< 2 Kings 12 >
1 Joash became king in the seventh year of the reign of Jehu, and he reigned in Jerusalem for forty years. His mother's name was Zibiah of Beersheba.
Katika mwaka wa saba wa utawala wa Yehu, Yoashi alianza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka arobaini. Jina la mama yake aliitwa Sibia, kutoka Beer-Sheba.
2 Joash did what was right in the Lord's sight during the years that Jehoiada the priest advised him.
Yoashi akafanya yaliyo mema machoni pa Bwana miaka yote ambayo Yehoyada kuhani alikuwa akimwelekeza.
3 Even so, the high places were not removed—the people went on sacrificing and presenting burnt offerings at these places.
Hata hivyo mahali pa juu pa kuabudia hapakuondolewa. Watu waliendelea kutoa kafara na kufukiza uvumba huko.
4 Joash told the priests, “Collect together all the money that is brought as holy offerings to the Lord's Temple, whether the census money, the money from individual vows, and the money brought as a voluntary donation to the Lord's Temple.
Yoashi akawaambia makuhani, “Kusanyeni fedha zote ambazo zitaletwa kama sadaka takatifu kwenye Hekalu la Bwana, yaani fedha zilizokusanywa kama kodi, fedha zilizopokelewa kutokana na nadhiri za watu binafsi, na fedha zilizoletwa kwa hiari hekaluni.
5 Let each priest receive the money from those who give, and use it to repair whatever damage is discovered in the Temple.”
Kila kuhani na apokee fedha kutoka kwa mmoja wa watunza hazina, nazo zitumike kukarabati uharibifu wowote unaoonekana katika Hekalu.”
6 But by the twenty-third year of the reign of Joash, the priests still had not repaired the damage to the Temple.
Lakini ikawa kufikia mwaka wa ishirini na tatu wa utawala wake Mfalme Yoashi, makuhani walikuwa bado hawajalikarabati Hekalu.
7 So King Joash called together Jehoiada and the other priests and asked, “Why haven't you repaired the damage in the Temple? Don't use any more money you're given for yourselves, instead hand it over to others to repair the Temple.”
Kwa hiyo Mfalme Yoashi akamwita Yehoyada kuhani na makuhani wengine, akawauliza, “Kwa nini hamtengenezi uharibifu uliofanyika hekaluni? Msichukue fedha zaidi kutoka kwa watunza hazina wenu kwa ajili ya matumizi yenu, lakini kuanzia sasa ni lazima fedha yote itumike kwa ajili ya kukarabati Hekalu.”
8 The priests agreed not to receive any more money from the people, and that they wouldn't carry out the repairs to the Temple themselves.
Makuhani wakakubali kuwa hawatakusanya tena fedha kutoka kwa watu na kwamba hawatakarabati Hekalu wenyewe.
9 Jehoiada the priest took a large wooden box, cut a hole in its lid, and placed it on the right side of the altar next to the entrance to the Lord's Temple. There the priests who guarded the doorway put all the money brought into the Lord's Temple into the collection box.
Yehoyada kuhani akachukua kisanduku na akatoboa tundu kwenye kifuniko chake. Akakiweka kando ya madhabahu upande wa kulia unapoingia hekaluni mwa Bwana. Makuhani waliolinda ingilio wakaweka ndani ya kisanduku fedha zote ambazo zililetwa katika Hekalu la Bwana.
10 Whenever they saw there was a lot of money in the box, the king's secretary and the high priest would come, count the money brought into the Lord's Temple, and put it into bags.
Kila mara walipoona kuwa kuna kiasi kikubwa cha fedha ndani ya kisanduku, mwandishi wa mfalme na kuhani mkuu walikuja, wakazihesabu fedha hizo zilizoletwa katika Hekalu la Bwana, na kuziweka katika mifuko.
