< 2 Kings 10 >

1 There were seventy sons of the house of Ahab living in Samaria. So Jehu wrote letters and sent them to the officials of Samaria, to the elders, and to the guardians of the sons of Ahab, saying:
Wakati huu katika Samaria walikuwepo wana sabini wa nyumba ya Ahabu. Kwa hiyo Yehu akaandika barua na kuzituma Samaria: kwa maafisa wa Yezreeli, kwa wazee, na kwa walezi wa watoto wa Ahabu. Akasema,
2 “Since your master's sons are with you, and you have at your disposal chariots, horses, a fortified city, and weapons, when you receive this letter,
“Mara tu barua hii itakapokufikia, kwa kuwa wana wa bwana wako wapo pamoja nawe, nawe una magari ya vita na farasi, mji wenye ngome na silaha,
3 choose the best and most appropriate son of your master, place him on his father's throne, and fight for your master's house.”
mchague mwenye uwezo zaidi kati ya wana wa bwana wako, na umweke juu ya kiti cha enzi cha baba yake. Kisha upigane kwa ajili ya nyumba ya bwana wako.”
4 But they were extremely frightened, and said to themselves, “If two kings couldn't defeat him, how could we?”
Lakini wakaogopa sana na kusema, “Ikiwa wafalme wawili hawakuweza kupambana na Yehu, sisi tutawezaje?”
5 So the palace and the city leaders, the elders, and the guardians sent a message to Jehu: “We are your servants, and we will do whatever you tell us. We're not going to make anyone king. Do what you think is best.”
Basi msimamizi wa jumba la mfalme, mtawala wa mji, na wazee na walezi wakatuma ujumbe huu kwa Yehu: “Sisi tu watumishi wako, na tutafanya kila kitu utakachosema. Hatutamteuwa mtu yeyote kuwa mfalme. Wewe fanya uonalo kuwa ni bora.”
6 Then Jehu wrote them a second letter, saying, “If you are on my side, and if you are going to obey what I say, bring the heads of your master's sons to me in Jezreel by this time tomorrow.” The seventy king's sons were being raised by the leading men of the city.
Kisha Yehu akawaandikia barua ya pili, akisema, “Ikiwa ninyi mko upande wangu na mtanitii mimi, twaeni vichwa vya wana wa bwana wenu, na mnijie huku Yezreeli kesho wakati kama huu.” Wakati huo wana sabini wa mfalme walikuwa wakiishi pamoja na viongozi wa mji wa Samaria, waliokuwa wakiwalea.
7 When the letter arrived, they seized the king's sons and killed all seventy of them, placed their heads in baskets, and sent them to Jehu at Jezreel.
Hiyo barua ilipowafikia, watu hawa wakawachukua wale wana sabini wa mfalme na kuwachinja wote. Wakaweka vichwa vyao ndani ya makapu na kumpelekea Yehu huko Yezreeli.
8 A messenger came in and told Jehu, “They have brought the heads of the king's sons.” Jehu gave the order, “Put them in two piles at the entrance to the city gate until the morning.”
Mjumbe alipofika, akamwambia Yehu, “Wameleta vichwa vya wana wa mfalme.” Ndipo Yehu akaagiza, “Viwekeni malundo mawili katika ingilio la lango la mji mpaka asubuhi.”
9 In the morning Jehu went out to speak to the people who had gathered. “You haven't done anything wrong,” he told them. “I was the one who plotted against my master and killed him. But who killed all these?
Asubuhi yake, Yehu akatoka nje. Akasimama mbele ya watu wote na akasema, “Hamna hatia. Ni mimi niliyefanya shauri baya dhidi ya bwana wangu na kumuua, lakini ni nani aliyewaua wote hawa?
10 Rest assured that nothing of what the Lord has prophesied against the house of Ahab will fail, for the Lord has done what he promised through his servant Elijah.”
Fahamuni basi kwamba, hakuna neno ambalo Bwana amesema dhidi ya nyumba ya Ahabu ambalo halitatimia. Bwana amefanya lile aliloahidi kupitia mtumishi wake Eliya.”
11 So Jehu killed everyone in Jezreel who was left of the house of Ahab, as well as all his high officials, close friends, and priests. This left Ahab without a single survivor.
Hivyo Yehu akaua kila mtu huko Yezreeli aliyekuwa amebaki wa nyumba ya Ahabu, ikiwa ni pamoja na wakuu wake, rafiki zake wa karibu, na makuhani wake. Hakuacha yeyote anusurike.
