< Luke 2 >
1 Now it happened in those days that a decree went out from Caesar Augustus that the whole inhabited world should be enrolled.
Siku zile, tangazo rasmi lilitolewa na Kaisari Augusto kuwataka watu wote chini ya utawala wake wajiandikishe.
2 This first census took place while Quirinius was governing Syria.
Kuandikishwa huku kulikuwa mara ya kwanza, wakati Kirenio alipokuwa mkuu wa mkoa wa Siria.
3 So everyone was traveling, each to his own town, to enroll himself.
Basi, wote waliohusika walikwenda kujiandikisha, kila mtu katika mji wake.
4 So Joseph also went up from Galilee, out of Natsareth town, into Judea to the city of David, that is called Bethlehem, because he was of David's ‘house’, that is, line of descent,
Yosefu pia alifanya safari kutoka mjini Nazareti mkoani Galilaya. Kwa kuwa alikuwa wa jamaa na ukoo wa Daudi alikwenda mjini Bethlehemu mkoani Yuda alikozaliwa Mfalme Daudi.
5 to enroll himself with Mary, the woman who had been betrothed to him, who was pregnant.
Alikwenda kujiandikisha pamoja na mchumba wake Maria ambaye alikuwa mja mzito.
6 So it happened that when they got there the days for her to give birth were completed;
Walipokuwa huko, siku yake ya kujifungua ikawadia,
7 and she gave birth to her firstborn Son, wrapped Him in pieces of cloth and laid Him in the manger, because there was no room for them in the lodging place.
akajifungua mtoto wake wa kwanza wa kiume, akamvika nguo za kitoto, akamlaza horini kwa sababu hawakupata nafasi katika nyumba ya wageni.
8 Now there were shepherds in that same area, staying out in the field and keeping the nightly watches over their flock.
Katika sehemu hizo, walikuwako wachungaji wakikesha usiku mbugani kulinda mifugo yao.
9 When wow, an angel of the Lord stood before them, and the glory of the Lord shone around them, and they were terrified.
Malaika wa Bwana akawatokea ghafla, na utukufu wa Bwana ukawaangazia pande zote. Wakaogopa sana.
10 The angel said to them: “Do not be afraid because listen, I am announcing the most joyful news to you, which will be to all the people!
Malaika akawaambia, “Msiogope! Nimewaleteeni habari njema ya furaha kuu kwa watu wote.
11 You see, today, in David's city, a Savior was born to you, who is Lord Christ!
Kwa maana, leo hii katika mji wa Daudi, amezaliwa Mwokozi kwa ajili yenu, ndiye Kristo Bwana.
12 And this is the sign to you: you will find a Baby wrapped in pieces of cloth, lying in a manger.”
Na hiki kitakuwa kitambulisho kwenu: mtamkuta mtoto mchanga amevikwa nguo za kitoto, amelazwa horini.”
13 Suddenly a multitude of the heavenly army was with the angel praising God and saying,
Mara kundi kubwa la jeshi la mbinguni likajiunga na huyo malaika, wakamsifu Mungu wakisema:
14 “Glory to God in the highest and on earth peace, good will toward mankind!”
“Utukufu kwa Mungu juu mbinguni, na amani duniani kwa watu aliopendezwa nao!”
15 So when the angels went away from them into the sky the men, the shepherds, said to one another, “Hey, let's go to Bethlehem and see this event that has taken place, that the Lord made known to us!”
Baada ya hao malaika kuondoka na kurudi mbinguni, wachungaji wakaambiana: “Twendeni moja kwa moja mpaka Bethlehemu tukalione tukio hili Bwana alilotujulisha.”
16 So they went in a hurry and located both Mary and Joseph, and the Baby lying in the manger.
Basi, wakaenda mbio, wakamkuta Maria na Yosefu na yule mtoto mchanga amelazwa horini.
17 And having seen they spread an exact account of the saying that had been spoken to them concerning this Child.
Hao wachungaji walipomwona mtoto huyo wakawajulisha wote habari waliyokuwa wamesikia juu yake.
18 All who heard marveled at the things told them by the shepherds.
Wote waliosikia hayo walishangaa juu ya habari walizoambiwa na wachungaji.
