< Ezekiel 13 >

1 A message from the Lord came to me, saying,
Tena, neno la Yahwe likanijia, kusema,
2 “Son of man, you are to prophesy against the prophets of Israel who right now are busy prophesying. Tell those who make up their own prophecies: Listen to the word of the Lord!
“Mwanadamu, tabiri dhidi ya manabii wanaotabiri katika Israeli, na uwaambie wale wanotabiri nje ya fikra zao wenyewe, 'Lisikilizeni neno la Yahwe.
3 This is what the Lord God says: Disaster is coming to these foolish prophets who follow their own ideas. They haven't seen anything.
Bwana Yahwe asema hivi: Ole wao manbii wajinga ambao wafwatao roho zao wenyewe, lakini wale wasioona kitu!
4 Israel, your prophets are like foxes that live in the ruins.
Israeli, manabii zako wamekuwa kama mbeha kwenye aridhi iliyoharibiwa na vita.
5 They didn't go and help repair the gaps in the wall that defends the people of Israel so that it would stand secure during the battle on the Day of the Lord.
Hamkwenda kwenye nyufa katika ukuta uliozunguka nyumba ya Israeli kwa ajili ya kuukarabati, ili kupigana katika vita katika siku ya Yahwe.
6 The visions they see are false, and the prophecies they give are lies. They claim, ‘This is what the Lord says,’ when the Lord didn't send them. Even so they still expect their message to be fulfilled!
Watu wameona uongo na kufanya utabiri wa uongo, wale wasemao, “Hivi na hivi ndvyo Yahwe asemavyo.” Yahwe hajawatuma, lakini hata hivyo wamewafanya watu kutumaini kwamba ujumbe wao utakuwa kweli.
7 Isn't it a false vision that you people saw? Isn't it a prophecy of lies when you announce, ‘This is what the Lord says,’ even though I haven't said anything?
Je hamkusikia maono ya uongo na kufanya utabiri wa uongo, ninyi msemao, “Hivi na hivi ndivyo Yahwe asemavyo” Wakati mimi mwenyewe sikuongea?'
8 So this is what the Lord God says: Since you've spoken lies and claimed to see false visions, then watch out, because I'm against you, declares the Lord God.
Kwa hiyo Bwana Yahwe asema hivi, 'Kwa sababu mmesikia maono ya uongo na kuwaambia uongo-kwa hiyo hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo dhidi yenu:
9 I will punish the prophets who see false visions and give prophecies that are lies. They will not belong to the assembly of my people or be listed in the register of Israelites, and they won't be allowed to enter the country of Israel. Then you will know that I am the Lord God.
Mkono wangu utakuwa juu yenu ninyi manabii mliodanganya maono na wale waliofanya unabii wa uongo. Hawatakuwepo kwenye kusanyiko la watu wangu, au kuandikishwa katika kumbukumbu ya nyumba ya Israeli; hawataenda kwenye nchi ya Israeli. Kwa kuwa mtajua yakwamba mimi ni Bwana Yahwe!
10 They have deceived my people by saying, ‘We shall have peace,’ when there won't be any peace. It's like they're putting a coat of whitewash on an unstable wall of loose stones that the people have built.
Kwa sababu hiyo, na kwa sababu wamewaongoza watu wangu kuwapotosha na kusema, “Amani!” wakati hakuna amani, wanajenga ukuta ambao wataupaka rangi ya chokaa.'
11 So tell those people whitewashing the wall that it's going to collapse. Rain will come pouring down. I will send hailstones crashing down on it. A windstorm will blow hard against it.
Waambie wale wanaopaka chokaa ukuta, 'Utaanguka chini; kutakuwa na mvua ya kufurika, na nitaleta mvua ya mawe kuufanya uanguke chini, na upepo wa dhoruba kupuliza hata kuuvunja chini.
12 Don't you think that when the wall collapses people are going to ask you, ‘What happened to the whitewash you painted it with?’
Tazama, ukuta utaanguka chini. Je wengine hawakuwaambia, “Iko wapi chokaa mliyoipaka juu yake?”
13 So this is what the Lord God says: In my furious anger I'm going to send a windstorm, pouring rain, and hailstones to destroy the wall.
Kwa hiyo Bwana Yahwe asema hivi: Nitaleta upepo wa dhoruba katika ghadhabu yangu, na kutakuwa na mafuriko ya mvua kwenye ghadhabu yangu! Mvua ya mawe katika ghadhabu yangu itauharibu kabisa.
