< Exodus 7 >

1 The Lord told Moses, “Look, I will make you seem like God to Pharaoh, and your brother Aaron will be your prophet.
Kisha Bwana akamwambia Mose, “Tazama, nimekufanya kuwa kama Mungu kwa Farao, naye Aroni, huyo ndugu yako, atakuwa nabii wako.
2 You are to repeat everything that I tell you to say, and your brother Aaron must repeat it to Pharaoh so that he will let the Israelites leave his country.
Utasema kila kitu nitakachokuagiza, naye Aroni ndugu yako atamwambia Farao awaachie Waisraeli watoke katika nchi yake.
3 But I will give Pharaoh a stubborn attitude, and though I will perform many signs and wonders in Egypt, he won't listen to you.
Lakini nitaufanya moyo wa Farao kuwa mgumu. Ingawa nitazidisha ishara na maajabu katika Misri,
4 Then I will attack Egypt, imposing heavy punishments on them, and I will lead out by their tribes my people the Israelites.
hatawasikiliza. Kisha nitaupeleka mkono wangu juu ya Misri, na kwa matendo makuu ya hukumu nitavitoa vikundi vyangu, watu wangu Waisraeli.
5 In this way the Egyptians will know that I am the Lord—when I take action against Egypt and lead the Israelites out of the country.”
Nao Wamisri watajua kuwa Mimi ndimi Bwana nitakapounyoosha mkono wangu dhidi ya Misri na kuwatoa Waisraeli watoke humo.”
6 Moses and Aaron did exactly as the Lord had ordered.
Mose na Aroni wakafanya sawasawa kama vile Bwana alivyowaagiza.
7 Moses was eighty and Aaron was eighty-three when they went and spoke to Pharaoh.
Mose alikuwa na umri wa miaka themanini na Aroni alikuwa na umri wa miaka themanini na mitatu walipozungumza na Farao.
8 The Lord told Moses and Aaron,
Bwana akamwambia Mose na Aroni,
9 “When Pharaoh asks you, ‘Why don't you perform a miracle, then?’ tell Aaron, ‘Take your walking stick and throw it down in front of Pharaoh,’ and it will turn into a snake.”
“Farao atakapowaambia, ‘Fanyeni muujiza,’ basi mwambie Aroni, ‘Chukua fimbo yako na uitupe chini mbele ya Farao,’ nayo fimbo itakuwa nyoka.”
10 Moses and Aaron went to Pharaoh and did what the Lord had ordered. Aaron threw down his staff in front of Pharaoh and his officials, and it turned into a snake.
Ndipo Mose na Aroni wakaenda kwa Farao wakafanya sawasawa kama vile Bwana alivyoagiza. Aroni akaitupa ile fimbo yake chini mbele ya Farao na maafisa wake, nayo ikawa nyoka.
11 But Pharaoh called in wise men and sorcerers, and these Egyptian magicians did the same thing using their magic arts.
Farao naye akawaita watu wenye maarifa na wachawi na waganga wa Kimisri, nao wakafanya vivyo hivyo kwa siri ya uganga wao.
12 Each of them threw down their walking sticks and they also turned into snakes, but Aaron's walking stick swallowed up all their walking sticks.
Kila mmoja alitupa fimbo yake chini, nayo ikawa nyoka. Lakini fimbo ya Aroni ikazimeza zile fimbo zao.
13 But Pharaoh had a hard, stubborn attitude, and he wouldn't listen to them, as the Lord had predicted.
Hata hivyo moyo wa Farao ukawa mgumu, naye hakuwasikiliza Mose na Aroni, sawasawa kama vile Bwana alivyokuwa amesema.
14 The Lord said to Moses, “Pharaoh has a stubborn attitude—he's refusing to let the people go.
Kisha Bwana akamwambia Mose, “Moyo wa Farao ni mgumu, anakataa kuwaachia watu kuondoka.
