< Acts 14 >

1 In Iconium the same thing happened. Paul and Barnabas went to the Jewish synagogue and spoke so convincingly that many of both the Jewish and Greek-speaking worshipers trusted in Jesus.
Huko Ikonio Paulo na Barnaba waliingia pamoja katika sinagogi la Wayahudi kama ilivyokuwa desturi yao. Huko wakahubiri kwa uwezo mkubwa kiasi kwamba Wayahudi pamoja na watu wa Mataifa wakaamini.
2 But the Jews that refused to believe in Jesus stirred up the feelings of the foreigners, and poisoned them against the believers.
Lakini wale Wayahudi waliokataa kuamini, wakawachochea watu wa Mataifa, wakatia chuki ndani ya mioyo yao dhidi ya wale walioamini.
3 Paul and Barnabas stayed there a long time, speaking to them boldly in the Lord, who confirmed their message of grace through the miraculous signs that they were enabled to perform.
Hivyo Paulo na Barnaba wakakaa huko kwa muda wa kutosha wakihubiri kwa ujasiri juu ya Bwana, ambaye alithibitisha ujumbe wa neema yake kwa kuwawezesha kufanya ishara na miujiza.
4 The inhabitants of the town were divided, with some supporting the Jews and some the apostles.
Lakini watu wa mji ule waligawanyika, wengine wakakubaliana na Wayahudi na wengine na mitume.
5 But then the foreigners and the Jews, together with their leaders, decided to attack and stone Paul and Barnabas.
Watu wa Mataifa na Wayahudi wakajiunga na baadhi ya viongozi, wakafanya mpango wa kuwatendea mitume mabaya na kuwapiga mawe.
6 However, they found out about it and fled to the region of Lycaonia, to the towns of Lystra and Derbe,
Lakini mitume walipopata habari hizi wakakimbilia Listra na Derbe, miji ya Likaonia na sehemu zilizopakana nayo.
7 where they continued to share the good news.
Huko wakaendelea kuhubiri habari njema.
8 In the town of Lystra there was a disabled man who was lame in both feet. He had been crippled from birth and had never been able to walk.
Katika mji wa Listra, alikuwako kiwete, ambaye alikuwa amelemaa tangu kuzaliwa na hakuwa ametembea kamwe.
9 He sat there listening to Paul speaking. When Paul looked directly at him, and realized that the man was trusting in God to heal him,
Alimsikiliza Paulo alipokuwa akihubiri. Paulo alipomtazama akaona ana imani ya kuponywa.
10 Paul said in a loud voice, “Stand up on your feet!” The man jumped to his feet and started walking.
Paulo akapaza sauti, “Simama kwa miguu yako!” Mara yule mtu akasimama upesi akaanza kutembea!
11 When the crowds saw what Paul had done, they shouted out in the language of Lycaonia, “The gods have come down to us looking like men!”
Ule umati wa watu ulipoona yaliyokuwa yamefanywa na Paulo, wakapiga kelele kwa lugha yao ya Kilikaonia wakasema, “Miungu imetushukia katika umbo la binadamu!”
12 They identified Barnabas as the Greek god Zeus, and Paul as the god Hermes because he was one who did most of the talking.
Wakamwita Barnaba Zeu na Paulo wakamwita Herme kwa kuwa ndiye alikuwa msemaji mkuu.
13 The priest of the temple of Zeus that lay just outside the town, brought oxen and wreaths to the town gates. He planned to carry out a sacrifice in front of the crowds.
Kuhani wa Zeu, ambaye hekalu lake lilikuwa nje kidogo tu ya mji, akaleta mafahali na mashada ya maua penye lango la mji kwa sababu yeye na ule umati wa watu walitaka kuwatolea dhabihu.
14 But when the apostles Barnabas and Paul learned what was happening, they tore their clothes, and rushed into the crowds, shouting out,
Lakini mitume Paulo na Barnaba waliposikia haya, wakararua nguo zao, wakawaendea wale watu kwa haraka, wakawapigia kelele, wakisema,
15 “People, what are you doing? We are human beings with the same kind of nature as you. We came to bring you good news, so you could turn from these pointless things to a God who is truly alive. He is the one who made heaven, earth, and sea, and everything in them.
