< 2 Chronicles 32 >

1 After Hezekiah's faithful work, Sennacherib, king of Assyria, invaded Judah and attacked its fortified towns, planning to conquer them for himself.
Baada ya mambo haya na matendo haya ya uaminifu, Senakeribu, mfalme wa Ashuru, akaja na kuingia Yuda. Alipiga kambi kwa ajili ya kuivamia miji yenye ngome, ambayo alikusudia kuiteka kwa ajili yake.
2 When Hezekiah saw that Sennacherib had come to attack Jerusalem,
Sedekia alipoona kwamba Senakeribu amekuja na kwamba amedhamiria kupigana zidi ya Yerusalemu,
3 he talked with his army commanders about blocking up the water sources that lay outside the city. This is what they did.
aliwashirikisha viongozi wake na watu wake wenye nguvu kuyazuia maji ya chemichemi yaliyokuwa nje ya mji; waalimsaidia kufanya hivyo.
4 They directed a large group of workers to block all the springs as well as the stream flowing nearby. “Why should the kings of Assyria come here and find plenty of water?” they asked.
Kwa hiyo watu wengi wakakusanyika na kuyazuia maji ya chemichemi zote na mikondo yote amabayo ilikuwa inatiririka katikati ya nchi. wakasema, “Kwa nini mfalme wa Ashuru aje na kupata maji mengi?”
5 Hezekiah set to work and rebuilt all the parts of the wall that had fallen down and constructed towers on it. He also built another wall outside the first wall. He reinforced the Millo in the city of David. He also made a large quantity of weapons and shields.
Hezekia akijipa ujasiri na kuujeenga ukuta wote uliokuwa umeangushwa chini. Akaijenga minara mirefu, na pia ukuta mwingine nje. Pia akaiimarisha Milo katika mji wa Dudi, na akafanya kiasi kikubwa cha silaha na ngao. (Maanshi ya kale yanasema hivi: “Badala ya, “akajenga minara amirefu”, baadhi ya matoleo ya zamani na kisasa yanasema, “akajenga minara mirefu juu yake”, Hii ni juu ya ukuta).
6 Hezekiah put army commanders in charge of the people. Then he summoned the people to gather in the square at the city gate. He spoke to them confidently, telling them,
Akaweka maamri jeshi juu wa watu. Akawakusanya pamoja kwake katika sehemu pana kwenye lango la mji na akasema kwao kwa ujasiri. Akasema,
7 “Be strong and be brave! Don't be afraid or discouraged because of the king of Assyria with his large army, for there are more with us than with him.
“Muwe imara na wenye ujasiri mzuri. Msiogope wala kukata tamaa kwa sababu ya mfalme wa Ashuru na jeshi lote ambalo liko naye, kwa maana kuna mtu yuko pamoja nasi ambaye ni mkuu kuliko
8 He has human help, but we have the Lord God on our side to help us and fight our battles.” The people were encouraged by this speech of Hezekiah, king of Judah.
walio naye mfalme wa Ashuru. walionaye ni jeshi la mwili tu, lakini aliye nasi ni Yahwe, Mungu wetu, kwa ajili ya kutusaidia, na kupiagana vita vyetu.” Kisha watu wakajifariji wenyewe kwa maneno ya Hezekia, mfalme wa Yuda.
9 Some time later, when Sennacherib was attacking the town of Lachish with his armies, he sent his officers to Jerusalem with this message for Hezekiah, king of Judah, and for everyone from Judah living there.
Baada ya hayo, Senakeribu, mfalme wa Ashuru, aliwatuma watumishi wake kwenda Yetusalemu (sasa alikuwa mbe ya Lakishi, na jeshi lake lote lilikuwa pamoja naye), kwa Hezekia, mfaalme wa Yuda, na watu wote wa Yuda walikuwa Yerusalemu. Akasema,
10 “This is what Sennacherib, king of Assyria, says. What are you going to trust in to help you survive when I come to attack Jerusalem?
“Hivi ndivyo Senakeribu, mfalme wa Ashuru, anasema: Ni kitu gani mnategemea kwa ajili ya kuhimili uvamizi katika Yerusalemu?
11 Can't you see that in reality Hezekiah is telling you to die from starvation and thirst when he tells you, ‘The Lord our God will save us from the king of Assyria’?
Je, Hezekia hawapotoshi ninyi, ili kwamba awatoe kufa kwa njaa na kiu, anapowaambia, “Yahwe Mungu wetu atatuokoa na mkono wa mfalme wa Ashuru?
12 Wasn't it Hezekiah who destroyed the high places and altars of this god and told Judah and Jerusalem, ‘You must worship at this one altar, and offer sacrifices on it alone’?
