< 1 Chronicles 10 >

1 The Philistines attacked Israel and all the Israelites soldiers ran away from them. Many Israelites were cut down on Mount Gilboa.
Wafilisti wakapigana dhidi ya Israeli. Kila mwanaume wa Israeli alikimbia Wafilisti na kuanguka na kufa katika Mlima Giliboa.
2 The Philistines chased down Saul and his sons. The killed Saul's sons Jonathan, Abinadab, and Malchishua.
Wafilisti waliwakimbiza Sauli na mwanae. Waflisti walimuua Yonathani, Abinadabu, na Malichishua, wana wake.
3 The battle raged intensely around Saul. The enemy archers saw where he was, and they wounded him.
Pambano lilikuwa zito kwa Sauli, na wapiga mishale wakamshambulia. Alipatwa na maumivu makali sababu ya wapiga mishale.
4 Saul told his armor bearer, “Take out your sword and kill me before these heathen come and torment me.” But his armor bearer refused—he was too afraid to do it. So Saul took his own sword and fell on it.
Kisha Sauli akasema kwa mbeba ngao wake, “Vuta upanga wako na unichome nao. Lasihivyo, hawa wasio tahiriwa watukuja na kunitesa”. Lakini mbeba ngao wake hakutaka, kwa kuwa aliogopa sana. Kwa hiyo Sauli akachukuwa upanga wake na kuuangukia.
5 When his armor bearer saw that Saul was dead, he also fell on his sword and died.
Mbeba ngao alivyoona kuwa Sauli amekufa, naye akaangukia upanga wake na kufa.
6 So Saul and three of his sons died there, along with his royal line.
Kwaiyo Sauli akafa, na wana wake watatu, wote wa nyumba yake wakafa pamoja.
7 When all the Israelites in the valley saw that their army had run away, and that Saul and his sons were dead, they abandoned their towns and they also ran away. The Philistines came and occupied them.
Kila mwanaume wa Israeli katika bonde alivyoona kuwa wamekimbia, na Sauli na wana wake wamekufa, walitelekeza miji yao na kukimbia. Kisha Wafilisti wakaja na kuishi humo.
8 The following day, when the Philistines came to strip the dead, they discovered the bodies of Saul and his sons on Mount Gilboa.
Ikawa siku inayofuata, Wafilisti walipo kuja kukagua wafu, walimkuta Sauli na wana wake wameanguka katika Mlima Giliboa.
9 They stripped him, cut off his head, and took his armor. Then they sent the news throughout the land of Philistia, to their idols and their people.
Wakamvua nguo zote na kuchukuwa kichwa chake na ngao yake. Wakatuma wajumbe wapeleke habari Filistia yote kwa miungu yao na watu wote.
10 They put Saul's armor in the temple of their idols and fixed his head to the temple of Dagon.
Ngao yake wakaeka ndani ya hekalu la miungu yao, na kichwa chake waka kining'iniza katika hekalu la Dagoni.
11 However, when everyone in Jabesh-gilead heard everything the Philistines had done to Saul,
Yabeshi Gileadi yote ilipo sikia Wafilisti waliyo mtendea Sauli,
12 all their fighting men went and recovered the bodies of Saul and his sons. They brought them back and buried them under the large tree in Jabesh. Then they fasted for seven days.
wanaume wote wa vita wakaenda na kuchukuwa mwili wa Sauli na hiyo ya wanae, na kuirejesha Yabeshi. Walizika mifupa yao chini ya mti huko Yabeshi na wakafunga siku saba.
13 Saul died because he was unfaithful to the Lord. He did not keep the Lord's commands, and he also went to consult a medium.
Kwaiyo Sauli akafa kwa kuwa hakuwa mwaminifu kwa Yahweh. Hakutii maelekezo ya Yahweh, lakini akauliza ushauri kwa mtu anaye ongea na wafu.
14 He did not consult the Lord, so the Lord put him to death and he handed over the kingship to David, son of Jesse.
Hakutafuta mwongozo kwa Yahweh, hivyo Yahweh akamua na kupindua ufalme kwa Daudi mwana wa Yese.

< 1 Chronicles 10 >