“Enyi watu, kwa nini mnafanya mambo haya? Sisi ni wanadamu tu kama ninyi! Tunawaletea habari njema, tukiwaambia kwamba mgeuke mtoke katika mambo haya yasiyofaa, mmwelekee Mungu aliye hai, aliyeziumba mbingu na nchi na bahari na vitu vyote vilivyomo.
16 In past times he allowed all the nations to follow their own ways.
Zamani aliwaachia mataifa waishi walivyotaka.
17 Even so he still provided evidence of himself by doing good, sending you rain from heaven and crops in their seasons, providing all the food you need, and filling you with happiness.”
Lakini hakuacha kuwaonyesha watu uwepo wake: Ameonyesha wema kwa kuwanyeshea mvua toka mbinguni na kuwapa mazao kwa majira yake, naye amewapa chakula tele na kuijaza mioyo yenu na furaha.”
18 With these words they barely managed to stop the crowds from offering sacrifices to them.
Hata kwa maneno haya yote, ilikuwa vigumu kuuzuia ule umati wa watu kuwatolea dhabihu.
19 But then some Jews from Antioch and Iconium arrived and won over the crowds. They stoned Paul, and dragged him outside the town, thinking he was dead.
Ndipo wakaja baadhi ya Wayahudi kutoka Antiokia na Ikonio wakawashawishi wale watu, wakampiga Paulo kwa mawe, wakamburuta hadi nje ya mji, wakidhani amekufa.
20 But when the believers gathered around him, he got up, and went back into the city. The next day he and Barnabas left for Derbe.
Lakini baada ya wanafunzi kukusanyika akainuka na kurudi mjini. Kesho yake yeye na Barnaba wakaondoka kwenda Derbe.
21 After sharing the good news with the people in that town, and after many had become believers, they went back to Lystra, Iconium, and Antioch.
Wakahubiri habari njema katika mji huo na kupata wanafunzi wengi. Kisha wakarudi Listra, Ikonio na Antiokia,
22 They encouraged the believers to remain firm and to continue to trust in Jesus. “We have to go through many trials to enter God's kingdom,” they said.
wakiwaimarisha wanafunzi na kuwatia moyo waendelee kudumu katika imani. Wakawaonya wakisema, “Imetupasa kuingia katika Ufalme wa Mungu kwa kupitia katika taabu nyingi.”
23 After they had appointed elders for every church, and had prayed and fasted with them, Paul and Barnabas left them in the Lord's care, the one that they trusted in.
Nao baada ya kuwateua wazee katika kila kanisa, kwa kufunga na kuomba wakawakabidhi kwa Bwana waliyemwamini.
24 They passed through Pisidia, and arrived in Pamphylia.
Kisha wakapitia Pisidia wakafika Pamfilia.
25 They spoke God's word in Perga, and then went on to Attalia.
Baada ya kuhubiri neno la Mungu huko Perga, wakateremkia Atalia.
26 From there they sailed back to Antioch where they had started out, having been dedicated there in God's grace to the work they had now accomplished.
Kutoka Atalia wakasafiri baharini wakarudi Antiokia, ambako walikuwa wamesifiwa kwa ajili ya neema ya Mungu kutokana na ile huduma waliyokuwa wameikamilisha.
27 When they arrived, they called the church together. They reported everything God had done through them, and how he had opened a door for the foreigners to trust in him.
Walipowasili Antiokia wakaliita kanisa pamoja na kutoa taarifa ya yale yote Mungu aliyokuwa ametenda kupitia kwao na jinsi alivyokuwa amefungua mlango wa imani kwa ajili ya watu wa Mataifa.
28 They stayed there with the believers for a long time.
Nao wakakaa huko pamoja na wanafunzi kwa muda mrefu.

< Acts 14 >