< 2 Kings 2 >
1 Just before the Lord took Elijah up to heaven in a whirlwind, Elijah and Elisha were walking together on their way from Gilgal.
Wakati Bwana alipokuwa karibu kumchukua Eliya mbinguni kwa upepo wa kisulisuli, Eliya na Elisha walikuwa njiani wakitoka Gilgali.
2 Elijah said to Elisha, “Please stay here, for the Lord has sent me to Bethel.” But Elisha replied, “As the Lord lives, and as you yourself live, I will not leave you.” So they went to Bethel.
Eliya akamwambia Elisha, “Kaa hapa. Bwana amenituma Betheli.” Lakini Elisha akasema, “Kwa hakika, kama Bwana aishivyo na wewe uishivyo, sitakuacha.” Kwa hiyo wakaenda Betheli pamoja.
3 The sons of the prophets who lived in Bethel came to Elisha and told him, “You do know that the Lord is going to take your master away from you today, don't you?” “Yes, I know,” he replied. “Don't talk about it.”
Wana wa manabii waliokuwako huko Betheli wakamjia Elisha na kumuuliza, “Je, unajua ya kwamba Bwana atakuondolea bwana wako leo?” Elisha akawajibu, “Ndiyo, najua, lakini msizungumze juu ya jambo hilo.”
4 Then Elijah said to him, “Please stay here, Elisha, for the Lord has sent me to Jericho.” He replied, “As the Lord lives, and as you live, I will not leave you.” So they went to Jericho.
Kisha Eliya akamwambia, “Baki hapa, Elisha. Bwana amenituma Yeriko.” Naye akajibu, “Kwa hakika kama Bwana aishivyo na wewe uishivyo, sitakuacha.” Hivyo wakaenda Yeriko.
5 The sons of the prophets who lived in Jericho came to Elisha and told him, “You do know that the Lord is going to take your master away from you today, don't you?” “Yes, I know,” he replied. “Don't talk about it.”
Wana wa manabii waliokuwako huko Yeriko wakamwendea Elisha na kumuuliza, “Je, unajua ya kwamba Bwana atakuondolea bwana wako leo?” Akawajibu, “Ndiyo, najua, lakini msizungumze juu ya jambo hilo.”
6 Then Elijah said to him, “Please stay here, Elisha, for the Lord has sent me to the Jordan.” He replied, “As the Lord lives, and as you live, I will not leave you.” So they travelled on together.
Kisha Eliya akamwambia, “Kaa hapa. Bwana amenituma kwenda Yordani.” Naye akamjibu, “Kwa hakika kama Bwana aishivyo na wewe uishivyo, sitakuacha.” Hivyo wote wawili wakaendelea pamoja.
7 Then a group of fifty of the sons of the prophets went and stood facing Elijah and Elisha at a distance as the two of them stood by the Jordan.
Wana hamsini wa manabii wakaenda na kusimama kwa mbali, kuelekea mahali ambapo Eliya na Elisha walikuwa wamesimama kando ya Mto Yordani.
8 Elijah took his cloak, rolled it up, and hit the water. It divided to the one side and to the other and both of them crossed over on dry ground.
Eliya akachukua vazi lake, akalisokota na kupiga nalo maji. Maji yakagawanyika upande wa kuume na upande wa kushoto, nao wawili wakavuka pakavu.
9 When they arrived on the other side, Elijah asked Elisha, “What can I do for you before I'm taken from you?” “Please let me have a double amount of your spirit,” Elisha replied.
Walipokwisha kuvuka, Eliya akamwambia Elisha, “Niambie, nikufanyie nini kabla sijaondolewa kutoka kwako?” Elisha akajibu, “Naomba nirithi sehemu maradufu ya roho yako.”
10 “What you have asked for is hard,” Elijah responded. “But if you see me when I am taken from you, you will have it, otherwise not.”
Eliya akasema, “Umeomba jambo gumu. Lakini kama utaniona wakati ninapoondolewa kutoka kwako litakuwa lako. La sivyo, hautalipata.”
11 As they were walking along, talking, a chariot of fire and horses of fire came between them, and Elijah was taken up in the whirlwind to heaven.
Walipokuwa wakitembea pamoja na kuzungumza, ghafula gari la moto na farasi wa moto vilitokea na kuwatenganisha wao wawili, naye Eliya akapanda mbinguni katika upepo wa kisulisuli.
12 Elisha saw what happened and cried out, “My father! My father! Look! The chariots and horsemen of Israel!” Then Elisha couldn't see him anymore. He took his clothes and ripped them to pieces.
