< Exodus 18 >
1 Moses' father-in-law Jethro, the priest of Midian, heard about everything God had done for Moses and his people the Israelites, and how the Lord had led them out of Egypt.
Yethro, kuhani wa Midiani, baba mkwe wake Musa, alisikia yote Mungu aliyo fanya kwa Musa na kwa Israeli watu wake. Alisikia Yahweh ametoa Israeli kutoka Misri.
2 When Moses had sent home his wife Zipporah, his father-in-law Jethro had welcomed her,
Yethro, baba mkwe wake Musa, akamchukuwa Zipora, mke wa Musa, baada ya kumpeleka nyumbani,
3 together with her two sons. One son was named Gershom, for Moses had said, “I have been a foreigner in a foreign land.”
na wana wake wawili; jina mmoja lilikuwa Gershomu, kwa kuwa Musa alisema, “Nimekuwa mgeni katika nchi ya kigeni.”
4 The other son was named Eliezer, because Moses had said, “The God of my father was my helper, and saved me from death at Pharaoh's hand.”
Jina la mwingine lilikuwa Eliezeri, kwa kuwa Musa alisema, “Mungu wa babu yangu alikuwa msaada wangu. Aliniokoa na mkono wa Farao.”
5 Moses' father-in-law Jethro, together with Moses' wife and sons, came to see him in the desert at the camp near the mountain of God.
Yethro, baba mkwe wake Musa, alikuja na watoto wake Musa na mke wake Musa nyikani alipo eka kambi katika mlima wa Mungu.
6 Moses was told beforehand, “I, your father-in-law Jethro, am coming to see you together with your wife and her two sons.”
Alimwambia Musa, “Mimi, baba mkwe wako Yethro, nina kuja kwako na mke wako na wanao wawili.”
7 Moses went out to meet his father-in-law and bowed down and kissed him. They asked each other how they were and then went into the tent.
Musa alitoka kwenda kukutana na baba mkwe wake, akamwinamia, na kumbusu. Wakajuliana hali na wakaingia ndani ya hema.
8 Moses told his father-in-law about everything the Lord had done to Pharaoh and the Egyptians on behalf of the Israelites, about all the troubles they had experienced on the way, and about how the Lord had saved them.
Musa akamwambia baba mkwe wake yale yote Yahweh aliyo ya fanya kwa Farao na Wamisri kwa ajili ya Waisraeli, magumu yote yaliyo watoke njianim na jinsi Yahweh alivyo waokoa.
9 Jethro was delighted to hear about all the good things the Lord had done for Israel when he'd saved them from the Egyptians.
Yethro akafurahia yale mema yote Yahweh aliyo watendea Israeli, kwa hilo amewaokoa na mkono wa Wamisri.
10 Jethro announced, “May the Lord be blessed, who saved you from the Egyptians and from Pharaoh.
Yethro akasema, “Yahweh atukuzwe, kwa kuwa amekuokoa na mkono wa Wamisri na mkono wa Faraom na kuwatoa watu kwenye mkono wa Wamisri.
11 This is so convincing to me that the Lord is greater than all other gods, for he saved the people from the Egyptians when they acted so arrogantly towards the Israelites.”
Sasa najua Yahweh ni mkuu kuliko miungu yote, kwasababu Wamisri walipo watenda Waisraeli kwa kiburi, Mungu aliwaokoa watu wake.”
12 Then Jethro presented a burnt offering and sacrifices to God, and Aaron came with all the elders of Israel to eat a meal with him in God's presence.
Yethro, baba mkwe wake Musa, akaleta sadaka ya kuteketeza na dhabihu kwa Mungu. Aruni na wazee wote wa Israeli wakaja kula chakula mbele za Yahweh na baba mkwe wake Musa.
13 The following day Moses sat as a judge for the people, and they presented their cases to him from morning to evening.
Siku iliyofuata Musa aliketi kuwa hukumu watu. Watu walisimama kumzunguka Musa kwanzia asubui hadi jioni.