12 Then Jehu left and went Samaria. At Beth-eked of the Shepherds,
Kisha Yehu akaondoka kuelekea Samaria. Alipokuwa njiani karibu na nyumba ya kukatia manyoya ya kondoo, yaani, Beth-Ekedi ya wachunga kondoo,
13 he met some relatives of Ahaziah, king of Judah. “Who are you?” he asked them. “We're relatives of Ahaziah,” they replied. “We've come to visit the sons of the king and of the queen mother.”
Yehu akakutana na watu wa jamaa ya Ahazia mfalme wa Yuda, akauliza, “Ninyi ni nani?” Wao wakasema, “Sisi ni jamaa ya Ahazia, nasi tumeshuka kuwasalimu jamaa ya mfalme na ya mama malkia.”
14 “Take them alive!” Jehu ordered. So they took them alive, then killed them at the well of Beth-eked. There were forty-two men. He didn't allow any of them to live.
Yehu akaagiza, “Wakamateni wakiwa hai!” Kwa hiyo wakawachukua wakiwa hai, watu arobaini na wawili, na kuwachinja kando ya kisima cha Beth-Ekedi. Hakuacha yeyote anusurike.
15 He left there and came across Jehonadab, son of Rekab, who was coming to meet him. Jehu greeted him and asked him, “Are you as committed to me, as I am to you?” “Yes I am,” Jehonadab replied. “In that case, give me your hand,” said Jehu. So he stretched out his hand, and Jehu helped him up into the chariot.
Baada ya kuondoka hapo, alimkuta Yehonadabu mwana wa Rekabu, aliyekuwa akienda kumlaki. Yehu akamsalimu na kusema, “Je, moyo wako ni mnyofu kwangu kama moyo wangu ulivyo kwako?” Yehonadabu akajibu, “Ndiyo.” Yehu akasema, “Kama ndivyo, nipe mkono wako.” Yeye akampa mkono, naye Yehu akampandisha kwenye gari lake la vita.
16 “Come with me and see how dedicated I am to the Lord!” Jehu said, and had him ride in his chariot.
Yehu akasema, “Twende pamoja ukaone wivu wangu kwa ajili ya Bwana.” Hivyo wakasafiri pamoja kwenye gari lake.
17 When Jehu arrived in Samaria, he went around killing everyone who was left of Ahab's family until he had killed all of them, just as the Lord had said through Elijah.
Yehu alipofika Samaria, akawaua wale wote waliokuwa wamesalia wa jamaa ya Ahabu, akawaangamiza, sawasawa na neno la Bwana alilosema kupitia Eliya.
18 Jehu had all the people gather together and told them, “Ahab worshiped Baal a little, but Jehu will worship him a lot.
Kisha Yehu akawaleta watu wote pamoja na kuwaambia, “Ahabu alimtumikia Baali kidogo. Lakini Yehu atamtumikia zaidi.
19 So summon all the prophets of Baal, all his servants and all his priests. Make sure no one is missing, because I'm organizing a great sacrifice for Baal. Anyone who doesn't attend will be executed.” But Jehu's plan was a trick to destroy the followers of Baal.
Sasa waiteni manabii wote wa Baali, watumishi wake wote na makuhani wake wote. Hakikisheni kwamba hakuna hata mmoja atakayekosekana, kwa sababu ninakwenda kutoa kafara kubwa sana kwa Baali. Yeyote atakayeshindwa kuja hataendelea kuishi.” Lakini Yehu alifanya hivyo kwa hila ili apate kuwaangamiza watumishi wote wa Baali.
20 Jehu gave the order, “Call a religious assembly to honor Baal!” So they did so.
Yehu akasema, “Itisheni kusanyiko kwa heshima ya Baali.” Basi wakatangaza jambo hilo.
21 Jehu sent the announcement through the whole of Israel. All the followers of Baal came—not a single man was missing. They went into the temple of Baal, filling it from end to end.
Kisha Yehu akapeleka ujumbe katika Israeli yote, nao watumishi wote wa Baali wakaja, hakuna hata mmoja ambaye hakufika. Wakasongana ndani ya hekalu la Baali hadi likajaa tangu mlango hadi mwisho wake.
22 Jehu said to the keeper of the wardrobe, “Distribute clothes for all the servants of Baal.” So he brought out clothes for them.
Naye Yehu akamwambia yule aliyekuwa mtunza chumba cha mavazi, “Leta majoho kwa ajili ya watumishi wote wa Baali.” Basi akawaletea majoho.
23 Then Jehu and Jehonadab, son of Rekab, went into the temple of Baal. Jehu told the followers of Baal, “Look around and make sure that no one who follows the Lord is here with you, only the worshipers of Baal.”
