< 2 Samuel 21 >

1 Once during David's reign there was a famine for three years in a row, and David asked the Lord about it. The Lord replied, “It's because Saul and his family are guilty of murdering the Gibeonites.”
Kulikuwa na njaa kwa miaka mitatu katika siku za utawala wa Daudi, na Daudi akautafuta uso wa Yahwe. “Hivyo Yahwe akasema, “njaa hii ni kwa sababu ya mauaji ya Sauli na familia yake, kwa kuwa aliwauwa Wagibeoni.”
2 David summoned the Gibeonites and spoke with them. The Gibeonites were not Israelites, but what was left of the Amorites. The Israelites had sworn an oath to them, but in his nationalistic passion for the Israelites and Judah, Saul had tried to wipe them out.
Basi Wagibeoni hawakuwa uzao wa Israeli; walikuwa ni masalia ya Waamori. Watu wa Israeli walikuwa wameapa kutowauwa, lakini Sauli alitaka kuwaangamiza wote kwa husuda kwa ajili ya watu wa Israeli na Yuda.
3 “What can I do for you?” David asked the Gibeonites. “How can I compensate you so that you may bless the Lord's people?”
Ndipo Daudi alipowaita pamoja Wagibeoni na kuwaambia, “Niwafanyie nini kwa ajili ya upatanisho? Ili kwamba mweze kuwabariki watu wa Yahwe wanaorithi wema na ahadi zake?”
4 “This isn't a question of us receiving payment in silver or gold from Saul or his family,” the Gibeonites replied. “In addition we don't have the right to have anyone in Israel put to death for us.” “I'll do whatever you ask,” David answered.
Wagibeoni wakamjibu, “Hili siyo jambo la fedha wala dhahabu kati yatu na Sauli au familia yake. Na siyo hitaji letu kumwua mtu yeyote katika Israeli.” Daudi akasema, “Chochote mtakacho omba nitawafanyia.”
5 They replied, “Regarding the man who destroyed us, who planned to prevent us having any place to live in the whole country of Israel,
Wakamjibu mfalme, “Mtu aliyetaka kutuuwa aliyepanga kunyume chetu, ili kutuangamiza na kukosa eneo katika mipaka ya Israeli -
6 have seven of Saul's male descendants be handed over to us, and we will hang them in the presence of the Lord at Gibeon of Saul, the Lord's chosen one.” “I will hand them over to you,” said the king.
haya na tupewe watu saba kutoka katika uzao wake, nasi tutawatundika mbele ya Yahwe katika Gibea ya Sauli, palipochaguliwa na Yahwe.” Mfalme akasema, “Nitawapeni”
7 However, the king spared Mephibosheth, son of Jonathan, son of Saul, because of the oath sworn before the Lord between David and Jonathan, son of Saul.
Lakini mfalme akamwifadhi Mefiboshethi mwana wa Yonathani mwana wa Sauli, kwa ajili ya kiapo cha Yahwe kati ya Daudi na Yonathani mwana wa Sauli.
8 The king took Armoni and Mephibosheth, the two sons of Rizpah the daughter of Aiah, whom she had borne to Saul, and the five sons of Merab, the daughter of Saul, whom she had borne to Adriel, son of Barzillai the Meholathite.
Mfalme akawachukua wana wawili wa Rispa binti Ayia aliomzalia Sauli, hawa wana wawili waliitwa Armoni na Mefiboshethi; na pia Daudi akawachukua wana watano wa Mikali binti Sauli, aliomzalia Adrieli mwana wa Berzilai Mmeholathi.
9 He handed them over to the Gibeonites, and they hanged them on the hill in the presence of the Lord. All seven of them died at the same time, executed at the beginning of the barley harvest.
Akawaweka katika mikono ya Wagibeoni. Nao wakawatundika juu ya mlima mbele za Bwana, na wote saba wakafa pamoja. Waliuawa katika kipindi cha mavuno, katika siku ya kwanza mwanzoni mwa mavuno ya shayiri.
10 Rizpah the daughter of Aiah took some sackcloth and spread it out for herself on a rock. From the beginning of the harvest until the time the rains came and poured down on the bodies, she kept the birds away from them during the day and the wild animals at night.
Kisha Rispa, binti Aiya, akachukua nguo ya gunia na akajitanda mwenyewe juu ya mlima kando ya miili ya waliokufa tangu mwanzo wa mavuno mpaka wakati mvua ilipoanza kunyesha. Hakuruhusu ndege wa angani kutua juu ya miili mchana wala ayawani wa mwituni wakati wa usiku.