14 When his father-in-law saw everything that Moses was doing for the people, he asked, “What's all this you're doing for the people? Why are you sitting alone as judge, with everyone presenting their cases to you from morning to evening?”
Baba mkwe wake Musa alipo ona yale yote aliyo yafanya kwa watu, alisema, “Ni nini unachofanya na watu? Kwanini unaketi peke yako na watu wote wamesimama kukuzunguka asubui hadi jioni?”
15 “Because the people come to me to ask God for his decision,” Moses replied.
Musa akamwambia baba mkwe wake, “Watu wanakuja kuniuliza muongozo wa Mungu.
16 “When they argue over something, the case is brought before me to decide between one them, and I explain to them the God's laws and regulations.”
Wanapo kuwa na malumbano, wanakuja kwangu. Ninaamua kati ya mtu mmoja na mwingine, na nina wafundisha maagizo na sheria.”
17 Jethro told him, “What you're doing is not the best.
Baba mkwe wake Musa alimwambia, “Unachofanya sicho kizuri sana.
18 You, and these people who come to you, are all going to wear yourselves out, because the workload is far too heavy. You can't handle it alone.
Hakika utajichosha, wewe na watu waliyopo na wewe. Huu mzigo ni mzito sana kwako. Hauwezi kufanya peke yako.
19 So please listen to me. I'm going to give you some advice, and God will be with you. Yes, you must continue to be the people's representative before God, and take their cases to him.
Nisikilize. Nitakupa ushauri, na Mungu ata kuwa na wewe, kwasababu wewe nimwakilishi wa watu kwa Mungu, na una leta malumbano yao kwake.
20 Go on teaching them the laws and regulations. Show them how to live and the work they are to do.
Lazima uwafundishe maagizo yake na sheria. Lazima uwafundishe njia yakutembea na kazi ya kufanya.
21 But now you should choose men who are competent from among the people, men who respect God and who are trustworthy and not corrupt. Put them in charge of the people as leaders of thousands, hundreds, fifties, and tens.
Mbali zaidi, lazima uchague wanaume wenye uwezo kutoka watu wote, wanaume wanao muheshimu Mungu, wanaume wa kweli wanao chukuia mapato ya ufisadi. Lazima uwaeke juu ya watu, kuwa viongozi wa maelfu, mamia, hamsini, na makumi.
22 These men are to judge the people on a continuing basis. Major issues they can bring to you, but they can decide all the small matters themselves. In this way your burden will be made lighter as they share it with you.
Watawa hukumu watu na kesi za kawaida, lakini kesi ngumu wataleta kwako. Kwa kesi ndogo, wanaweza kuhukumu wenyewe. Kwa hivyo itakuwa rahisi kwako, na watabeba mzigo na wewe.
23 If you follow my advice, and if it's what God tells you to do, then you will be able to survive, and all these people can go home satisfied that their cases have been heard.”
Ukifanya hivi, na kama Mungu akikuamuru kufanya al kadhalika, basi utaweza kuvumilia, na watu wote watarudi nyumbani wameridhika.”
24 Moses listened to what his father-in-law said and followed all his advice.
Hivyo Musa akasikiliza maneno ya baba mkwe wake na akafanya yale yote aliyo yasema.
25 So Moses chose competent men from all of Israel and put them in charge of the people as leaders of thousands, hundreds, fifties, and tens.
Musa alichagua wanaume wenye uwezo kutoka Israeli na kuwa fanya vichwa juu ya watu, viongozi wahusika wa maelfu, mamia, hamsini, na makumi.
26 They acted as judges for the people on a continuing basis. They brought the difficult cases to Moses, but they would judge the small matters themselves.
Waliwa hukumu watu katika hali za kawaida. Kesi ngumu walimletea Musa, lakini wao wenyewe wali hukumu kesi ndogo.
27 Then Moses sent Jethro on his way, and he went back to his own country.
Kisha Musa akamwacha baba mkwe wake kuondoka, na Yethro akarudi kwenye nchi yake.