< Ecclesiastes 7 >

1 A good reputation is better than expensive perfume, and the day you die is better than the day you were born.
Jina zuri ni bora kuliko manukato ya gharama, na siku ya kufa ni bora kuliko siku ya kuzaliwa.
2 It's better to go to a funeral than to a party. In the end, everyone dies, and those who are still alive should think about it.
Ni bora kwenda kwenye nyumba ya maombolezo kuliko nyumba ya karamu, kwa kuwa maombolezo huja kwa watu wote wakati wa mwisho wa uhai, kwa hiyo watu wanaoishi ni lazima waweke hili moyoni.
3 Sorrow is better than laughter, for tragedy helps us by making us think.
Huzuni ni bora kuliko kicheko, kwa kuwa baada ya uso wa huzuni huja furaha ya moyo.
4 Wise people think about the impact of death, while those who are fools only think about having a good time.
Moyo wa mwenye hekima uko katika nyumba ya maombolezo, lakini moyo wa wapumbavu uko katika nyumba ya karamu.
5 It's better to listen to criticism from a wise person than to hear the song of fools.
Ni bora kusikiliza maonyo ya mtu mwenye hekima kuliko kusikiliza wimbo wa wapumbavu.
6 The laughter of fools is like the crackling of thorn twigs burning under a pot—without sense and quickly over.
Kwa kuwa kama mlio wa miiba chini ya chungu, ndivyo kilivyo kicheko cha wapumbavu. Huu pia ni mvuke.
7 Extorting money from others makes wise people into fools, and accepting bribes corrupts the mind.
kweli jeuri humfanya mtu mwenye hekima kuwa mpumbavu, na rusha huharibu moyo.
8 Completing something is better than starting it. Being patient is better than being proud.
Ni heri mwisho wa jambo kuliko mwanzo; na watu wenye uvumilivu ni bora kuliko wenye majivuno rohoni.
9 Don't be quick to get angry, for anger controls the minds of fools.
Usikasirike haraka rohoni mwako, kwa sababu hasira hukaa katika mioyo ya wapumbavu.
10 Don't ask, “Why were the good old days better than now?” Asking such questions shows you are not wise.
Usiseme, “Kwa nini siku za zamani zilikuwa bora kuliko siku hizi?” Kwa kuwa sio kwa sababu ya hekima kwamba unauliza swali hili.
11 Wisdom is good—it's like receiving an inheritance. It benefits everyone in life.
Hekima ni njema kama vitu vya thamani tunavyorithi kutoka kwa wazazi wetu. Inatoa faida kwa wale wanaoliona jua.
12 For wisdom provides security, as does money, but the advantage for those who have wisdom is that they are kept safe and sound!
Kwa kuwa hekima hutoa ulinzi kama vile fedha inavyoweza kutoa ulinzi, lakini faida ya maarifa ni kwamba hekima humpa uhai kwa yeyote aliye nayo.
13 Think about what God does. If he makes something bent, you can't straighten it!
Tafakaria matendo ya Mungu: Ni nani awezaye kuimarisha chochote alichokipindisha?
14 On a good day, be happy. When a bad day comes, stop and think. God made each day, so you don't know what will happen to you next.
Wakati nyakati vinakuwa njema, ishi kwa furaha katika hali hiyo, lakini wakati unapokuwa mbaya, tafakari hili: Mungu ameruhusu hali zote ziwepo, Kwa sababu hii, hakuna mwanadamu yeyote atakaye fahamu chochote kinacho kuja baada yake.
15 Throughout my life I've seen so much that is hard to understand. Good people who die young despite doing what is right, and wicked people who live long evil lives.
Nimeona mambo mengi katika siku zangu za ubatili. Kuna watu wenye haki ambao wanaangamia licha ya kwamba wana haki, na kuna watu waovu wanaoishi maisha marefu licha ya kwamba ni waovu.
16 Don't think you can make yourself right by a lot of religious observance, and don't pretend to be so wise. Do you want to destroy yourself?
Usiwe mwenye haki katika macho yako mwenyewe. Kwa nini kujiharibu mwenyewe?
17 On the other hand, don't decide to live an evil life—don't be a fool! Why die before your time?
Usiwe mwovu sana au mpumbavu. Kwa nini ufe kabla ya wakati wako?
18 You ought to keep in mind these warnings. Those who follow God will be sure to avoid both.
Ni vyema kwamba ushike hekima hii, na kwamba usiache haki iende zake. Kwa kuwa mtu amchae Mungu atatimiza ahadi zake zote.
19 Wisdom gives a wise person greater power than ten town councilors.
Hekima ina nguvu ndani ya mwenye hekima, zaidi ya watawala kumi katika mji.
20 There's not one good person in all the world who always does what is right and never sins.
Hakuna mtu mwenye haki juu ya nchi anayefanya mema na hatendi dhambi.
21 Don't take to heart everything that people say, otherwise you may hear your servant talking badly about you,
Usisikilize kila neno linaongelewa, kwa sababu unaweza kusikia mtumishi wako anakulaani.
22 for you know how many times you yourself have talked badly about others!
Vivyo hivyo unafahamu mwenyewe ndani ya moyo wako umewalaani wengine mara kadhaa.
23 I have examined all this using the principles of wisdom. I told myself, “I will think wisely.” But wisdom eluded me.
Haya yote nimeyathibitisha kwa hekima. Nikasema, “nitakuwa mwenye hekima,” lakini zaidi ambavyo ningekuwa.
24 Everything that exists is beyond our grasp—too deep for our understanding. Who can comprehend it?
Hekima i mbali na kina sana. Ni nani awezaye kuipata?
25 I turned my thoughts to discover, investigate, and to find out more about wisdom and what makes sense. I wanted to know more about how stupid evil really is, and how ridiculous it is to be a fool.
Nikageuza moyo wangu kujifunza kuchunguza na kutafuta hekima na ufafanuzi wa ukweli, na kufahamu kwamba ubaya ni ujinga na kwamba upumbavu ni wazimu.
26 I discovered something more horrible than death: foolishness like a woman who tries to entrap you, who wants to use her mind and hands to catch you and tie you up. Those who follow God will not be caught, but sinners will fall into her trap.
Nikapata kufahamu kwamba uchungu kuliko kifo, ndivo alivyo mwanamke yeyote ambaye moyo wake umejaa mitego, na nyavu, na ambaye mikono yake ni minyororo. Yeyote ampendezaye Mungu ataponyoka kutoka kwake, lakini mwenye dhambi atachukuliwa naye.
27 This is what I discovered after putting two and two together to try and find out what it all meant, says the Teacher.
“Tafakari kile nilichovumbua,” asema Mwalimu. “Nimekuwa nikiongeza uvumbuzi mmoja hadi mwingine ili kwamba nipate ufafanuzi wa ukweli.
28 Although I really searched, I didn't find what I was looking for. People say, “I found one man among a thousand, but not one woman.”
Hii ndiyo bado natafuta, lakini bado sijapata. Sikupata mwanamme mmoja mwenye haki miongoni mwa elfu, lakini sikupata mwanamke miongoni mwa wale wote.
29 But I did find this one thing: God made people to do what's right, but they have followed their own ideas.
Nimegundua hili: kwamba Mungu alimuumba binadamu akiwa mnyoofu, lakini wametoka katika hali ya unyofu wakitafuta magumu mengi.

< Ecclesiastes 7 >