.
12 When the prince decides to make a freewill offering to the Lord, whether it's a burnt offering or a peace offering, the east gate is to be opened for him. He shall offer his burnt offering or peace offering in the same way he does on the Sabbath. When he leaves, the gate must be closed after him.
Mkuu anayetawala anapotoa sadaka ya hiari kwa Bwana, ikiwa ni sadaka ya kuteketezwa au sadaka ya amani, lango linaloelekea mashariki litafunguliwa kwa ajili yake. Atatoa sadaka yake ya kuteketezwa au sadaka yake ya amani kama afanyavyo katika siku ya Sabato. Kisha atatoka nje, naye akiisha kutoka nje, lango litafungwa.
13 Every morning a year-old lamb without defects is to be sacrificed as a daily burnt offering to the Lord.
“‘Kila siku utamtoa mwana-kondoo wa mwaka mmoja asiyekuwa na dosari kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa kwa Bwana, utaitoa kila siku asubuhi.
14 Every morning a grain offering of a sixth of an ephah with a third of a hin of olive oil to moisten the best flour is to be provided as a grain offering to the Lord. This regulation is to be followed forever.
Pia kila siku asubuhi pamoja na hiyo sadaka utatoa sadaka ya nafaka, ikiwa na sehemu ya sita ya efa pamoja na theluthi moja ya hini ya mafuta ya kuchanganya na ule unga. Utoaji wa sadaka hii ya nafaka kwa Bwana ni amri ya daima.
15 Make sure the lamb, the grain offering, and the olive oil is presented every morning as a regular burnt offering.
Kwa hiyo mwana-kondoo na sadaka ya nafaka na mafuta vitatolewa kila siku asubuhi kwa ajili ya sadaka ya daima ya kuteketezwa.
16 This is what the Lord God says: If the prince gives a gift of property to any of his sons to own, it will belong to his descendants. They will be able to inherit the property.
“‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ikiwa mkuu atawalaye atatoa zawadi kutoka kwenye urithi wake na kumpa mmoja wa wanawe, hiyo zawadi itakuwa pia kwa wazao wake, itakuwa mali yao kwa urithi.
17 However, if he gives a gift of his property to one of his servants, that servant will only own it until the Jubilee Year. Then ownership will return to the prince. His property that he passes on through inheritance belongs only to his sons—it is theirs.
Hata hivyo, kama atatoa zawadi kutoka urithi wake na kumpa mmoja wa watumishi wake, mtumishi anaweza kuiweka mpaka mwaka wa uhuru, kisha itarudishwa kwa mkuu anayetawala. Urithi wake ni wa wanawe peke yao, ni mali yao.
18 The prince is not to take people's land, driving them off their property. He is to give land to his sons from his own property, so that none of my people shall be evicted from their property.”
Mkuu anayetawala hana ruhusa kuchukua urithi wowote wa watu na kuwaondoa kwenye mali zao. Mkuu atawalaye atawapa wanawe urithi wao, kutoka kwenye mali zake mwenyewe, ili kwamba pasiwe na mtu wangu yeyote atakayetengwa na urithi wake.’”
19 The man took me through the entrance beside the gate into the north-facing holy rooms that belonged to the priests. He showed me a place at the far western end
Kisha mtu yule akanileta kwa kupitia kwenye ingilio lililokuwa kando ya lango mpaka kwenye vyumba vitakatifu vinavyoelekea kaskazini, ambavyo ni vya makuhani, naye akanionyesha mahali fulani upande wa mwisho wa magharibi.
20 and told me, “This is where the priests cook guilt offerings and sin offerings, and where they bake the grain offering. This is so that they don't take them to the outer courtyard and carry holiness to the people.”
Akaniambia, “Mahali hapa ndipo makuhani watakapotokosea sadaka ya hatia na sadaka ya dhambi na kuoka sadaka ya nafaka, kuepuka kuzileta katika ukumbi wa nje na kushirikisha utakatifu kwa watu.”
21 He took me into the outer courtyard and led me to each of its four corners. I saw a separate courtyard in each corner.
Baada ya hapo akanileta kwenye ukumbi wa nje na kunizungusha kwenye pembe zake nne, nami nikaona katika kila pembe ya huo ukumbi kulikuwa na ukumbi mwingine.
22 There were separate walled courtyards in the four corners of the outer courtyard. They each measured forty cubits by thirty cubits—they were all the same size.
Katika pembe nne za huo ukumbi wa nje kulikuwa na kumbi nyingine, zenye urefu wa dhiraa arobaini na upana wake dhiraa thelathini, ambapo hizo kumbi kwenye hizo pembe nne zilikuwa na vipimo vilivyo sawa.
23 Each of the four courts had a stone ledge with ovens built into the base of the walls on every side.
Mzunguko wa ndani wa hizo kumbi nne ulikuwa na ukingo wa jiwe, zikiwa na sehemu zilizojengwa kwa ajili ya moto kuzunguka chini ya huo ukingo.
24 He told me, “These are the kitchens where those who serve in the Temple will cook the people's sacrificial offerings.”
Akaniambia, “Hizi ndizo sehemu za kupikia ambazo wale wanaohudumu kwenye Hekalu watatokosea dhabihu za watu.”