< Ezekiel 33 >

1 A message from the Lord came to me, saying,
Kisha neno la Yahwe likanijia, kusema,
2 “Son of man, tell your people: If I brought an army to attack a country, the people there would choose one of them to be their watchman.
“Mwanadamu, sema hivi kwa watu wako; waambie, 'Nitakapoleta upanga juu ya nchi, kisha watu wa hiyo nchi wakamchukua mtu mmoja kutoka mingoni mwao na kumfanya awe mlinzi wao.
3 When he saw the army advancing to attack the country, he would blow the trumpet to warn everyone.
Atazamapo kwa upanga kama unakuja juu ya nchi, na apige tarumbeta kuwaonya watu!
4 So if you hear the trumpet but don't pay attention to the warning, and you're killed in the attack, you will be responsible for your own death.
Kama watu wakisikia sauti ya tarumbeta lakini bila kusikia, na kama upanga ukija na kuwaua, kisha damu ya kila mmoja iko juu ya kichwa chake mwenyewe.
5 Since you heard the trumpet but didn't pay attention to the warning, then you will be responsible for your own death. If you had paid attention the warning, you could have saved your life.
Kama mtu akisikia sauti ya tarumbeta na hakusikiliza, damu yake iko juu yake; lakini kama akisikia, ataokoa maisha yake mwenyewe.
6 But if the watchman saw the attack coming and didn't blow the trumpet to warn everyone, and someone is killed, then that person will die in their sins, but I will hold the watchman responsible for their death.
Bali, kama mlinzi akiona upanga unakuja, lakini kama asipopiga tarumbeta, pamoja na matokeo kwamba watu hawajaonywa, na kama upanga ukija na kuchukua uhai wa mtu yeyote, kisha yule mtu akafa kwenye dhambi yake mwenyewe, lakini nitaitaka damu yake kutoka mlinzi.'
7 Son of man, I have appointed you as a watchman for the people of Israel. Listen to what I tell you and warn them for me.
Sasa wewe mwenyewe, mwanadamu! Nimekufanya kuwa mlinzi kwa ajili ya nyumba ya Israeli; utasikia maneno kutoka kinywani mwangu na uwaonye badala yangu.
8 If I tell the wicked ‘You're wicked; you're going to die’; but you don't warn them to change what they're doing, then they'll die in their sins and I will hold your responsible for their deaths.
Kama nikimwambia mtu mwovu, 'Mwovu, hakika utakufa!' lakini kama hutangazi hivi ili kwa ajili ya kumuonya mtu mwovu kuhusu hii njia, kisha huyo mtu mwovu atakufa katika dhambi yake, lakini nitaitaka damu yake kutoka kwenye mkono wako!
9 But if you warn the wicked to change what they're doing, and they don't, they will die in their sins, but you will save your own life.
Lakini wewe, kama ukimwonya mwovu kuhusu hii njia, hivyo basi anaweza kurudi kutoka hiyo, na kama kama asipogeuka kutoka njia yake, kisha atakufa katika dhambi yake, lakini wewe mwenyewe utakuwa umeokoa maisha yako.
10 Son of man, tell the people of Israel that this is what they've been saying, ‘We recognize our sins and wrongs, and they weigh on us, wearing us out. How can we go on living?’
Basi wewe, mwanadamu, sema kwa nyumba ya Israeli, 'Mnasema hivi, Makosa yetu na dhambi zetu zi juu yetu, na tunadhoofika kwa ajili yao! Je! tutaishije?”'
11 Tell them: As I live, declares the Lord God, it brings me no pleasure when wicked people die. I wish they would stop sinning and live! Stop! Stop sinning! Why should you die, people of Israel?
Waambie, 'Kama niishivyo-asema Bwana Yahwe-sifurahii kifo cha mwovu, kwa kuwa kama mwovu akitubu kutoka njia yake, kisha ataishi! Tubu! Tubu kutoka njia zako mbaya! Kwa nini mnataka kufa, nyumba ya Israeli?'
12 So, son of man, tell your people: All the good things a good person has done won't save them when they sin; while the bad things a bad person has done won't be a problem for them if they stop sinning. But good people won't live if they start sinning.
Hivyo basi wewe, mwanadamu, waambe watu wako, 'Haki ya mwenye haki haitamwokoa kama akikosa! Uovu wa mtu mwovu hautamfanya kuangamia kama akitubu dhambi zake! Kwa kuwa mtu mwenye haki hataweza kuishi kwa sababu ya haki yake kama akikosa.
13 If I tell a good person that they will live and then they rely on their goodness and start sinning, then none of the good things they did will be remembered; he will die because of the sins.
Kama nikisema kwa mwenye haki, “Hakika ataisha!” na kama akiamini katika haki yake na kisha akafanya udhalimu, sitokumbuka haki yake yoyote. Atakufa kwa ajili ya uovu alioufanya.
14 But if I tell a bad person, ‘You're going to die’ and they stop sinning and do what is good and right,
Hivyo kama nikisema kwa mwovu, “Utakufa hakika,” lakini kama akitubu kutoka kwenye dhambi zake na kufanya yaliyo halali na haki-
15 if they return security given for a loan, pay back what they've stolen, and follows my laws about how to live, not doing wrong—then they will live; they won't die.
kama akirudisha dhamana ambayo aliyomnyang'anya, au kama akirudisha alichokipoteza, na kama akitembea katika amri zitoazo uhai na bila kufanya dhambi-kisha ataishi hakika. Hatakufa.
16 None of their sins will be remembered; they have done what is good and right and so they will live.
Dhambi alizozifanya hazitakumbukwa kwa ajili yake. Ametenda halali na haki, na hivyo, ataishi hakika!