14 I will demolish the wall you whitewashed, knocking it to the ground to reveal its foundations. The city is going to fall, and you're going to be destroyed with it. Then you will know that I am the Lord.
Kwa kuwa nitaurarua chini ukuta ambao mlioufunika kwa chokaa, na nitaubomoa hata kwenye nchi na kuifunua misingi yake. Hivyo utaanguka, nanyi nyote mtaangamizwa katikati ya huo.
15 Once the wall and those who whitewashed it have experienced my anger, I will tell you: The wall is no more, and those who whitewashed it are no more,
Ndivyo nitakavouangamiza kwa ghadhabu yangu ukuta na wale walioupaka chokaa. Nitawaambia, “Ukuta hautaonekana tena, wala watu wanaoupaka chokaa-
16 those ‘prophets’ of Israel who prophesied to Jerusalem and claimed to have seen a vision of peace for her when there wasn't going to be any peace, declares the Lord God.
manabii wa Israeli wale waliotabiri kuhusu Yerusalemu na wale waliokuwa wameona amani kwa ajili yake. Lakini hakuna amani! -hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.”
17 Now, son of man, you are to oppose those Israelite women who make up prophecies in their own minds. Prophesy against them
Hivyo wewe, mwanadamu, weka uso wako dhidi ya binti za watu wako wale wanaotabiri kwa akili zao wenyewe, na kutabiri dhidi yao.
18 and tell them that this is what the Lord God says: Disaster is coming to the women who sew bracelets of magic charms for their wrists and make veils for all kinds of people to wear as ways to trap and exploit them. Do you think you can trap the lives of my people yet still keep your own?
Sema, 'Bwana Yahwe asema hivi: Ole kwa wanawake washonao hiziri kwenye kila sehemu ya mkono wao na kutengeza vitambaa vya shela kwa ajili ya vichwa vyao kwa kila kipimo, ili kuwinda watu. Je mtawawinda watu wangu ila kuokoa maisha yenu wenyewe?
19 You have disgraced me among my people for a few handfuls of barley and scraps of bread. By lying to my people who believe in you, you have killed those who shouldn't have died and let others live who shouldn't.
Ninyi mmenikufuru mbele ya watu wangu kwa ajili ya makonzi ya shayiri na vipande vya mkate, kuwaua watu ambao hawakutakiwa kufa, na kuyalinda maisha ya wale ambao hawatakiwi kuendelea kuishi, kwa sababu ya uongo wenu kwa watu wangu walio wasikiliza.
20 So this is what the Lord God says: Watch out! I condemn the magic charms you use to trap people like birds, and I will rip them off your arms. I will set free those you have trapped.
Kwa hiyo Bwana Yahwe asema hivi: Niko kinyume dhidi ya hirizi ambazo mlizozitumia kuyakamata kwa hila maisha ya watu kana kwamba wamekuwa ndege. Naam, nitazichana kutoka kwenye mikono yenu; na wale watu mlio watega kama ndege-nitawaacha waende huru.
21 I will also rip off your veils and rescue my people from your power, so that they will no longer be your victims. Then you will know that I am the Lord.
Nitavichana mbali vitambaa vya shela na kuwaokoa watu wangu kutoka kwenye mikono yangu, kwa hiyo hawatategwa tena kwenye mikono yenu. Mtajua kwamba mimi ni Yahwe.
22 Because you have discouraged good people with your lies, even though I didn't have anything against them, and because you have encouraged the wicked that they shouldn't give up from their evil ways to save their lives,
Kwa sababu mmeuvunja moyo wa mtu mwenye haki kwa uongo, ingawa hata mimi sikutamani kuvunjwa kwake moyo, na kwa sababu mmemtia moyo badala yake matendo ya mtu mwovu ili kwamba asitaweze kurudi kutoka kwenye njia yake kuokoa maisha yake-
23 from now on you won't claim these false visions or practice magic. I will rescue my people from your power. Then you will know that I am the Lord.”
kwa hiyo hamtayaona tena maono ya uongo au kuendelea kufanya utabiri, kwa kuwa nitawaokoa watu wangu kutoka kwenye mkono wako. Nanyi mtajua kwamba mimi ni Yahwe.'”

< Ezekiel 13 >