19 As for Mary, she treasured all these sayings, pondering them in her heart.
Lakini Maria aliyaweka na kuyatafakari mambo hayo yote moyoni mwake.
20 The shepherds returned, glorifying and praising God over all that they had heard and seen, just as it was told them.
Wale wachungaji walirudi makwao huku wakimtukuza na kumsifu Mungu kwa yote waliyokuwa wamesikia na kuona; yote yalikuwa kama walivyokuwa wameambiwa.
21 When eight days were completed so as to circumcise Him, His name was indeed called JESUS, the name given by the angel before He was conceived in the womb.
Siku nane baadaye, wakati wa kumtahiri mtoto ulipofika, walimpa jina Yesu, jina ambalo alikuwa amepewa na malaika kabla hajachukuliwa mimba.
22 And when the days of their purification according to the law of Moses were completed, they took Him to Jerusalem to present Him to the Lord
Siku zilipotimia za Yosefu na Maria kutakaswa kama walivyotakiwa na Sheria ya Mose, wazazi hao walimchukua mtoto, wakaenda naye Yerusalemu ili wamweke mbele ya Bwana.
23 (just as it is written in the law of the Lord, “Every male who opens a womb shall be called holy to the Lord”),
Katika Sheria ya Bwana imeandikwa: “Kila mzaliwa wa kwanza wa kiume atawekwa wakfu kwa Bwana.”
24 and to offer a sacrifice according to what was specified in the Lord's Law, “a pair of turtledoves or two young pigeons”.
Pia walikwenda ili watoe sadaka: hua wawili au makinda wawili ya njiwa, kama ilivyotakiwa katika Sheria ya Bwana.
25 Well now, there was a man in Jerusalem whose name was Simeon; this man was righteous and devout, expectantly waiting for the Consolation of Israel, and Holy Spirit was upon him.
Wakati huo huko Yerusalemu kulikuwa na mtu mmoja, mwema na mcha Mungu, jina lake Simeoni. Yeye alikuwa akitazamia kwa hamu ukombozi wa Israeli. Roho Mtakatifu alikuwa pamoja naye.
26 (It had been revealed to him repeatedly by the Holy Spirit that he would not see death until he saw the Lord's Messiah.)
Roho Mtakatifu alikuwa amemhakikishia kwamba hatakufa kabla ya kumwona Masiha wa Bwana.
27 So by the Spirit he came into the temple; and when the parents brought the Child Jesus in, to do concerning Him according to the custom of the law,
Basi, akiongozwa na Roho Mtakatifu, Simeoni aliingia Hekaluni; na wazazi wa Yesu walipomleta Hekaluni mtoto wao ili wamfanyie kama ilivyotakiwa na Sheria,
28 Simeon took Him into his arms and blessed God and said:
Simeoni alimpokea mtoto Yesu mikononi mwake huku akimtukuza Mungu na kusema:
29 “Sovereign, now You can release your slave in peace, according to Your word,
“Sasa Bwana, umetimiza ahadi yako, waweza kumruhusu mtumishi wako aende kwa amani.
30 because my eyes have seen Your salvation,
Maana kwa macho yangu nimeuona wokovu utokao kwako,
31 which You have prepared before the face of all peoples:
ambao umeutayarisha mbele ya watu wote:
32 a light for revelation to Gentiles, and the glory of Your people Israel.”
Mwanga utakaowaangazia watu wa mataifa, na utukufu kwa watu wako Israeli.”
33 And Joseph and His mother were marveling at the things being spoken concerning Him.
Baba na mama yake Yesu walikuwa wakistaajabia maneno aliyosema Simeoni juu ya mtoto.
34 Then Simeon blessed them, and said to Mary His mother: “Listen, this One is appointed to bring about the fall and rising of many in Israel, and to be a sign that is spoken against,
Simeoni akawabariki, akamwambia Maria mama yake, “Mtoto huyu atakuwa sababu ya kupotea na kuokoka kwa watu wengi katika Israeli. Naye atakuwa ishara itakayopingwa na watu;
35 so that the reasonings of many hearts may be revealed (furthermore, a sword will pass through your own soul also).”
na hivyo mawazo ya watu wengi yataonekana wazi. Nawe mwenyewe, uchungu ulio kama upanga mkali utauchoma moyo wako.”