17 However, your people are complaining, ‘What the Lord does isn't right.’ But it's what they're doing that isn't right.
Lakini watu wako husema, “Njia ya Bwana haiko sawa!” lakini ni njia zako ndizo haziko sawa!
18 If a good person stops doing good and sins, they will die because of it.
Wakati mtu mwenye haki ageukapo kutoka kwenye haki na kufanya dhambi, kisha atakufa katika hiyo!
19 On the other hand, if a bad person turns from their sins and they do what is good and right, they will live as a result.
Wakati mtu mbaya ageukapo kutoka kwenye ubaya wake na kufanya iliyo halali na haki, ataishi kwa sababu ya hayo mambo!
20 So how can you say, ‘What the Lord does isn't right’? Well, I'm going to judge each of you depending on what you've done, people of Israel.”
Lakini ninyi watu husema, “Njia ya Bwana haiko sawa!” Nitawahukumu kila mmoja wenu kulingana na njia yake, nyumba ya Israeli!”'
21 On the fifth day of the tenth month of the twelfth year of our exile, a refugee who'd escaped from Jerusalem arrived and told me, “The city has been captured!”
Ikawa katika mwaka wa kumi na mbili, siku ya tano ya mwezi wa kumi ya uhamisho wetu, mtu mmoja akatoroka kutoka Yerusalemuna kusema, “Mji umetekwa!”
22 The previous evening before the messenger arrived the Lord had touched me so I could speak again. This was before the man came to see me in the morning. I wasn't mute any longer—I could speak again.
Mkono wa Yahwe ulikuwa juu yangu jioni kabla yule mtoro hajaja, na mdomo wangu ulikuwa wazi mda huo alikuja kwangu wakati wa mapambazuko. Hivyo mdomo wangu ulikuwa wazi; sikuwa bubu tena!
23 A message from the Lord came to me, saying,
Kisha neno la Yahwe likanijia, kusema,
24 “Son of man, people living among the ruins in Israel are saying, ‘Abraham was only one man, but the country was given to him to own. There's plenty of us, so the country should belong to us.’
“Mwanadamu, wale waishio mahali palipoharibika katika nchi ya Israeli huongea na kusema, 'Ibrahimu alikuwa mtu pekee, na alirithi nchi, lakini sisi tukowengi! Tumepewa nchi kama wamiliki.”
25 So tell them that this is what the Lord God says: You eat meat with the blood still in it. You go and worship your idols. You commit murder. Do you really think the country should belong to you?
Kwa hiyo waambie, 'Bwana Yahwe asema hivi: Mnakula damu, na mmeziinulia macho yenu sanamu, kisha mnazimwagia damu za watu. Je! mna uhakika wa kuimiliki hii nchi?
26 You rely on your swords to get your way. You have done some disgusting things. You're all having sex with each other's wives. Should the country belong to you?
Mnategemea upanga wenu na mmetenda mambo maovu; kila mtu amemnajisi mke wa jirani yake. Je! kweli mtaimiliki nchi?'
27 Tell them that this is what the Lord God says: As I live, in the people living among the ruins will be killed by the sword. Those living in the countryside will be eaten by wild animals. Those living in the fortresses and caves will die from disease.
Utawaambia hivi, 'Bwana Yahwe asema hivi: Kama niishivyo, hakika wale walio katika uharibifu wataanguka kwa upanga, na nitawapatia wale walio katika mashamba viumbe hai kama chakula, na wale walio katika ngome na mapango watakufa kwa tauni.
28 I will turn the country into a wasteland, and power you are so proud of will be ended. The mountains of Israel will become wild places that no one will want to travel through.
Kisha nitairudisha nchi kwenye ukiwa na tishio, na kiburi cha uwezo wake kitakoma, kwa kuwa milima ya Israeli itakuwa jangwa, na hakutakuwa na mtu yeyote atakayewapitia.'
29 Then the people will acknowledge that I am the Lord, when I have turned the country into a wasteland because of all the disgusting things they have done.
Hivyo watajua kwamba mimi ni Yahwe, nitakapoifanya nchi ukiwa na tishio kwa sababu ya machukizo yote waliyoyafanya.
30 Son of man, your people are talking about you out in the streets and in the doorways of their houses. They encourage one another, saying, ‘Come on! Let's go and hear a message from the Lord!’
Hivyo basi wewe, mwanadamu-watu wako wanasema mambo yako karibu na kuta na malango ya nyumba, na kila mmoja anaambizana na mwenzake-kila mtu na ndugu yake, 'Twende na tukasikilize neno la nabii lililotoka kwa Yahwe!
31 So my people come and visit you like they usually do. They sit and listen to the message you share, but they don't do anything about it. Even though they talk about love, all they're thinking about is how to cheat others.
Hivyo watu wangu watakuja kwako, kama wafanyavyo mara nyingi, na nitaketi mbele yako na kusikiliza maneno yako, lakini mioyo yao inafuata udhalimu kwa faida yao.
32 In fact, to them you're just someone who sings love songs with a lovely voice and who is a fine musician. They listen to the message you share, but they don't do anything about it.
Kwa kuwa umekuwa kama wimbo mzuri kwao, sauti nzuri awezaye kucheza kinanda vizuri, hivyo watasikia maneno yako, lakini hakuna atakaye yatii.
33 So when what you say does happen (and it will), then they will realize that they did have a prophet among them.”
Hivyo wakati haya yote yatakapotokea-tazama! itatokea! -watajua yakwamba nabii alikuwa miongoni mwao.”

< Ezekiel 33 >