< Romans 10 >
1 Brothers, my heart's desire and prayer to God for Israel is for their salvation.
Ndugu zangu, shauku ya moyo wangu na maombi yangu kwa Mungu ni kwa ajili ya Waisraeli, kwamba waokolewe.
2 For I bear them witness that they have a zeal for God, but not according to real knowledge.
Kwa maana ninaweza nikashuhudia wazi kwamba wao wana juhudi kubwa kwa ajili ya Mungu, lakini juhudi yao haina maarifa.
3 For they, failing to understand God's righteousness and seeking to establish their own righteousness, have not submitted to God's righteousness.
Kwa kuwa hawakuijua haki itokayo kwa Mungu, wakatafuta kuweka haki yao wenyewe, hawakujitia chini ya haki ya Mungu.
4 Now for everyone who believes into righteousness, Christ is the end of the law
Kwa maana Kristo ni ukomo wa sheria ili kuwe na haki kwa kila mtu aaminiye.
5 —Moses writes about the righteousness that is from the law: “The person who does these things will live by them.”
Mose anaandika kuhusu haki ile itokanayo na sheria, kwamba, “Mtu atendaye matendo hayo ataishi kwa hayo.”
6 But the righteousness that is from faith speaks like this: “Do not say in your heart, ‘Who will ascend into heaven?’” (that is, to bring Christ down)
Lakini ile haki itokanayo na imani husema hivi: “Usiseme moyoni mwako, ‘Ni nani atakayepanda mbinguni?’” (yaani ili kumleta Kristo chini)
7 “or, ‘Who will descend into the abyss?’” (that is, to bring Christ up from the dead). (Abyssos )
“au ‘Ni nani atashuka kwenda kuzimu?’” (yaani ili kumleta Kristo kutoka kwa wafu.) (Abyssos )
8 So what does it say? “The message is near you, in your mouth and in your heart” (that is, the message of faith that we proclaim):
Lakini andiko lasemaje? “Lile neno liko karibu nawe, liko kinywani mwako na moyoni mwako,” yaani, lile neno la imani tunalolihubiri.
9 That if you confess with your mouth, “Jesus is Lord,” and believe in your heart that God raised Him from the dead, you will be saved.
Kwa sababu kama ukikiri kwa kinywa chako kwamba “Yesu ni Bwana,” na kuamini moyoni mwako kwamba Mungu alimfufua kutoka kwa wafu, utaokoka.
10 Because with the heart one believes into righteousness, and with the mouth one promises into salvation.
Kwa maana kwa moyo mtu huamini na hivyo kuhesabiwa haki, tena kwa kinywa mtu hukiri na hivyo kupata wokovu.
11 Because the Scripture says: “Everyone who believes on Him will never be put to shame”;
Kama yasemavyo Maandiko, “Yeyote amwaminiye hataaibika kamwe.”
12 because there is no distinction between Jew and Greek, since the same Lord of all is rich to all who call upon Him;
Kwa maana hakuna tofauti kati ya Myahudi na Myunani, yeye ni Bwana wa wote, mwenye utajiri kwa wote wamwitao.
13 because: “Everyone who calls on the name of the Lord will be saved.”
Kwa maana, “Kila mtu atakayeliitia Jina la Bwana, ataokolewa.”
14 How then will they call on Him in whom they have not believed? And how can they believe on Him of whom they have not heard? And how will they hear without someone proclaiming it?
Lakini watamwitaje yeye ambaye hawajamwamini? Nao watawezaje kumwamini yeye ambaye hawajamsikia? Tena watamsikiaje bila mtu kuwahubiria?
15 And how will they proclaim unless they are sent? As it is written: “How timely is the arrival of those who bring good news of peace, of those who announce the good things.”
Nao watahubirije wasipopelekwa? Kama ilivyoandikwa, “Tazama jinsi ilivyo mizuri miguu yao wale wanaohubiri habari njema!”
16 (However, they did not all obey the gospel; because Isaiah says: “Lord, who has believed our message?”)
Lakini si wote waliotii Habari Njema. Kwa maana Isaya asema, “Bwana, ni nani aliyeamini ujumbe wetu?”
17 So, the faith is from a message, and that message is by the Word of God.
Basi, imani chanzo chake ni kusikia, na kusikia huja kwa neno la Kristo.
18 But I say, did they really not hear? Indeed yes: “Their voice has gone out into all the earth, and their spoken words to the ends of the inhabited world.”
Lakini nauliza: Je, wao hawakusikia? Naam, wamesikia, kwa maana: “Sauti yao imeenea duniani pote, nayo maneno yao yameenea hadi miisho ya ulimwengu.”
19 Again I say, did Israel really not know? First Moses says: “I will provoke you to jealousy by a non-nation, I will move you to anger by a senseless nation.”
Nami nauliza tena: Je, Waisraeli hawakuelewa? Kwanza, Mose asema, “Nitawafanya mwe na wivu kwa watu wale ambao si taifa. Nitawakasirisha kwa taifa lile lisilo na ufahamu.”
20 But Isaiah is so bold as to say: “I was found by those who were not seeking me; I was revealed to those who were not asking for me.”
Naye Isaya kwa ujasiri mwingi anasema, “Nimeonekana na watu wale ambao hawakunitafuta. Nilijifunua kwa watu wale ambao hawakunitafuta.”
21 But concerning Israel he says: “All day long I have held out my hands to a disobedient and contrary people.”
Lakini kuhusu Israeli anasema, “Mchana kutwa nimewanyooshea watu wakaidi na wasiotii mikono yangu.”