11 When David heard what Rizpah the daughter of Aiah, Saul's concubine of Saul had done,
Daudi akaambia alichokifanya Rispa, binti Aiya, suria wa Sauli.
12 he retrieved the bones of Saul and his son Jonathan from the men of Jabesh-gilead, who had taken them from the public square of Beth-shan where the Philistines had hung the bodies after they had killed Saul at Gilboa.
Hivyo Daudi akaenda na kuchukua mifupa ya Sauli na mifupa ya Yonathani mwanawe kutoka kwa watu wa Yabeshi Gileadi, waliokuwa wameiiba kutoka katika eneo la jumuiya la Beth Shani, Wafilisti walipokuwa wamewatundika baada ya Wafilisti kumwua Sauli katika Gilboa.
13 David had the bones of Saul and his son Jonathan brought back, and also had the bones of those who had been hanged gathered up.
Daudi akaiondoa pale mifupa ya Sauli na mifupa ya Yonathani mwanawe, na wakakusanya pia mifupa ya wale watu saba waliotundikwa.
14 They buried the bones of Saul and his son Jonathan at Zela in the land of Benjamin, in the tomb of Saul's father Kish. Once they finished doing everything the king had ordered, God answered their prayers to end the famine in the land.
Wakaizika mifupa ya Sauli na Yonathani mwanawe huko Zela katika nchi ya Benjamini, katika kaburi la Kishi babaye. Wakafanya kila alichoagiza mfalme. Ndipo Mungu akajibu maombi yao kwa ajili ya nchi.
15 There was war once more between the Philistines and Israel. David went down with his men to fight the Philistines, and he got worn out.
Kisha Wafilisti wakaenda tena katika vita na Israeli. Hivyo Daudi na jeshi lake wakashuka na kupigana na Wafilisti. Akiwa vitani Daudi akachoshwa na vita.
16 Ishbi-benob, one of the descendants of Rapha, whose bronze spear weighed three hundred shekels, and who was carrying a new sword, said he was going to kill David.
Ishbibenobu, wa uzao wa majitu, ambaye mkuki wake wa shaba ulikuwa na uzito wa shekeli mia tatu na alikuwa na upanga mpya, alitaka kumwua Daudi.
17 But Abishai, son of Zeruiah, came to his rescue, attacked the Philistine, and killed him. Then David's men swore to him, “Don't ever go out with us to battle again, so that the Israel's light isn't snuffed out!”
Lakini Abishai mwana wa Seruya akamwokoa Daudi, akampiga Mfilisti na kumwua. Ndipo watu wa Daudi wakamwapia, kusema, “Hautakwenda vitani pamoja nasi tena usije ukaizima taa ya Israeli.”
18 Some time after this there was another battle with the Philistines at Gob. But then Sibbecai the Hushathite killed Saph, one of the descendants of Repha.
Ikawa baadaye kuwa na vita tena kati ya Wafilisti huko Gobu, wakati Sibekai Mhushathi alipomwua Safu, aliyekuwa miongoni mwa uzao wa Warefai.
19 In another battle with the Philistines at Gob, Elhanan, son of Jair, from Bethlehem, killed the brother of Goliath the Gittite. The shaft of his spear was as thick as a weaver's rod.
Ikawa tena katika vita na Wafilisti huko Gobu, huyo Elhanani mwana wa Jari Mbethlehemu akamwua Goliathi Mgiti, ambaye fumo la mkuki wake lilikuwa kama mti wa mfumaji.
20 In yet another battle at Gath, there was a gigantic man, who had six fingers on each hand and six toes on each foot, making twenty-four all. He too was descended from the giants.
Ikawa katika vita nyingine huko Gathi kulikuwa na mtu mrefu sana mwenye vidole sita katika kila mkono na vidole sita katika kila mguu, jumla yake ishirini na vinne. Yeye naye alikuwa wa uzao wa Warefai.
21 But when he insulted Israel, Jonathan, son of Shimea, David's brother, killed him.
Alipowatukana Israeli, Yonathani mwana mwana wa Shama, nduguye Daudi, akamwua.
22 These four were the descendants of the giants in Gath, but they were all killed by David and his men.
Hawa walikuwa wa uzao wa Warefai wa Gathi, waliuawa kwa mkono wa Daudi na kwa mkono wa askari wake

< 2 Samuel 21 >