< 1 Chronicles 10 >

1 The Philistines attacked Israel and all the Israelites soldiers ran away from them. Many Israelites were cut down on Mount Gilboa.
Basi Wafilisti wakapigana na Israeli. Waisraeli wakawakimbia, na wengi wakauawa katika mlima Gilboa.
2 The Philistines chased down Saul and his sons. The killed Saul's sons Jonathan, Abinadab, and Malchishua.
Wafilisti wakawafuatia kwa bidii Sauli na wanawe, wakawaua Yonathani, Abinadabu na Malki-Shua.
3 The battle raged intensely around Saul. The enemy archers saw where he was, and they wounded him.
Mapigano yakawa makali kumzunguka Sauli na wakati wapiga mishale walipompata, wakamjeruhi.
4 Saul told his armor bearer, “Take out your sword and kill me before these heathen come and torment me.” But his armor bearer refused—he was too afraid to do it. So Saul took his own sword and fell on it.
Sauli akamwambia mbeba silaha wake, “Futa upanga wako unichome nao, la sivyo hawa watu wasiotahiriwa watakuja na kunidhalilisha.” Lakini mbeba silaha wake akaogopa sana wala hakuweza kufanya hivyo. Kwa hiyo Sauli akachukua upanga wake mwenyewe na kuuangukia.
5 When his armor bearer saw that Saul was dead, he also fell on his sword and died.
Mbeba silaha wake alipoona kwamba Sauli amekufa, naye pia akauangukia upanga wake akafa.
6 So Saul and three of his sons died there, along with his royal line.
Kwa hiyo Sauli na wanawe watatu wakafa, pamoja na nyumba yake yote.
7 When all the Israelites in the valley saw that their army had run away, and that Saul and his sons were dead, they abandoned their towns and they also ran away. The Philistines came and occupied them.
Waisraeli wote waliokuwa bondeni walipoona kwamba jeshi limekimbia na kwamba Sauli na wanawe wamekufa, waliacha miji yao wakakimbia. Nao Wafilisti wakaja na kukaa humo.
8 The following day, when the Philistines came to strip the dead, they discovered the bodies of Saul and his sons on Mount Gilboa.
Kesho yake Wafilisti walipokuja kuwavua maiti silaha, walimkuta Sauli na wanawe wameanguka katika Mlima Gilboa.
9 They stripped him, cut off his head, and took his armor. Then they sent the news throughout the land of Philistia, to their idols and their people.
Wakamvua mavazi, wakachukua kichwa chake pamoja na silaha zake, wakawatuma wajumbe katika nchi yote ya Wafilisti kutangaza habari hizi miongoni mwa sanamu zao na watu wao.
10 They put Saul's armor in the temple of their idols and fixed his head to the temple of Dagon.
Waliweka silaha zake katika hekalu la miungu yao, wakatundika kichwa chake katika hekalu la Dagoni.
11 However, when everyone in Jabesh-gilead heard everything the Philistines had done to Saul,
Wakazi wote wa Yabeshi-Gileadi waliposikia yote Wafilisti waliyomtendea Sauli,
12 all their fighting men went and recovered the bodies of Saul and his sons. They brought them back and buried them under the large tree in Jabesh. Then they fasted for seven days.
mashujaa wao wote wakaondoka, wakautwaa mwili wa Sauli na miili ya wanawe, wakaileta Yabeshi. Wakaizika mifupa yao chini ya mti mkubwa huko Yabeshi, nao wakafunga kwa siku saba.
13 Saul died because he was unfaithful to the Lord. He did not keep the Lord's commands, and he also went to consult a medium.
Sauli alikufa kwa sababu hakuwa mwaminifu kwa Bwana. Hakulishika neno la Bwana, hata akataka shauri kwa mwaguzi kwa ajili ya uongozi,
14 He did not consult the Lord, so the Lord put him to death and he handed over the kingship to David, son of Jesse.
hakumuuliza Bwana. Kwa hiyo Bwana alimuua, na ufalme akampa Daudi mwana wa Yese.

< 1 Chronicles 10 >