Je, siyo Hezekia yule yule ambaye amezipeleka juu sehemu zake na madhabahu zake na kuwaamuru Yuda na Yerusalemu, juu ya madhabahu moja lazima muabudu, na juu yake lazima mchome sadaka zenu?
13 Don't you know what I and my fathers have done to all the nations of the earth? None of their gods could save them or their lands from me!
Je, hamjui mimi na babu zangu tulifanya nini kwa makundi ya wote wa inchi zingine? Je, miungu ya watu wa hizo nchi iliweza kwa njia yoyote kuziokoa nchi zao zidi ya nguvu zangu?
14 Which one of all these gods of these nations that my fathers destroyed has been able to save them from me? So why would you think your god can save you from me?
Miongoni mwa miungu yote ya mataifa hayo amabayo babu zangu waliwatekeza, je, kulikuwa na muungu yeyote aliyeweza kuwaokoa watu wake kutoka kwenye mkono wangu? Itakuwaje Mungu wenu aweze kuwakoa ninyi zidi ya nguvu zangu?
15 So don't let Hezekiah fool you, and don't let him mislead you like this. Don't trust him, for no god of any nation or kingdom has been able to save their people from me or from my fathers. So it's even less possible for your god to save you from me!”
Sasa msimuruhusu Hezekia awadanganye au kuwashawishi katika njia hii. Msimwamini, kwa maana hakuna muungu wa taifa lolote au ufalme amewahi kuwaokoa watu wake nje ya mkono wangu, au nje ya mkono wa babu zangu. Sembuse na Mungu wenu kwa namna gani atawaokoa na mkono wangu?
16 Sennacherib's officers continued criticizing the Lord God and his servant Hezekiah.
Watumishi wa Senakeribu hata walinena mabaya zaidi juu ya Yahwe Mungu na juu ya mtumishi wake Hezekia.
17 Sennacherib also wrote letters insulting the Lord, the God of Israel, taunting him by saying, “In the same way the gods of the nations did not save their people from me, so the god of Hezekiah will not save his people from me either.”
Senakeribu pia akandika barua ili kumdhihaki Yahwe, Mungu wa Israeli, na kunena kinyume naye. Alisema, “Kama ambavyo miungu ya mataifa haikuwaokoa watu wake kutoka kwenye mkono wangu, hivyo hivyo na Mungu wa Hezekia hatawaokoa watu wake kutoka kwenye mkono wangu.”
18 The Assyrians also shouted this out in Hebrew to the people of Jerusalem standing on the wall to frighten and to terrify them so that the city would be surrendered.
Wakawalilia kwa lugha ya Wayahudi watu wa Yerusalemu waliokuwa juu ya ukuta, ili kuwaogopesha na kuwasumbua, ili kwamba waweze kuuteka mji.
19 They talked about the God of Jerusalem like they did about the gods of the other nations, gods made by human beings.
Wakamnenea Mungu wa Yerusalemu kama walivyowanenea miungu wa Dunia, ambao ni kazi ya mikono ya wanadamu tu.
20 King Hezekiah and the prophet Isaiah, son of Amoz, appealed about this in prayer to the God of heaven.
Hezekia, mfalme, na Isaya mwana wa Amozi, nabii, wakaomba kwa sababu ya jambo hili na wakalia hadi mbinguni.
21 The Lord sent an angel who wiped out every warrior, leader, and commander in the camp of the Assyrian king. So he returned home in disgrace. When he went into the temple of his god, some of his own sons killed him with their swords.
Yahwe akatuma malaika, ambaye aliwaua wanaume wa kupigana vita, majemedari, na maakida wa mfalme katika kambi. Kwa hiyo Senakeribu akarudi katika nchi yake akiwa na uso wa aibu. Alipokuwa ameenda katika nyumba ya muungu wake, baadhi ya watoto wake wakamuua huko kwa upanga.
22 The Lord saved Hezekiah and the people of Jerusalem from King Sennacherib of Assyria and all other enemies, giving them peace in every direction.
Katika namna hii, Yahwe akamwokoa Hezekia na wakazi wa Yerusalemu kutoka kwenye mkono wa Senakeribu, mfalme wa Ashuru, na kutoka kwenye mikono ya wengine, na akawapa pumzika juu ya kila upande. (Maandishi ya kale yanasema hivi: badala ya “akawapa pumziko juu ya kila pande”, baadhi ya matoleo ya zamani na ya kisasa yanasema, “akawaongoza juu ya kila pande”).
23 From then on he was very well respected by all the nations, and many brought offerings to Jerusalem for the Lord and valuable gifts for Hezekiah, king of Judah.
