< 1 Chronicles 19 >

1 Some time later, Nahash, king of the Ammonites, died and his son succeeded him.
Ikajakuwa baadae kwamba Nahashi, mfalme wa watu wa Amoni, akafa, na mwanae akawa mfalme baada yake.
2 David said, “I will be kind to Hanun, son of Nahash, for his father was kind to me.” So David sent messengers to comfort him over his father's death. David's ambassadors arrived in the land of the Ammonites and went comfort Hanun.
Daudi akasema, “Nitaonyesha ukarimu kwa mwana wa Hanuni wa Nahashi, kwasababu baba yake alionyesha ukarimu kwangu.” Hivyo Daudi akatuma wajumbe kumfariji kuhusu baba yake. Watumishi wa Daudi wakaingia nchi ya Waamoni na kumfuata Hanuni, ilikumfariji.
3 But the Ammonite princes said to Hanun, “Do you really think that David is honoring your father by sending comforters to you? Haven't these ‘comforters’ only come to spy out the land to find ways to conquer it?”
Lakini viongozi wakamwambia Hanuni, “Unadhani Daudi anamheshimu baba yako sababu ametuma watu kukufaraji? Je watumishi wake hawajaja kutadhimini nchi iliwaipindue?
4 So Hanun detained David's ambassadors and had them shaved, and their robes cut off at the buttocks. Then he sent them back.
Hanuni akawakamata watumishi wa Daudi, akawanyoa, akakata mavazi ya nusu kwenye kiuno kushuka, na kuwarudisha.
5 A message was sent to David to explain what had happened to the men. David then sent messengers to the men to tell them, “Stay at Jericho until your beards grow, and then you can come back.”
Walipo eleza haya kwa Daudi, alienda kukutana nao, kwa kuwa walifedheeka sana. Mfalme akasema, “Bakini Yeriko hadi ndevu zenu ziote tena, kisha mrudi.”
6 Then the Ammonites realized that they had really been offensive to David So Hanun and the Ammonites sent a thousand talents of silver to hire chariots and charioteers from Aram-naharaim, Aram-maacah, and Zobah.
Waamoni walipoona wamekuwa kikwazo kwa Daudi, Hanuni na Waamoni walituma talanta elfu moja za fedha kukodisha magari ya farasi kwa Waaremei na wanaume wa farasi kutoka Naharaimu, Maka, na Zoba.
7 They also hired 32,000 chariots and the king of Maacah with his army. They came set up camp near Medeba. The Ammonites were also called up from their towns and prepared for battle.
Waliwakodishia magari ya farasi elfu thelathini na mbili pamoja na mfalme wa Maka na watu wake, walio kuja na kueka kambi mbele ya Medeba. Waamoni walijikusanya pamoja kutoka miji yao, na wakaja kwa vita.
8 When David learned of this, he sent Joab and the entire army to confront them.
Daudi alipo sikia, alimtuma Yoabu na wanajeshi wake wote.
9 The Ammonites set up their battle lines near the town entrance, while the other kings who had joined them took up positions in the open fields.
Watu wa Amoni walikuja na kupanga mstari kwa ajili ya pambano katika lango la mji, wafalme waliokuja walikuwa peke yao katika shamba.
10 Joab realized he would have to fight both in front of him and behind him, he chose some of Israel's best troops and he took charge of them to lead the attack the Arameans.
Yoabu alipoona mistari ya pambano imemzunguka mbele na nyuma, alichagua wapambanaji shupavu wa Israeli na kuwa panga dhidi ya Waaremi.
11 He put the rest of the army under the command of Abishai, his brother. They were to attack the Ammonites.
Wanajeshi wengine wote, aliwaeka chini ya Abishai kaka yake, akawapanga kwa mstari dhidi ya Amoni.
12 Joab told him, “If the Arameans are stronger than me, you come and help me. If the Ammonites are stronger than you, I'll come and help you.
Yoabu akasema, “Kama Waaremi wananguvu kunizidi, kisha wewe, Abishai, lazima uniokoe. Lakini kama jeshi la Waamoni lina nguvu kukuzidi, nitakuja kukuokoa.
13 Be brave, and fight your best for our people and the towns of our God. May the Lord do what he sees as good!”
Kuwa thabiti, natujionyeshe kwa watu wetu kuwa ni wenye nguvu na kwa miji ya Mungu wetu, kwa kuwa Yahweh ata fanya lililo jema kwa kusudi lake.”
14 Joab attacked the Arameans with his forces and they ran away from him.
Hivyo Yoabu na wanajeshi wasogea kwenye pambano dhidi ya Waaremi, walio lazimika kukimbia mbele ya jeshi la Waisraeli.
15 When the Ammonites saw that the Arameans had run away, they also ran away from Abishai, Joab's brother, and retreated into the town. So Joab went back to Jerusalem.
Jeshi la Waamoni walipoona kuwa Waaremi wamekimbia, wao pia wakamkimbia kaka yake Yoabu Abishai na kurudi mjini. Kisha Yoabu akarudi kutoka kwa watu wa Amoni na kurudi Yerusalemu.
16 As soon as the Arameans saw they had been defeated by the Israelites so they sent for reinforcements from the other side of the Euphrates River, under the leadership of Shobach, commander of Hadadezer's army.
Waaremi walipoona kuwa wanashindwa na Waisraeli, wakatuma msaada nyuma ya Mto Frati, na Shofaki mkuu wajeshi la Hadadezeri.
17 When this was reported to David, he assembled all Israel together. He crossed the Jordan and approached the Aramean army, drawing up his forces in battle line against them. When David engaged in battle with them they fought with him.
Daudi alipo ambiwa haya, akakusanya Israeli yote, akuvuka Yordani, na kuja juu yao. Alipanga jeshi kwa ajili ya pambano dhidi ya Waaremi, na wakapigana nao.
18 But the Aramean army ran away from the Israelites, and David killed 7,000 charioteers and 40,000 infantry, as well as Shobach, their army commander.
Waaremi waliwakimbia Waisraeli, na Daudi akaua waendesha magari ya farasi ya Waaremi elfu saba na wanajeshi wa miguu elfu arobaini. Pia alimuua Shopaki, mkuu wa jeshi.
19 When Hadadezer's allies realized that they had been defeated by Israel, they made peace with David and became subject to him. As a result, the Arameans didn't want to help the Ammonites any more.
Wafalme wote walio kuwa watumishi wa Hadadezeri walipoona kuwa wameshindwa na Israeli, walifanya amani na Daudi na kumtumikia. Hivyo watu wa Aramu hawakuwa tayari kuwasaidia Waamoni.

< 1 Chronicles 19 >