< Daniel 10 >

1 In the third year of the reign of King Cyrus of Persia, a message was revealed to Daniel (also called Belteshazzar). The message was certain and concerned a great conflict. He understood the message and gained understanding of the vision.
Katika mwaka wa tatu wa Koreshi mfalme wa Uajemi, ujumbe ulifunuliwa kwa Danieli, aliyeitwa pia Belteshaza. Ujumbe huu ulikuwa ni wa kwelil. Ulihusu vita kuu. Danieli aliufahamu ujumbe alipopata ufumbuzi kutoka katika maono.
2 When this happened, I, Daniel, had been in mourning for three full weeks.
Katika siku hizo, mimi Danieli, nilikuwa katika maombolezo kwa wiki tatu.
3 I ate no fine food. No meat or wine passed my lips. I used no perfumed oils until those three weeks were over.
Sikula chakula kizuri, sikula nyama, sikunywa divai, na sikujipaka mafuta mwenyewe mpaka ukamilifu wa wiki tatu nzima.
4 On the twenty-fourth day of the first month I was standing on the bank of the great River Tigris.
Katika siku ya ishirini na nne ya mwezi wa kwanza, nilipokuwa niko karibu na mto mkubwa (ambao ni Tigrisi),
5 I looked around and saw a man dressed in linen, and around his waist was a belt of pure gold.
Nilitazama juu na nikamwona mtu aliyevaa kitani, akiwa na mkanda kiunoni mwake uliotengenezwa kwa dhahabu safi kutoka Ufazi.
6 His body shone like a jewel; his face was as bright as lightning; his eyes were like blazing torches; his arms and legs gleamed like polished bronze; and his voice sounded like the roar of a crowd.
Mwili wake ulikuwa kama kito, na sura yake ilikuwa kama radi. Macho yake yalikuwa kama miali ya tochi, na mikono yake na miguu yake ilikuwa kama shaba iliyosafishwa. Sauti ya maneno yake ilikuwa kama sauti ya umati mkubwa wa watu.
7 I, Daniel, was the only one to see this vision—the others with me did not see the vision, but they suddenly felt very frightened and ran away to hide themselves.
Mimi, Danieli peke yangu niliyaona maono, na watu niliokuwa na pamoja hawakuyaona maono. Lakini, jambo kuu la kuogofya liliwaijia juu yao, na walikimbia na kujificha wao wenyewe.
8 I was left alone to see this wonderful vision. My strength drained away, and my face turned pale as death. I didn't have an ounce of strength left.
Hivyo niliachwa peke yangu na niliyaona maono haya ajabu. Hakuna nguvu iliyobakia ndani yangu; mwonekano wangu wa kung'aa ulibadilika na kuwa mwonekano wa uharibifu, na hazikubakia nguvu ndani yangu.
9 I heard him speaking, and when I heard his voice I lost consciousness and I lay face down on the ground.
Kisha nikasikia maneno yake, na nilipoyasikia, nilianguka kifudifudi na kupata usingizi mzito.
10 Then a hand touched me and lifted me onto my hands and knees.
Mkono ulinigusa, na ilinifanya nitetemeke katika magoti yangu na viganja vya mikono yangu.
11 He said to me, “Daniel, God loves you very much. Pay attention to what I'm telling you. Stand up, because I have been sent to you.” When he told me this I stood up, trembling.
Malaika aliniambia, “Danieli, mtu aliyetunzwa sana, yafahamu maneno ninayokwambia wewe. Simama wima, kwa kuwa nimeshakutuma.” Na alipomaliza kuniambia ujumbe huu, nilisimama nikiwa natetemeka.
12 “Don't be afraid, Daniel,” he said. “From the first day you concentrated on trying to understand this, and to humble yourself before God, your prayer was heard, and I have come to answer you.
Kisha aliniambia, “Usiogope, Danieli. Tangu siku ya kwanza ulipoiweka akili yako kutaka kufahamu na kujinyenyekeza mwenyewe mbele ya Mungu, maneno yako yalisikiwa, na nimekuja kwasababu ya maneno yako.
13 But the prince of the kingdom of Persia opposed me for twenty-one days. Then Michael, one of the chief princes, came to help me, because I was being detained there by the kings of Persia.
Mwana wa mfalme wa ufalme wa Uajemi alinizuia, na niliwekwa huko na mfalme wa Uajemi kwa siku ishirini na moja. Lakini Mikaeli, mmoja kati ya wakuu alikuja kunisaidia.
14 Now I've come to explain to you what will happen to your people in the last days, for the vision is about a time in the future.”
Sasa nimekuja kukusaidia ili ufahamu kile kitakachotokea kwa watu wako katika siku za mwisho. Kwa kuwa maono ni kwa ajili siku ambazo hazijatokea bado.
15 As he told me this I remained there with my face to the ground and couldn't say a word.
Na alipokuwa akali akiniambia maneno haya, niligeuza uso wangu na kuuelekeza chini na sikuwa na uwezo wa kuzungumza.
16 Then the one who looked like a human being touched my lips and I was able to speak. I told the one standing in front of me, “My lord, since I saw the vision I've been in agony and I feel really weak.
Yeye aliyekuwa kama wana wa mtu alinigusa mdomo wangu na nifumbua kinywa changu na nilimwambia huyo aliyekuwa amesimam mbele yangu: “Bwana wangu, niko katika masumbuko makali kwasababu ya maono; sina nguvu ndani yangu iliyosalia.
17 How can I, your servant, speak to you, my lord? I have no strength, and I can hardly breathe.”
Mimi ni mtumishi wako. Je ninawezaje kuongea na Bwana wangu? Kwa kuwa sasa sina nguvu, na hakuna pumzi iliyosalia ndani yangu.”
18 Once again the one who looked like a human being touched me and restored my strength.
Tena yule mwenye mwonekano wa mtu alinigusa na kunitia nguvu.
19 “Don't be afraid; God loves you very much. May you have peace! Be strong! Have courage!” As he spoke to me, I became stronger and I said, “My lord, speak to me, for you have strengthened me.”
Alisema, “Usiogope, mtu ulithaminiwa sana. Amani na iwe kwako! Uwe mwenye nguvu, uwe na nguvu!” Na alipokuwa anaongea na mimi, nilipata nguvu. Nilimwambia, “Bwana wangu na aseme, kwa kuwa umenitia nguvu.”
20 “Do you know why I've come to you?” he asked. “Shortly I will have to go back and fight the prince of Persia, and after that the prince of Greece will come.
Aliniambia, “Je unajua ni kwanini nimekuja kwako? Nitarudi hivi karibuni kupigana na mkuu wa Uajemi. Na nitakapoenda, mkuu wa Ugiriki atakuja.
21 But before that I will tell you what is written down in the Book of Truth. No one helps me fight against these princes except Michael your prince.
Lakini nitakwambia kile kilichoandikwa katika Kitabu cha Ukweli. Hakuna yeyote anayejionesha kuwa na nguvu pamoja nami dhidi yao, isipokuwa Mikaeli mkuu wenu.”

< Daniel 10 >