11 Then they weighed out the money and gave it to the supervisors of the work on the Lord's Temple. They paid the ones doing the work—the carpenters, builders,
Wakiisha kuthibitisha kiasi cha hizo fedha, waliwapa watu walioteuliwa kusimamia kazi katika Hekalu. Kwa fedha hizo, wakawalipa wale watu waliofanya kazi katika Hekalu la Bwana: yaani, maseremala na wajenzi,
12 masons, and stonecutters. They also bought the timber and blocks of cut stone needed for the repair of the Lord's Temple, and paid all the other costs of restoring the Temple.
waashi na wakata mawe. Walinunua mbao na mawe ya kuchongwa kwa ajili ya ukarabati wa Hekalu la Bwana, na kulipia gharama nyingine zote za kulitengeneza.
13 However, the money collected for the Lord's Temple was not used for making silver basins, lamp trimmers, bowls, trumpets, or any items of gold or silver for the Lord's Temple.
Fedha zilizoletwa kwenye Hekalu hazikutumiwa kutengenezea masinia ya fedha, mikasi ya kusawazishia tambi, mabakuli ya kunyunyizia, tarumbeta wala vyombo vingine vyovyote vya dhahabu au fedha kwa ajili ya Hekalu la Bwana;
14 It was used to pay the workers doing the repairs to the Lord's Temple.
zililipwa kwa wafanyakazi, ambao walizitumia kwa kukarabati Hekalu.
15 No accounts were demanded from the men who received the money to pay the workers because they did everything honestly.
Wao hawakudai kupewa hesabu ya fedha kutoka kwa wale waliowapa ili kuwalipa wafanyakazi, kwa sababu walifanya kwa uaminifu wote.
16 The money from the guilt offerings and sin offerings was not collected for the Lord's Temple because it belonged to the priests.
Fedha zilizopatikana kutokana na sadaka za hatia na sadaka za dhambi hazikuletwa katika Hekalu la Bwana; zilikuwa mali ya makuhani.
17 Around this time Hazael, king of Aram, went and attacked Gath, and captured it. Then he marched to attack Jerusalem.
Wakati huu Hazaeli mfalme wa Aramu akapanda kuishambulia Gathi, akaiteka. Kisha akageuka ili kuishambulia Yerusalemu.
18 So King Joash of Judah took all the holy objects dedicated by his forefathers Jehoshaphat, Jehoram, and Ahaziah, the kings of Judah, along with all the items he had dedicated himself, and all the gold found in the treasuries of the Lord's Temple and the royal palace, and he sent everything to Hazael, king of Aram. So Hazael retreated from Jerusalem.
Lakini Yoashi mfalme wa Yuda akavichukua vyombo vyote vitakatifu vilivyowekwa wakfu na baba zake, yaani Yehoshafati, Yehoramu na Ahazia, wafalme wa Yuda, zawadi ambazo yeye mwenyewe alikuwa ameziweka wakfu pamoja na dhahabu yote iliyokutwa katika hazina za Hekalu la Bwana na katika jumba la kifalme, akazipeleka kwa Hazaeli mfalme wa Aramu, ambaye hatimaye aliondoka Yerusalemu.
19 The rest of what happened in Joash's reign and all that he did are recorded in the Book of Chronicles of the Kings of Judah.
Kwa matukio mengine ya utawala wa Yoashi na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
20 His officials plotted against him and murdered him at Beth Millo, on the road that goes down to Silla.
Maafisa wake wakafanya shauri baya dhidi yake, nao wakamuulia Yoashi huko Beth-Milo, kwenye barabara iteremkayo kuelekea Sila.
21 The officials who attacked and killed him were Jozacar, son of Shimeath, and Jehozabad, son of Shomer. They buried him with his forefathers in the City of David. His son Amaziah succeeded him as king.
Maafisa waliomuua walikuwa Yozabadi mwana wa Shimeathi, na Yehozabadi mwana wa Shomeri. Akafa na akazikwa pamoja na baba zake katika Mji wa Daudi. Naye Amazia mwanawe akawa mfalme baada yake.