< Colossians 1 >

1 This letter comes from Paul, an apostle of Christ Jesus according to the will of God, and from our brother Timothy.
Paulo, mtume wa Kristo Yesu, kwa mapenzi ya Mungu, na Timotheo ndugu yetu:
2 To the believers and trusting Christians at Colossae: may you have grace and peace from God our Father.
Kwa ndugu watakatifu na waaminifu katika Kristo, waishio Kolosai: Neema na amani zitokazo kwa Mungu Baba yetu ziwe nanyi.
3 We are always thankful to God the Father of our Lord Jesus Christ for you, and pray for you.
Siku zote tunamshukuru Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, tunapowaombea ninyi,
4 We've heard about your trust in Christ Jesus and your love for all the believers
kwa sababu tumesikia kuhusu imani yenu katika Kristo Yesu, na upendo wenu mlio nao kwa watakatifu wote:
5 because of the hope prepared for you in heaven. You already heard about this in the good news, the message of truth
imani na upendo ule utokao katika tumaini mlilowekewa akiba mbinguni, na ambalo mmesikia habari zake katika neno la kweli, yaani, ile Injili
6 that came to you just as it has gone throughout the whole world, spreading widely and bringing results. It's done the same for you too, ever since you heard it and realized the true nature of God's grace.
iliyowafikia ninyi. Duniani kote Injili hii inazaa matunda na kuenea kama ilivyokuwa kwenu tangu siku ile mlipoisikia na kuielewa neema ya Mungu katika kweli yote.
7 Our dear friend and fellow-worker Epaphras, who is a trustworthy minister of Christ on our behalf, taught you about this.
Mlijifunza habari zake kutoka kwa Epafra, mtumishi mwenzetu mpendwa, yeye aliye mhudumu mwaminifu wa Kristo kwa ajili yenu,
8 He's also made clear to us your love in the Spirit.
ambaye pia ametuambia kuhusu upendo wenu katika Roho.
9 Because of this we continue to pray for you from the time we heard about you, asking God to give you understanding of what he wants you to do and to give you every kind of spiritual wisdom and understanding.
Kwa sababu hii, tangu siku ile tuliposikia habari zenu, hatujakoma kuomba kwa ajili yenu na kumsihi Mungu awajaze ninyi maarifa ya mapenzi yake katika hekima yote ya kiroho na ufahamu.
10 That way you'll live lives that rightly represent the Lord and please him, producing all kinds of good results and gaining greater knowledge of God.
Nasi tunaomba haya ili mpate kuishi maisha yanayostahili mbele za Bwana, na mpate kumpendeza kwa kila namna: mkizaa matunda kwa kila kazi njema, mkikua katika kumjua Mungu,
11 May you be made powerfully strong by his wonderful strength, having great patience and endurance.
mkiwa mmetiwa nguvu kwa uwezo wote kwa kadiri ya nguvu yake yenye utukufu, ili mpate kuwa na wingi wa saburi na uvumilivu. Nanyi kwa furaha
12 May you happily praise the Father, who has made it possible for us to share in the inheritance of God's people who live in the light.
mkimshukuru Baba, ambaye amewastahilisha kushiriki katika urithi wa watakatifu katika ufalme wa nuru.
13 He rescued us from the tyranny of darkness and brought us into the kingdom of the Son he loves,
Kwa maana ametuokoa kutoka ufalme wa giza na kutuingiza katika ufalme wa Mwana wake mpendwa,
14 through whom we have been set free and our sins forgiven.
ambaye katika yeye tunao ukombozi, yaani msamaha wa dhambi.
15 The Son is the visible picture of the invisible God. He was before all creation,
Yeye ni mfano wa Mungu asiyeonekana, mzaliwa wa kwanza wa viumbe vyote.
16 for everything was created through him—in heaven and on earth, visible and invisible, empires, rulers, leaders and authorities—everything was created through him and for him.
Kwake yeye vitu vyote vilivyoko mbinguni na juu ya nchi viliumbwa: vitu vinavyoonekana na visivyoonekana, viwe ni viti vya enzi au falme, au wenye mamlaka au watawala; vitu vyote viliumbwa na yeye na kwa ajili yake.