Wengi walikuwa wakileta sadaka kwa Yahwe katika Yarusalemu, na zawadi za thamani kwa Hezekia mfalme wa Yuda, kwa hiyo aliinuliwa mbele za macho ya mataifa yote toka wakati huo na kuendelea.
24 Around that time Hezekiah fell sick and was about to die. So he prayed to the Lord, who replied by healing him and giving him a miraculous sign.
Katika siku hizo Hezekia akaugua hadi hatua ya kufa. Akaomba kwa Yahwe, ambaye alisema kwake na kumpa ishara kwamba angeponywa.
25 But because he had become proud, Hezekiah did not acknowledge the gift he'd been given. So the Lord's anger fell on him, and on Judah and Jerusalem.
Lakini Hezekia hakumlipa Yahwe kwa ajili ya msaada uliotolewa kwake, kwa maana moyo wake uliinuliwa juu.
26 Then Hezekiah apologized for his arrogance, as did the people of Jerusalem, and the Lord's anger no longer fell on them during Hezekiah's lifetime.
Kwa hiyo hasira ikaja juu yake, na juu ya Yuda na Yerusalemu. Hata hivyo, baadaye Hezekia alijinyenyekesha mwenyewe kwa jali ya kiburi cha moyo wake, wote Yeye na wakaaji wa Yerusalemu, hivyo hasira ya Yahwe haikuja juu yao wakati wa siku za Hezekia.
27 Hezekiah was very rich and highly honored, and he built treasury storerooms to hold silver, gold, precious stones, spices, shields, and all kinds of valuable things.
Hezekia alikuwa na utajiri mwingi sana na heshima kubwa. Alijipatia mwenyewe vyumba vya kuhifadhia kwa ajili ya fedha, dhahabu, vito vya thamani, na kwa ajili ya manukato, na kwa ajili ya ngao na na vyombo vyote vya thamani pia.
28 He constructed buildings to store supplies of grain, new wine, and olive oil, and stalls for all kinds of animals, including cattle and sheep.
Pia alikuwa na nyumba za maghala kwa ajili ya mavuno ya nafaka, divai mpya, na mafuta, na malisho kwa ajili ya aina zote za wanyama.
29 He built many towns, and he owned large herds of cattle and flocks of sheep, for God had made him very wealthy.
Pia alikuwa na makundi katika mazizi. Zaidi ya hayo, alijipatia mwenyewe miji na makundi ya na ng'ombe kwa wingi, kwa maana Mungu alaikuwa amempa afya tele. (Maandishi ya kale yanasema hivi: Badala ya “miji” baadji ya matoleo ya kisasa yanasema “punda”, na baadhi mengine ya kisasa yanaacaha neno nzima)
30 Hezekiah blocked off the outlet of the upper Gihon spring and made the water flow down to the west side of the City of David. Hezekiah was successful in everything he did.
Alikuwa ni Hezekia huyu huyu ambaye alisimamisha chemi chemi ya juu ya maji ya Gihoni, na aliye ileta moja kwa moja chini upande wa magharibi mwa mji wa Daudi. Hezekia alifanikiwa katika miradi yake yote.
31 But when ambassadors of the rulers of Babylon came to him to ask about the miraculous sign that had happened in the country, God left him to himself test him, so he could know Hezekiah's true thinking.
Hata hivyo, katika jambo la mabolozi wa wakuu wa Babeli, waliotumwa kwake kuwauliza waliofahamu, kuhusu ishara za miujiza iliyokuwa imefanywa katika nchi, Mungu alimwachia mwenyewe, ili kumjaribu, na kujua yote yaliyokuwa katika moyo wake.
32 The rest of what Hezekiah did, including his acts of loyalty, are recorded in the vision of the prophet Isaiah, son of Amoz, in the Book of the Kings of Judah and Israel.
Kwa mambo mengine kuhusu Hezekia, pamoja na matendo yake ya uaminifu wa agano, unaweza kuona kwamba yameandikwa katika Maono ya Nabii Isaya Mwana wa Amozi, na katika kitabu cha wafalme wa Yuda na Israeli.
33 Hezekiah died and was buried in the upper cemetery of David's descendants. All Judah and the people of Jerusalem honored him at his death. His son Manasseh took over as king.
Hezekia akalala pamaoja na babu zake, na wakamzika katika mlima wa makaburi ya vizazi vya Daudi. Yuda wote na wakaaji wa Yerusalemu wakamheshimu katika kifo chake. Manase mwanaye akawa mfalme katika nafasi yake.

< 2 Chronicles 32 >