< Deuteronomy 26 >

1 Once you've entered the country that the Lord your God is giving you to own, and you take it over and settle there,
Utakapofika katika nchi ambayo Yahwe Mungu wako anakupatia kama urithi, na utakapoimiliki na kuishi ndani yake,
2 take some of the firstfruits of all your crops produced by the land that the Lord your God is giving you and place them in a basket. Then go to the place the Lord your God will choose to live with you,
basi unatakiwa kuchukua baadhi ya mavuno yote ya kwanza ya ardhi uliyoyaleta kutoka katika nchi ambayo Yahwe Mungu wako anakupatia. Unatakiwa kuyaweka ndani ya kikapu na kuelekea katika eneo ambalo Yahwe Mungu wako atapachagua kama mahali patakatifu.
3 and tell the priest in charge at the time, “Today I declare to the Lord your God that I now live in the country that the Lord promised our forefathers to give us.”
Unatakiwa kwenda kwa kuhani ambaye atakuwa akihudumu katika siku hizo na kumwambia, “Siku ya leo ninakiri kwa Yahwe Mungu wako ya kuwa nimekuja katika nchi ambayo Yahwe aliapa kwa mababu zetu kutupatia”.
4 The priest will take the basket from you and place it in front of the altar of the Lord your God.
Kuhani anatakiwa kuchukua kikapu mkononi mwako na kukiweka madhabahuni ya Yahwe Mungu wako.
5 Then this is what you are to publicly declare before the Lord your God, “My father was a Aramean who moved from place to place. There were only a few of them when he and his family went to live in Egypt. But they became a large and powerful nation.
Unapaswa kusema mbele ya Yahwe Mungu wako, “Babu yangu alikuwa Mwaremi mzururaji. Alikwenda chini hadi Misri na kukaa kule, na idadi ya watu wake ilikuwa chache. Kule akawa taifa kubwa, lenye nguvu na idadi kubwa.
6 But the Egyptians treated us very badly, oppressing us and forcing us to do hard labor.
Wamisri walitutendea vibaya na kututesa. Walitulazimisha kufanya kazi za watumwa.
7 We cried out for help to the Lord, the God of our forefathers; and the Lord answered us as he saw how much we were suffering, forced to work so hard in such cruelty.
Tulimlilia Yahwe, Mungu wa baba zetu, naye akasikia sauti yetu na kuona mateso yetu, kazi zetu na mateso yetu.
8 The Lord led us out of Egypt with his great power and incredible strength and terrifying actions, signs and miracles.
Yahwe alituondoa Misri kwa mkono wake mkuu, kwa mkono wake ulionyoshwa, kwa hofu kuu, kwa ishara na miujiza;
9 He brought us here and gave us this country, a land flowing with milk and honey.
na ametuleta katika sehemu hii na kutupatia nchi hii, nchi inayotiririka kwa maziwa na asali.
10 Look, Lord! I have brought you the firstfruits of the land that you have given me.” You shall place the basket before the Lord your God and bow down in worship before him.
Tazama sasa, nimeleta mavuno ya kwanza kutoka katika nchi ambayo wewe, Yahwe, umenipatia.” Unapaswa kuweka chini mbele ya Yahwe Mungu wako na kuabudu mbele zake;
11 Then you, the Levites, and the foreigners who live with you are to celebrate all the good things the Lord your God has given to you and your family.
na unapaswa kufurahia katika mema yote ambayo Yahwe Mungu wako amekufanyia, kwa ajili na nyumba yako – wewe, na Mlawi, na mgeni aliye miongoni mwako.
12 Once you've finished storing up a tenth of all your crops in the third year, (the year of the tithe), you shall give it to the Levites, the foreigners, the orphans, and the widows, so they will have enough to eat in your towns.
Utakapomaliza kutoa zaka yote ya mavuno katika mwaka wa tatu, yaani, mwaka wa kutoa zaka, basi unapaswa kuwapatia Mlawi, kwa mgeni, kwa yatima, na kwa mjane, ili kwamba waweze kula ndani ya malango yenu ya mji na kujazilishwa.
13 Then you are to make this declaration in the presence of the Lord your God: “I have brought the holy tithe and I have given it to the Levite, the foreigners, the orphans, and the widows as you have ordered me to do. I have not broken or forgotten your commandments.
Unatakiwa kusema mbele ya Yahwe Mungu wako, “Nimetoa kutoka nyumbani mwangu vitu ambavyo ni mali ya Yahwe, na kumpatia Mlawi, mgeni, yatima, na mjane, kulingana na amri zote ulizonipatia. Sijavunja amri yako yoyote, wala sijazisahau.
14 I have not eaten any of the holy tithe while in mourning, or taken any of it while I was unclean, or used any of it as an offering for the dead. I have obeyed the Lord my God. I have done everything you ordered me to do.
Sijala kati yao wakati wa maombolezo yangu, wala sijaziweka mahali pengine nilipokuwa mchafu, wala sijazitoa kati yao kwa heshima ya wafu. Nimesikiliza sauti ya Yahwe Mungu wangu; Nimetii kila kitu ulichoniamuru kukifanya.
15 Please look down from your home in heaven, and bless your people the Israelites and the country you have given us as you promised our fathers—a land flowing with milk and honey.”
Tazama chini kutoka mahali patakatifu unapoishi, kutoka mbinguni, na ubariki watu wako Israeli, na nchi uliyotupatia, kama ulivyoapa kwa mababu zetu, nchi inayotiririka kwa maziwa na asali.
16 Today the Lord your God orders you to carry out these rules and regulations. Make sure you follow them with all your mind and with all your being.
Leo Yahwe Mungu wako anawaamuru kuzitii sheria na amri hizi; basi utazishikilia na kuzitenda kwa moyo wako wote na kwa nafsi yako yote.
17 Today you have publicly declared that the Lord is your God and that you will follow his ways, keep rules and commandments and regulations, and obey what he says.
Umetamka leo ya kuwa Yahwe ni Mungu wako, na kwamba utatembea katika njia zake na kushikilia sheria zake, maagizo yake na amri zake, na kwamba utaisikiliza sauti yake.
18 Today the Lord has announced that you are a special people who belong to him as he promised. He has announced that you are to keep all his commandments.
Leo Yahwe ametamka ya kwamba mu watu ambao ni mali yake, kama alivyoahidi kwenu, na kwamba mnapaswa kushikilia amri zake zote.
19 He has announced that he will give you greater praise and reputation and honor than any other nation he has made. He has announced that you will be a holy people to the Lord your God, as he promised.
Na atawaweka juu zaidi ya mataifa mengine aliyoyaumba nanyi mtapokea sifa, umaarufu na heshima. Mtakuwa watu waliowekwa kando kwa Yahwe Mungu wako, kama alivyosema.”

< Deuteronomy 26 >