Kisha Yehu na Yehonadabu mwana wa Rekabu wakaingia ndani ya hekalu la Baali. Yehu akawaambia watumishi wa Baali, “Tazameni kila mahali mhakikishe kwamba hakuna hata mtumishi mmoja wa Bwana aliye hapa pamoja nanyi, ila ni watumishi wa Baali tu.”
24 They were inside presenting sacrifices and burnt offerings. Now Jehu had positioned eighty men outside and cautioned them, “I'm handing these men over to you. If you let any of them escape, you will pay for his life with yours.”
Kwa hiyo wakaingia ndani ili kutoa kafara na sadaka ya kuteketezwa. Wakati huu, Yehu alikuwa amewaweka watu wake themanini akiwa amewapa onyo kwamba, “Ikiwa mmoja wenu atamwachia mtu yeyote ninayemweka mikononi mwake atoroke, itakuwa uhai wako kwa uhai wake.”
25 As soon as Jehu had finished presenting the burnt offering, he ordered his guards and officers, “Go in and kill them all! Don't let even one escape!” So they killed them with their swords. The guards and officers threw their bodies outside, and then they went into the inner sanctuary of the temple of Baal.
Mara baada ya Yehu kutoa sadaka ya kuteketezwa, akawaamuru walinzi na maafisa: “Ingieni ndani, waueni; asitoroke hata mmoja.” Basi wakawakatakata kwa upanga. Walinzi na maafisa wakazitupa zile maiti nje, kisha wakaingia mahali pa ndani pa kuabudia miungu katika hekalu la Baali.
26 They dragged out the idol pillars and burned them.
Wakaileta ile nguzo ya kuabudiwa nje ya hekalu la Baali, na wakaichoma moto.
27 They smashed the sacred pillar of Baal, and tore down the temple of Baal and turned it into a toilet, which it still is to this day.
Wakabomoa ile nguzo ya kuabudiwa ya Baali pamoja na hekalu la Baali, nao watu wakapafanya kuwa choo hadi leo.
28 This was how Jehu destroyed Baal worship in Israel,
Kwa hiyo Yehu akaangamiza kuabudiwa kwa Baali katika Israeli.
29 but he did not end the sins that Jeroboam, son of Nebat, had made Israel commit—the worship of the golden calves at Bethel and Dan.
Hata hivyo, Yehu hakuziacha dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati, ambazo alikuwa amesababisha Israeli kuzitenda, yaani kuabudu ndama za dhahabu huko Betheli ya Dani.
30 The Lord said to Jehu, “Since you have done well, and have carried out what is right in my sight, and have accomplished all that I planned for the house of Ahab, your descendants will sit on the throne of Israel to the fourth generation.”
Bwana akamwambia Yehu, “Kwa kuwa umefanya vyema kwa kutimiza yaliyo sawa machoni pangu, na umetenda kwa nyumba ya Ahabu yale yote niliyokuwa nimekusudia kutenda, wazao wako wataketi juu ya kiti cha enzi cha Israeli hadi kizazi cha nne.”
31 But Jehu was not completely committed to following the law of the Lord, the God of Israel. He did not end the sins that Jeroboam had made Israel commit.
Lakini Yehu hakuwa mwangalifu kushika sheria za Bwana, Mungu wa Israeli, kwa moyo wake wote. Hakuziacha dhambi za Yeroboamu, ambazo alikuwa amesababisha Israeli kuzitenda.
32 At that time the Lord began to reduce the extent of Israel. Hazael defeated the Israelites throughout their territory
Katika siku hizo, Bwana akaanza kupunguza ukubwa wa Israeli. Hazaeli akawashinda Waisraeli sehemu zote za nchi yao
33 east of the Jordan, all the land of Gilead (the region occupied by Gad, Reuben, and Manasseh), and from Aroer through the Arnon Valley up to Gilead and Bashan.
mashariki ya Yordani, katika nchi yote ya Gileadi (eneo la Gadi, Reubeni na Manase), kutoka Aroeri karibu na Bonde la Arnoni kupitia Gileadi hadi Bashani.
34 The rest of what happened in Jehu's reign, all that he did and what he accomplished, are recorded in the Book of Chronicles of the Kings of Israel.
Kwa matukio mengine ya utawala wa Yehu, yote aliyofanya na mafanikio yake yote, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
35 Jehu died and was buried in Samaria. His son Jehoahaz succeeded him as king.
Yehu akalala pamoja na baba zake, naye akazikwa huko Samaria. Naye Yehoahazi mwanawe akawa mfalme baada yake.
36 Jehu reigned over Israel in Samaria for twenty-eight years.
Muda Yehu aliotawala juu ya Israeli huko Samaria ilikuwa miaka ishirini na minane.

< 2 Kings 10 >