< Exodus 36 >
1 So Bezalel, Oholiab, and all the other craftsmen with the necessary expertise and given the skill and ability by the Lord, are to work out how to accomplish all the work of constructing the sanctuary as commanded by the Lord.”
Hivyo Bezaleli na Oholiabu na kila mtu mwenye ustadi ambaye Yahweh aliye mpa ustadi na uwezo kujua jinsi ya kufanya kazi katika ujenzi wa sehemu takatifu wafanye kazi kadiri ya yote Yahweh aliyo amuru.”
2 Moses summoned Bezalel, Oholiab, and all the skilled people who had been given special abilities by the Lord, everyone willing to come and do the work.
Musa akamuita Bezaleli, Oholiabu, na kila mtu mwenye ujuzi ambaye Yahweh kampa ujuzi, na ambaye moyoni mwake ulichochewa kuja na kufanya kazi.
3 Moses gave them everything the Israelites had contributed to carry out the work of constructing the sanctuary. In the meantime the people went on bringing freewill offerings every morning,
Walipokea kutoka kwa Musa sadaka zote ambazo Waisraeli walizo leta kwa ujenzi ya sehemu takatifu. Watu walikuwa bado wanaleta sadaka za hiari kila asubui kwa Musa.
4 so much so that all the craftsmen who were working on the sanctuary stopped what they were doing
Hivyo watu wote walikuwa na ujuzi walikuwa wakifanya kazi sehemu takatifu walikuja kutoka kwenye kazi walikuwa wakifanya.
5 and went and told Moses, “The people have already brought enough to complete the work the Lord has ordered us to do.”
Wachonga mawe walimwabia Musa, “Watu wanaleta zaidi sana ya yanayo itajika kufanya kazi Yahweh aliyo tuamuru.”
6 Moses gave the order, and an announcement was made throughout the camp: “Men and women, don't bring anything more as an offering for the sanctuary.” So the people were stopped from bringing anything more,
Hivyo Musa akaamuru mtu yeyote asilete tena kwa ujenzi wa sehemu takatifu. Kisha watu wakaacha kuleta hivi vitu.
7 since there was already more than enough to do all the work necessary.
Walikuwa na zaidi ya vitu vya ujenzi.
8 The skilled craftsmen among the workers made the ten curtains for the Tabernacle. They were made of finely-spun linen together with blue, purple, and crimson thread, embroidered with cherubim.
Hivyo wachonga mawe miongoni mwao wakajenga lile hema la kuabudia kwa mapazia kumi yaliyo jengwa kitamba kizuri na buluu, zambarau, na sufu nyekundu kwa aina ya kerubi. Hii ni kazi ya Bezaleli, mjenzi mwenye ujuzi sana.
9 Each curtain was twenty-eight cubits long by four cubits wide, and they were all the same size.
Urefu wa kila pazia ulikuwa mikono ishirini na nane, nao upana wa kila kitambaa ulikuwa mikono minne. Vitambaa vyote hivyo vilikuwa na kipimo kimoja.
10 They joined together five of the curtains as one set, and the other five he joined as a second set.
Bezaleli akaunganisha vitambaa vitano pamoja, na vile vitambaa vingine vitano akaviunganisha pamoja.
11 They used blue material to make loops on the edge of the last curtain of both sets.
Kisha akafanya vitanzi vya uzi wa bluu kwenye upindo wa kitambaa kilicho mahali pa kuungania. Akafanya vivyo hivyo kwenye upindo wa kitambaa cha nje kabisa kilicho mahali pale pengine pa kuungania.
12 They made fifty loops on one curtain and fifty loops on the last curtain of the second set, lining up the loops with each another.
Akafanya vitanzi hamsini kwenye kitambaa kimoja, akafanya vitanzi hamsini kwenye mwisho wa kitambaa kilichokuwa mahali pale pengine pa kuungania, vitanzi hivyo vikiwa vinaelekeana.
13 They also made fifty gold clips and joined the curtains together with the clips, so that the Tabernacle was a single structure.
Mwishowe akafanya kulabu hamsini za dhahabu na kuviunganisha vitambaa hivyo pamoja kwa kulabu hizo, hivi kwamba hiyo ikawa maskani moja.
14 They made eleven curtains of goat hair as a tent to cover the Tabernacle.
Bezaleli akafanya vitambaa vya mahema vya manyoya ya mbuzi kwa ajili ya hema lililo juu ya maskani. Vitambaa kumi na moja ndivyo alivyofanyiza.
15 Each of the eleven curtains was the same size—thirty cubits long by four cubits wide.
Urefu wa kila kitambaa ulikuwa mikono thelathini, nao upana wa kila kitambaa ulikuwa mikono minne. Vitambaa hivyo kumi na moja vilikuwa na kipimo kimoja.
16 They joined five of the curtains together as one set and the other six as another set.
Kisha akaunganisha vitambaa vitano pamoja na vile vitambaa vingine sita pamoja.
17 They made fifty loops on the edge of the last curtain in the first set, and fifty loops along the edge of the last curtain in the second set.
Kisha akafanya vitanzi hamsini kwenye upindo wa kitambaa cha nje kabisa kilicho mahali pa kuungania, naye akafanya vitanzi hamsini kwenye upindo wa kile kitambaa kingine kilichoungana nacho.