Elisha aliona hili, naye akapaza sauti, “Baba yangu! Baba yangu! Magari ya Israeli na wapanda farasi wake!” Naye Elisha hakumwona tena. Kisha akazishika nguo zake mwenyewe na kuzirarua.
13 Then Elisha picked up Elijah's cloak that had fallen from him, and went back and stood on the bank of the Jordan.
Akaliokota lile vazi lililoanguka kutoka kwa Eliya, kisha akarudi na kusimama ukingoni mwa Yordani.
14 He took Elijah's cloak that had fallen from him, hit the water, and cried out, “Where is the Lord, the God of Elijah?” When he hit the water, it divided to the one side and to the other and Elisha crossed over.
Ndipo akalichukua lile vazi ambalo lilikuwa limeanguka kutoka kwa Eliya, naye akayapiga yale maji nalo. Akauliza, “Yuko wapi sasa Bwana, Mungu wa Eliya?” Elisha alipoyapiga maji, yakagawanyika kulia na kushoto, naye akavuka.
15 The sons of the prophets who lived in Jericho saw him from the opposite side and shouted out, “Elijah's spirit now rests upon Elisha!” They went over to meet him, and bowed to the ground before him.
Wale wana wa manabii kutoka Yeriko waliokuwa wakitazama wakasema, “Roho wa Eliya inamkalia Elisha.” Nao wakaenda kumlaki na kusujudu hadi nchi mbele yake.
16 “Look,” they said to Elisha, “we your servants have fifty good men here. Please allow them to go and search for your master. Maybe the Spirit of the Lord has taken him and put him down on a mountain or in a valley somewhere.” “Don't bother sending them,” Elisha replied.
Wakasema, “Tazama, sisi watumishi wako tunao watu hamsini wenye uwezo. Waruhusu waende kumtafuta bwana wako. Labda Roho wa Bwana amemtwaa na kumweka katika mlima fulani au bonde fulani.” Elisha akajibu, “Hapana, msiwatume.”
17 But they went on trying to persuade him until he was too embarrassed to say no. “Go ahead and send them,” he told them. So they sent fifty men, who searched for Elijah for three days but couldn't find him.
Lakini wakasisitiza, mpaka akaona aibu kuwakatalia. Hivyo akasema, “Watumeni.” Nao wakawatuma watu hamsini, wakamtafuta kwa siku tatu, lakini hawakumpata.
18 When they returned to Elisha, who was staying in Jericho, he said to them, “Didn't I tell you not to bother going?”
Walipomrudia Elisha, ambaye alikuwa akingojea huko Yeriko, akawaambia, “Je, sikuwaambia msiende?”
19 The townspeople said to Elisha, “Look, sir, while our town has a good location as you can see, the water is bad and the soil is poor.”
Watu wa mji wakamwambia Elisha, “Tazama, bwana wetu, mahali mji huu ulipojengwa ni pazuri, kama bwana wangu aonavyo, lakini maji yake ni mabaya, na nchi haizai.”
20 “Bring me a brand new bowl and put some salt in it,” he replied. So they brought it to him.
Akasema, “Nileteeni bakuli mpya, mweke chumvi ndani yake.” Kwa hiyo wakamletea.
21 Then Elisha went to the spring, threw the salt into it, and said, “This is what the Lord says: ‘I have purified this water. It won't cause death or miscarriages anymore.’”
Kisha akaenda kwenye chemchemi na kuitupa ile chumvi ndani yake, akisema, “Hili ndilo asemalo Bwana: ‘Nimeyaponya maji haya. Kamwe hayatasababisha mauti tena wala kutozaa.’”
22 The water there is still pure to this very day, just as Elisha said it would be.
Nayo yale maji yakaponywa mpaka leo, sawasawa na neno la Elisha alilokuwa amesema.
23 Elisha went on from there to Bethel. As he was walking along the road, a group of youths came from the town. They made fun of him, calling out, “Go on up, baldy! Go on up, baldy!”
Kutoka huko Elisha akakwea kwenda Betheli. Ikawa alipokuwa akitembea barabarani, baadhi ya vijana wakatoka mjini na kumfanyia mzaha. Wakasema, “Paa, wewe mwenye upaa! Paa, wewe mwenye upaa!”
24 Turning around, he looked at them and called down a curse on them in the Lord's name. Suddenly two female bears came out of the forest and mauled forty-two of them.
Akageuka, akawatazama na kuwalaani kwa Jina la Bwana. Kisha dubu wawili wa kike wakatokea mwituni na kuwararua vijana arobaini na wawili miongoni mwao.
25 Elisha carried on to Mount Carmel, and from there he went back to Samaria.
Naye akaondoka huko, akaenda Mlima Karmeli, na kutoka huko akarudi Samaria.