< Ecclesiastes 11 >

1 Send your bread out on the surface of the water, and many days later you will find it again.
Peleka mkate wako juu ya maji, kwa kuwa utaupata tena baada ya siku nyingi.
2 Share what you own with seven or eight people, for you never know what disaster could happen.
Shiriki mkate na watu saba, hata wanane kwa kuwa haujui ni majanga gani yanayo kuja juu ya nchi.
3 When the clouds are full they pour rain down upon the earth. Whether a tree falls to the north or to the south, it stays where it fell.
Kama mawingu yamejaa mvua, yanajivua yenyewe chini ya nchi. Na kama mti ukianguka kuelekea kusini au kuelekea kaskazini, popote mti unapoangukia papo hapo utabakia.
4 The farmer who pays attention to the direction of the wind knows when not to sow, and by watching the clouds knows when not to reap.
Yeyote autazamaye upepo yawezekana asipande, na yeyote atazamaye mawingu yawezekana asivune.
5 Just as you don't know how the breath of life comes to the child in its mother's womb, so you can't understand the work of God, the Creator of everything.
Kama usivyo jua njia ya upepo, wala vile ambavyo mtoto akuavyo tumboni, vivyo hivyo huwezi kuielewa kazi ya Mungu, aliye umba kila kitu.
6 In the morning, sow your seed. In the evening, don't stop. For you have no way of knowing which crop will grow well—one may be profitable, or the other—or maybe both.
Asubuhi panda mbegu yako; hadi jioni, fanya kazi kwa mikono yako kama inavyo hitajika kwa kuwa haujui ni ipi itafanikiwa, jioni au asubuhi, au hii au ile au zote zitakuwa nzuri.
7 How sweet it is to live in the light, to see the sun rise on another day.
Kweli nuru ni tamu, na ni kitu cha kufurahisha kwa ajili ya macho kuona jua.
8 May you live for many years, and may you enjoy them all. But remember there will many days of darkness, and all that is to come is uncertain.
Kama mtu akiishi miaka mingi, na aifurahie yote, lakina na afikiri juu ya siku zijazo za giza, kwa kuwa zitakuwa nyingi. Kila kitu kijacho ni mvuke unaoteketea.
9 Young people, enjoy your youth! Be happy with what's good! While you're young, let your mind guide your life, and do as you think best. But remember that God will judge you for all your thoughts and actions.
Furahia kijana, katika ujana wako, na moyo wako ufurahie siku za ujana wako. fuatilia yale mema ya moyo wako, chochote kilicho mbele ya macho yako. Ingawa, fahamu kwamba MUngu atakuleta hukumuni kwa ajili ya vitu hivi vyote.
10 So don't let your mind worry, and avoid things that hurt your body. Even so, despite youth and enthusiasm, life is still so hard to understand!
Ondoa hasira kutoka moyoni mwako, na usijali maumivu yoyote katika mwili wako, kwa sababu ujana na nguvu zake ni mvuke.

< Ecclesiastes 11 >