15 So tomorrow morning go to Pharaoh as he walks down to the river. Wait to meet him on the bank of the Nile. Take with you the walking stick that turned into a snake.
Nenda kwa Farao asubuhi wakati anapokwenda mtoni. Ngoja ukingoni mwa Naili ili uonane naye, na uchukue mkononi mwako fimbo ile iliyobadilishwa kuwa nyoka.
16 Tell him: The Lord, the God of the Hebrews, has sent me to say to you, ‘Let my people go, so that they can worship me in the desert. But you have not listened up until now.
Kisha umwambie, ‘Bwana, Mungu wa Waebrania, amenituma nikuambie: Waachie watu wangu waende, ili wapate kuniabudu jangwani. Lakini hadi sasa hujasikiliza.
17 This is what the Lord is now telling you: This is how you will know that I am the Lord.’” “Watch! Using the walking stick I'm holding, I'm going to hit the water of the Nile, and it will turn to blood.
Hili ndilo Bwana asemalo: Kwa hili utajua kuwa Mimi ndimi Bwana: Fimbo iliyo mkononi mwangu nitapiga nayo maji ya Naili nayo yatabadilika kuwa damu.
18 The fish in the Nile will die, the river will smell, and the Egyptians won't be able to drink any of its water.”
Samaki waliomo katika Mto Naili watakufa, nao mto utanuka vibaya, Wamisri hawataweza kunywa hayo maji yake.’”
19 The Lord said to Moses, “Tell Aaron, ‘Take your walking stick in your hand and hold it out over the waters of Egypt, over their rivers and canals and ponds and pools, so that they will turn to blood. There will be blood through all of Egypt, even in containers made of wood and stone.’”
Bwana akamwambia Mose, “Mwambie Aroni, ‘Chukua ile fimbo yako unyooshe mkono wako juu ya maji ya Misri, juu ya chemchemi na mifereji, juu ya madimbwi na mabwawa yote,’ navyo vitabadilika kuwa damu. Damu itakuwa kila mahali katika Misri, hata kwenye vyombo vya miti na vya mawe.”
20 Moses and Aaron did exactly as the Lord had ordered. While Pharaoh and all his officials watched, Aaron lifted up his walking stick and hit the water of the Nile. Immediately the whole river turned to blood!
Mose na Aroni wakafanya kama vile Bwana alivyokuwa amewaagiza. Akainua fimbo yake machoni pa Farao na maafisa wake na kuyapiga maji ya Mto Naili, na maji yote yakabadilika kuwa damu.
21 The fish in the Nile died, and the river smelled so awful that the Egyptians could not drink its water. There was blood through all of Egypt!
Samaki katika Mto Naili wakafa, nao mto ukanuka vibaya sana kiasi kwamba Wamisri hawakuweza kunywa maji yake. Damu ilikuwa kila mahali katika nchi ya Misri.
22 But the Egyptian magicians did the same thing using their magic arts. Pharaoh maintained his stubborn attitude and he wouldn't listen to Moses and Aaron, just as the Lord had predicted.
Lakini waganga wa Misri kwa kutumia siri ya uganga wao wakafanya vivyo hivyo, nao moyo wa Farao ukawa mgumu, hakuwasikiliza Mose na Aroni, kama vile Bwana alivyokuwa amesema.
23 Pharaoh went back to his palace and didn't pay any attention to what had happened.
Badala yake, Farao akageuka, akaenda kwenye jumba lake la kifalme, wala hakulitia hili moyoni.
24 All the Egyptians dug alongside the Nile because they couldn't drink its water.
Nao Wamisri wote wakachimba kandokando ya Mto Naili kupata maji ya kunywa, kwa sababu hawakuweza kunywa maji ya mto.
25 Seven days went by after the Lord hit the Nile.
Zilipita siku saba baada ya Bwana kuyapiga maji ya Mto Naili.

< Exodus 7 >