< Ezekiel 39 >

1 “Son of man, prophesy against Gog and announce that this is what the Lord God says: Watch out, because I'm condemning you Gog, chief prince of Meshech and Tubal.
“Kisha wewe, mwanadamu, tabiri dhidi ya Gogu na sema, 'Bwana Yahwe asema hivi: Tazama! ni kinyume nawe, Gogu, mkuu wa Mesheki na Tubali.
2 I will send you in a different direction, drag you along, bring you from the distant places of the north, and send you to attack the mountains of Israel.
Nitakugeuza na kukuongoza; nitakupandisha juu kutoka mbali kaskazini na kukuleta hata milima ya Israeli.
3 Then I will knock the bow out of your left hand and make you drop the arrows from your right hand.
Kisha nitaufunga upinde wako utoke katika mkono wako wa kushoto na kuifanya mishale kuanguka kutoka kwenye mkono wako wa kuume.
4 You will be killed on the mountains of Israel, you and your whole army and armies of your allies. I will provide you as food to all kinds of flesh-eating birds and animals.
Utaanguka juu ya milima ya Israeli-wewe na jeshi lako late na maaskari walio pamoja nawe. Nitawapatia ndege mbua na wanyama pori wa mashambani kwa ajili ya chakula.
5 You will fall and die out in the open, for I have spoken, declares the Lord God.
Utaanguka juu ya uso wa shamba, kwa kuwa mimi mwenyewe nimesema hivyo-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.
6 I will set Magog on fire, as well as the coastlands where people think it's safe to live, and then they will acknowledge that I am the Lord.
Kisha nitapeleka moto juu ya Magogu na kwa wale waishio salama juu ya pwani, na watajua yakwamba mimi ni Yahwe.
7 In this way I will make my reputation for holiness known among my people Israel and won't allow it to be ruined anymore. Then the nations will acknowledge that I am the Lord, the Holy One of Israel.
Kwa kuwa nitalifanya jina langu takatifu lijulikane kati ya watu wangu Israeli, na sitaruhusu tena jina langu takatifu litukanwe; mataifa watajua kwamba mimi ni Yahwe, Mtakatifu katika Israeli.
8 Yes, it's coming! It will definitely happen, declares the Lord God. This is the day that I have spoken about.
Tazama! Siku inakuja, na itachukua nafasi-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.
9 Then those living in the towns of Israel will go out to light fires and burn the weapons—the large and small shields, the bows and arrows, the clubs and spears. They will use the weapons to make fires for seven years.
Hao wakaao katika miji ya Israeli watatoka nje na watatumia silaha kuwasha moto na kutengeneza moto na kuwachoma-ngao ndogo, ngao kubwa, pinde, mishale, rungu, na mikuki; watatengeneza mioto pamoja nao kwa muda wa siku saba.
10 They won't need to go and gather firewood from the countryside or cut it from the forests, because they'll use the weapons to make fires. They will loot and plunder those who looted and plundered them, declares the Lord God.
Hawatakusanya kuni kutoka mashambani wala kukata miti kutoka kwenye misitu, kwa kuwa watazichoma hizo silaha; watawateka nyara wale watakaotaka kuwateka nyara-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.”
11 At that time I will give Gog a place to be buried in Israel, the Travelers' Valley, east of the Sea. People won't be able to travel through because all his army will be buried there. So it will be called the Valley of Gog's Army.
Kisha itakuwa katika hiyo siku ambayo nitaifanya sehemu huko kwa ajili ya Gogu-kaburi la Israeli, bonde kwa ajili ya wale wanaosafiri hata mashariki ya bahari. Litawazuia wale wanaotegemea kupita. Huko watamzika Gogu pamoja na kundi lake lote. Watapaita bonde la Hamon-Gogu.
12 It will take the people of Israel seven months to bury them in order to make the country clean.
Kwa muda wa siku saba nyumba ya Israeli itawazika ili kuitakasa nchi.
13 Everyone in the country will be involved in burying them, and this will give them a good reputation when I reveal my glory, declares the Lord God.
Kwa kuwa watu wa nchi watawazika; itakuwa siku ya kukumbukwa kwao wakati nitakapotukuzwa-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.
14 Men will be chosen to go repeatedly through the country to make it clean it by burying the bodies of the invaders that are still left lying the ground. They will start doing this at the end of the seven months.
Kisha watawateua watu kuendelea kwenda kwenye nchi, kuwatafuta wale waliokuwa wakisafiri, lakini waliokufa na miili yao kubaki juu ya uso wa nchi, ili kwamba waweze kuwazika, kwa ajili ya kusafisha nchi. Katika siku ya mwisho ya mwezi wa saba wataanza kutafuta.
15 As they search the country, if they find a human bone they will place a marker next to it so that those in charge of burials can have it buried in the Valley of Gog's Army.