18 They made fifty bronze clips to join the tent together as a single cover.
Bezaleli akafanya kulabu hamsini za shaba kwa ajili ya kuliunganisha hilo hema pamoja liwe kipande kimoja.
19 They made a covering for the goat hair tent from tanned ram skins, and placed an extra covering of fine leather over that.
Naye akafanya kifuniko cha hema kutokana na ngozi za kondoo dume zilizotiwa rangi nyekundu na kifuniko kutokana na ngozi za sili, upande wa juu.
20 They made an upright framework of acacia wood for the Tabernacle.
Bezaleli akafanya viunzi vya mbao vya hema ya kukutani kutokana na mbao za mshita.
21 Each frame was ten cubits long by one and a half cubits wide.
Urefu wa kiunzi ulikuwa mikono kumi, nao upana wa kila kiunzi ulikuwa mkono mmoja na nusu.
22 Each frame had two pegs so the frames could be connected to each other. They made all the frames of the Tabernacle like this.
Kila kiunzi kilikuwa na ndimi mbili zilizounganishwa. Hivyo ndivyo alivyofanya viunzi vyote vya maskani.
23 They made twenty frames for the south side of the Tabernacle.
Basi akafanya viunzi vya maskani, viunzi ishirini kwa ajili ya upande kuelekea kusini.
24 They made forty silver stands as supports for the twenty frames using two stands per frame, one under every frame peg.
Bezaleli akafanya vikalio arobaini vya fedha viwe chini ya vile viunzi ishirini, vikalio viwili chini ya kiunzi kimoja pamoja na ndimi zake mbili na vikalio vingine viwili chini ya kiunzi kingine pamoja na ndimi zake mbili.
25 Similarly for the north side of the Tabernacle, they made twenty frames
Na kwa ajili ya ule upande mwingine wa maskani, upande wa kaskazini, akafanya viunzi ishirini
26 and forty silver stands, two stands per frame.
na vikalio vyake arobaini vya fedha. Vikalio viwili chini ya kiunzi kimoja na vikalio viwili chini ya kiunzi kingine
27 They made six frames for the back (west side) of the Tabernacle,
Na kwa ajili ya zile pande za nyuma za maskani kuelekea magharibi akafanya viunzi sita.
28 along with two frames for its two back corners.
Naye akafanya viunzi viwili vya pembeni ya maskani kwenye pande zake mbili za nyuma
29 They joined these corner frames at the bottom and at the top near to the first ring. This is how they made the two corner frames.
Hizi zilikuwa pacha upande wa chini, lakini juu ya kila moja kwenye pete ya kwanza. Hivyo ndivyo alivyoifanya yote miwili, ile miimo ya pembeni.
30 In total there were eight frames and sixteen silver stands, two under each frame.
Basi vikajumlika kuwa viunzi vinane na vikalio vyake kumi na sita vya fedha, vikalio viwili kando ya vikalio viwili chini ya kila kiunzi.
31 They made five crossbars of acacia wood to hold together the frames on the south side of the Tabernacle,
Bezaleli akafanya miti ya mshita, mitano kwa ajili ya viunzi vya upande mmoja wa maskani,
32 five for those on the north, and five for those at the back of the Tabernacle, to the west.
na miti mitano kwa ajili ya viunzi vya upande ule mwingine wa maskani na miti mitano kwa ajili ya viunzi vya maskani kwa ajili ya zile pande mbili za nyuma za magharibi.
33 They made the central crossbar which was placed halfway up the frames and ran from one end to the other.
Kisha akafanya mti wa katikati upitie katikati ya vile viunzi toka mwisho mmoja mpaka ule mwingine.
34 They covered the frames with gold, and made gold rings to hold the crossbars in place. They covered the crossbars with gold too.
Naye akavifunika vile viunzi kwa dhahabu, akafanyiza pete zake za dhahabu ziwe vitegemezo kwa ajili ya ile miti, akaifunika ile miti kwa dhahabu.
35 They made a veil out of blue, purple, and crimson thread, and finely-spun linen, embroidered with cherubim by someone who was skilled.
Bezaleli akafanya pazia, la uzi wa bluu na sufu iliyotiwa rangi ya zambarau na kitambaa cha rangi nyekundu ya kochinili na kitani bora kilichosokotwa, kalitia makerubi kwa kazi ya mjenzi.
36 They made four posts of acacia wood for it and covered them with gold. They made gold hooks for the posts and cast their four silver stands.
Kisha akalifanyia nguzo nne za mshita na kuzifunika kwa dhahabu, vibanio vyake vikiwa vya dhahabu, na kutengeneza vikalio vinne vya fedha kwa ajili yake.
37 They made a screen for the entrance to the tent using blue, purple, and crimson thread, and finely-spun linen, and had it embroidered.
Naye akafanya kisitiri kwa ajili ya mwingilio wa hema kutokana na uzi wa bluu na sufu iliyotiwa rangi ya zambarau na kitambaa chenye rangi nyekundu ya kochinili na kitani bora kilichosokotwa, kazi ya mfumaji.
38 They also made five posts of acacia wood with hooks to hang the screen. They covered the tops of the posts and their bands with gold, and their five stands were made of bronze.
Pia akafanya na nguzo zake tano na vibanio vyake. Naye akavifunika vilele vyake na viungo vyake kwa dhahabu, lakini vile vikalio vyake vitano vilikuwa vya shaba.