36 Also there was a prophetess Anna, a daughter of Phanuel, of the tribe of Asher—she was of a great age, having lived with a husband seven years from her virginity
Palikuwa na nabii mmoja mwanamke, mzee sana, jina lake Ana, binti Fanueli, wa kabila la Asheri. Alikuwa ameishi na mumewe kwa miaka saba tangu alipoolewa.
37 and having been a widow for about eighty-four years—who did not depart from the temple, serving God with fastings and petitions night and day.
Halafu alibaki mjane hadi wakati huo akiwa mzee wa miaka themanini na minne. Wakati huo wote alikaa Hekaluni akifunga na kusali usiku na mchana.
38 Well she, having come up at that very moment, started praising the Lord, and kept on speaking of Him to all those in Jerusalem who were looking for redemption.
Saa hiyohiyo alijitokeza mbele, akamshukuru Mungu, na akaeleza habari za huyo mtoto kwa watu wote waliokuwa wanatazamia ukombozi wa Yerusalemu.
39 When they had completed everything, according to the law of the Lord, they went back to Galilee, to their own town, Natsareth.
Hao wazazi walipokwisha fanya yote yaliyoamriwa na Sheria ya Bwana, walirudi makwao Nazareti, mkoani Galilaya.
40 And the Child kept growing and being strengthened in spirit, being filled with wisdom; yes, the grace of God was upon Him.
Mtoto akakua, akazidi kupata nguvu, akajaa hekima, na neema ya Mungu ilikuwa pamoja naye.
41 Now every year His parents would go to Jerusalem to the feast of the Passover;
Wazazi wa Yesu walikuwa na desturi ya kwenda Yerusalemu kila mwaka wakati wa sikukuu ya Pasaka.
42 so when He was twelve years old they went up to Jerusalem according to the custom of the feast.
Mtoto alipokuwa na umri wa miaka kumi na miwili, wote walikwenda kwenye sikukuu hiyo kama ilivyokuwa desturi.
43 When they had fulfilled the days, as they were returning, the boy Jesus stayed behind in Jerusalem, but Joseph and His mother did not know it.
Baada ya sikukuu, walianza safari ya kurudi makwao, lakini Yesu alibaki Yerusalemu bila wazazi wake kuwa na habari.
44 Supposing Him to be in the caravan, they went a day's journey and then started looking for Him among their relatives and acquaintances.
Walidhani alikuwa pamoja na kundi la wasafiri, wakaenda mwendo wa kutwa, halafu wakaanza kumtafuta miongoni mwa jamaa na marafiki.
45 Not finding Him, they returned to Jerusalem seeking Him.
Kwa kuwa hawakumwona, walirudi Yerusalemu wakimtafuta.
46 So it happened that after three days they found Him in the temple, sitting in the midst of the teachers, both listening to them and asking them questions.
Siku ya tatu walimkuta Hekaluni kati ya walimu, akiwasikiliza na kuwauliza maswali.
47 (All who heard Him were astonished at His understanding and answers.)
Wote waliosikia maneno yake walistaajabia akili yake na majibu yake ya hekima.
48 So upon seeing Him they were amazed, and His mother said to Him: “Son, why have you treated us like this? Look, your father and I have been searching for you in distress.”
Wazazi wake walipomwona walishangaa. Maria, mama yake, akamwuliza, “Mwanangu, kwa nini umetutenda hivyo? Baba yako na mimi tumekuwa tukikutafuta kwa huzuni.”
49 So He said to them: “Why were you seeking me? Didn't you know that I must be about my Father's concerns?”
Yeye akawajibu, “Kwa nini mlinitafuta? Hamkujua kwamba inanipasa kuwa katika nyumba ya Baba yangu?”
50 But they did not understand the statement that He made to them.
Lakini wazazi wake hawakuelewa maana ya maneno aliyowaambia.
51 Then He went down with them and came to Natsareth, and continued subordinating Himself to them; His mother kept all these sayings in her heart.
Basi, akarudi pamoja nao hadi Nazareti, akawa anawatii. Mama yake akaweka mambo hayo yote moyoni mwake.
52 And Jesus kept increasing in wisdom and stature, and in favor with God and men.
Naye Yesu akaendelea kukua katika hekima na kimo; akazidi kupendwa na Mungu na watu.