Kama hawa watu wapitao kwenye nchi, watakapoona mfupa wowote wa binadamu, wataweka alama kwa huo, hadi wachimba kaburi watakapokuja na kuizika katika bonde la Hamoni Gogu.
16 Even the town there will be named Hamonah. In this way they will make the country clean.
Kutakuwa na mji huko unaitwa Hamona. Wataitakasa nchi kwa njia hii.
17 Son of man, this is what the Lord God says: Call out to every kind of flesh-eating bird and wild animal: Come from everywhere around and gather for the sacrifice I'm going to prepare for you, a great sacrificial feast on the mountains of Israel where you'll have flesh to eat and blood to drink.
Kwako wewe, mwanadamu, Bwana Yahwe asema hivi: Waambie ndege wote wenye mabawa na wanyama wote wa porini katika mashamba, 'Kusanyikeni pamoja na mje. Kusanyikeni kutoka pande zote kwenda kwenye dhabihu yote ambayo mimi mwenyewe ninayoifanya kwa ajili yako, dhabihu kubwa juu ya milima ya Israeli, ili kwamba mle nyama na kunywa damu.
18 You will eat the flesh of the powerful and drink the blood of the world's leaders just as if they were rams, lambs, goats, and bulls—all the fattened animals that come from Bashan.
Mtakula nyama ya walio hodari na kunywa damu ya wakuu wa dunia; watakuwa kondoo waume, wana kondoo, mbuzi, na ng'ombe, wote walikuwa wanene katika Basheni.
19 You will eat fat until you are totally full and drink blood until you are drunk at the sacrifice I'm going to prepare.
Kisha mtakula mafuta hata kuridhika kwenu; mtakunywa damu hadi kulewa; hii itakuwa dhabihu nitakayoichinja kwa ajili yenu.
20 You will eat at my table until you're full, consuming horses and riders, powerful men and all kinds of warriors, declares the Lord God.
Mtatosheka kwenye meza yangu pamoja na farasi, magari ya farasi, shujaa, na kila mtu wa vita-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.'
21 I will reveal my glory to the other nations, and all of them will see the punishment I hand out to them.
Nitauweka utukufu wangu kati ya mataifa, na mataifa yote yataona hukumu yangu ninayoionyesha na mkono wangu nimeuweka juu yao.
22 From that time on the people of Israel will know that I am the Lord their God.
Nyumba ya Israeli itajua yakwamba mimi ni Yahwe Mungu wao kutoka hiyo siku na kuendelea.
23 The nations will realize that the people of Israel were taken prisoner because of their sins, because they were unfaithful to me. So I gave up on them and handed them over to their enemies, so that they were all killed by the sword.
Mataifa yatajua kwamba nyumba ya Israeli wameenda uhamishoni kwa sababu ya udhalimu wao kwa kunisaliti, hivyo naficha uso wangu kwao na kuwaweka kwenye mkono wa maadui zao ili kwamba wote waanguke kwa upanga.
24 I dealt with them because of their uncleanness and sins, and I gave up on them.
Nimewafanyia kutokana na uchafu wao na dhambi zao, nitakapokuwa nimeuficha uso wangu kwao.
25 So this is what the Lord God says: Now I will bring back the descendants of Jacob from exile and I will show mercy to all the people of Israel, and I will demonstrate my reputation for holiness.
Kwa hiyo Bwana Yahwe asema hivi: Sasa nitawarudisha watu wa Yakobo, na kuwa na huruma juu ya nyumba yote ya Israeli, wakati nitakapoona wivu kwa ajili ya jina langu.
26 They will forget their shameful actions and all the ways they were unfaithful to me once they live in safety in their country, with no one to threaten them.
Kisha watabeba aibu yao na uhaini mkubwa walio nihaini. Watayasahau haya yote watakapopumzika katika nchi yao katika usalama, wala hakuna mtu atakaye waogofya.
27 When I bring them home from the nations, gathering them from the countries of their enemies, I will reveal my holiness among as many nations watch.
Wakati nitakapokuwa nimewarudisha kutoka kwa watu na kuwakusanya kutoka kwenye nchi za maadui zao, nitajionyesha mimi mwenyewe kuwa mtakatifu kwenye uso wa mataifa mengi.
28 Then they will know that I am the Lord their God, when I bring them home to their own country again, not leaving any of them behind.
Kisha watajua kwamba mimi ni Yahwe Mungu wao, kwa kuwa nimewapeleka utumwani kati ya mataifa, lakini kisha nitawakusanya kuwarudisha hata nchi yao. Sitamuacha hata mmoja wao kati ya mataifa.
29 I won't give up on them anymore, for I will fill the people of Israel with my Spirit, declares the Lord God.”
Sitawaficha uso wangu kwao wakati nitakapomwaga Roho wangu katika nyumba ya Israeli-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.”

< Ezekiel 39 >