17 He existed before everything, and he holds everything together.
Yeye alikuwepo kabla ya vitu vyote, na katika yeye vitu vyote vinashikamana pamoja.
18 He is also the head of the body, the church. He is the beginning, the first and highest of those raised from the dead, so that he is supreme in everything.
Yeye ndiye kichwa cha mwili, yaani kanisa, naye ndiye mwanzo na mzaliwa wa kwanza kutoka kwa wafu, ili yeye awe mkuu katika vitu vyote.
19 God was pleased to have his full nature live in him,
Kwa kuwa ilimpendeza Mungu kwamba utimilifu wake wote ukae ndani yake,
20 and through him brought back everything in the universe to himself, since he made peace through the blood of his cross, through him reconciling all those on the earth and in heaven.
na kwa njia yake aweze kuvipatanisha vitu vyote na yeye mwenyewe, viwe ni vitu vilivyo duniani au vilivyo mbinguni, kwa kufanya amani kwa damu yake, iliyomwagika msalabani.
21 You once were alienated from God, enemies in the way you thought and the way you acted,
Hapo kwanza mlikuwa mmetengana na Mungu, na mlikuwa adui zake katika nia zenu kwa sababu ya mienendo yenu mibaya.
22 but now he has reconciled you through his dying human body, bringing you into his presence where you stand holy, pure, and faultless.
Lakini sasa Mungu amewapatanisha ninyi kwa njia ya mwili wa Kristo kupitia mauti, ili awalete mbele zake mkiwa watakatifu, bila dosari wala lawama,
23 But your trust in him must continue rock-solid and immovable. Don't be shaken from the hope of the good news that you heard, the good news that's been shared throughout the world—that's the work that I Paul have been doing.
ikiwa mnaendelea katika imani yenu mkiwa imara na thabiti, pasipo kuliacha tumaini lililoahidiwa katika Injili. Hii ndiyo ile Injili mliyoisikia, ambayo imehubiriwa kwa kila kiumbe chini ya mbingu, na ambayo mimi Paulo nimekuwa mtumwa wake.
24 I'm happy to have trouble for your sake, for by means of what happens to me physically I'm part of Christ's sufferings that he continues to experience for the sake of his body, the church.
Sasa nafurahia kule kuteseka kwangu kwa ajili yenu, na katika mwili wangu ninatimiliza yale yaliyopungua katika mateso ya Kristo kwa ajili ya mwili wake, ambao ni kanisa.
25 I serve the church following the direction God gave me about you, to present fully the word of God to you.
Mimi nimekuwa mtumishi wa kanisa kwa wajibu alionipa Mungu ili kuwaletea ninyi Neno la Mungu kwa ukamilifu:
26 This is the mystery that was hidden down through the ages and for many generations, but it's now been revealed to God's people. (aiōn g165)
Hii ni siri iliyokuwa imefichika tangu zamani na kwa vizazi vingi, lakini sasa imefunuliwa kwa watakatifu. (aiōn g165)
27 God wanted to make known to them the glorious wealth of this mystery to the nations: Christ living in you is the glorious hope!
Kwao, Mungu amechagua kujulisha miongoni mwa watu wa Mataifa utukufu wa utajiri wa siri hii, ambayo ni Kristo ndani yenu, tumaini la utukufu.
28 We're telling everyone about him, instructing and teaching them in the best way we know how so that we can bring everyone before God fully mature in Christ.
Yeye ndiye tunayemtangaza, tukimwonya kila mtu na kumfundisha kila mtu kwa hekima yote ili tuweze kumleta kila mmoja akiwa amekamilika katika Kristo.
29 That's what I'm working for too, making every effort as I rely on his strength which is powerfully at work in me.
Kwa ajili ya jambo hili, ninajitaabisha, nikijitahidi kwa kadiri ya nguvu zake ambazo hutenda kazi ndani yangu kwa uweza mwingi.

< Colossians 1 >