< Ruth 4 >
1 Then Booz went up to the gate, and sat there. And when he had seen the kinsman going by, of whom he had spoken before, he said to him, calling him by his name: Turn aside for a little while, and sit down here. He turned aside, and sat down.
Ndipo Boazi akaenda kwenye lango la Bethelehemu na kukaa chini. Muda mfupi tu akaja ndugu wa karibu ambaye Boazi alimuongelea. Boazi akamwambia, “Rafiki yangu, njoo hapa na uketi. Kisha mtu huyo akaja na kuketi.
2 And Booz taking ten men of the ancients of the city, said to them: Sit ye down here.
Ndipo Boazi akakusanya viongozi kumi wa mji na kusema, “Katini hapa.” Hivyo wakaketi.
3 They sat down, and he spoke to the kinsman: Noemi, who is returned from the country of Moab, will sell a parcel of land that belonged to our brother Elimelech.
Boazi alimwambia yule jamaa wa karibu, “Naomi aliyerudi kutoka mji wa Moabu, anauza sehemu ya aridhi ambayo ilikuwa ni miliki ya kaka yetu Elimeleki.
4 I would have thee to understand this, and would tell thee before all that sit here, and before the ancients of my people. If thou wilt take possession of it by the right of kindred: buy it and possess it: but if it please thee not, tell me so, that I may know what I have to do. For there is no near kinsman besides thee, who art first, and me, who am second. But he answered: I will buy the field.
Nilifikiria kukujulisha na kukwambia, 'Inunue mbele ya hawa waliokaa hapa, na mbele ya viongozi wa watu wangu.' Ikiwa utapenda kuikomboa, ikomboe. Lakini ikiwa hauhitaji kuikomboa, uniambie, ili nijue, kwa kuwa hakuna mwingine wa kuikomboa isipokuwa wewe, na mimi ni mdogo wako.” Ndipo huyo mtu mwingine akasema, “Nitalikomboa.”
5 And Booz said to him: When thou shalt buy the field at the woman’s hand, thou must take also Ruth the Moabitess, who was the wife of the deceased: to raise up the name of thy kinsman in his inheritance.
Kisha Boazi akasema, “Ile siku utakayonunua shamba kutoka mkononi mwa Naomi, yakupasa pia kumchukua Ruth Mmoabu, mjane wa mtoto wa Elimeleki, ili kuliinua jina la marehemu kama urithi wake.”
6 He answered: I yield up my right of next akin: for I must not cut off the posterity of my own family. Do thou make use of my privilege, which I profess I do willingly forego.
Ndipo yule jamaa wa karibu akasema, “Mimi siwezi kuikomboa ardhi kwa ajili yangu bila kuleta athari kwenye urithi wangu binafsi. Nakupa wewe haki ya kuikomboa kwa ajili yako mwenyewe, kwa kuwa mimi sitoweza.”
7 Now this in former times was the manner in Israel between kinsmen, that if at any time one yielded his right to another: that the grant might be sure, the man put off his shoe, and gave it to his neighhour; this was a testimony of cession of right in Israel.
Hii ilikuwa ni desturi ya zamani ya Israeli kuhusu ukombozi na kubadilishana mazuri. Kudhibitisha mambo haya yote, mtu huyu alivua kiatu chake na kumpatia jirani yake; hii ilikuwa ni namna ya kufanya makubaliano ya kisheria katika Israeli.
8 So Booz said to his kinsman: Put off thy shoe. And immediately he took it off from his foot.
Kwa hiyo huyu jamaa wa karibu akamwambia Boazi, “Inunue mwenyewe.” Kisha akavua kiatu chake.
9 And he said to the ancients and to all the people: You are witnesses this day, that I have bought all that was Elimelech’s, and Chelion’s, and Mahalon’s, of the hand of Noemi:
Ndipo Boazi akawaambia viongozi na watu wote, “Ninyi ni mashaidi kuwa nimenunua kila kilichokuwa cha Elimeleki na kila kilichokuwa na Kileoni na Mahilon kutoka kwenye mikono ya Naomi.
10 And have taken to wife Ruth the Moabitess, the wife of Mahalon, to raise up the name of the deceased in his inheritance lest his name be cut off, from among his family and his brethren and his people. You, I say, are witnesses of this thing.
Zaidi ya hayo kumhusu Ruth Mmoabu, mke wa Mahlon: nimempa kibali cha kuwa mke wangu, ili kuendeleza jina na urithi wa marehumu, ili kwamba jina lake lisipotee kati ya ndugu zake na lango la watu wake. Ninyi ni mashahidi leo.”
11 Then all the people that were in the gate, and the ancients answered: We are witnesses: The Lord make this woman who cometh into thy house, like Rachel, and Lia, who built up the house of Israel: that she may be an example of virtue in Ephrata, and may have a famous name in Bethlehem:
Watu wote na viongozi waliokuwa katika lango, walisema, “Tu mashahidi. Yahweh amfanye mwanamke huyu ambaye amekuja nyumbani kwako kama Raheli na Leya, ambao wawili hawa wameijenga nyumba ya Israeli. Na ubarikiwe katika Efrata na kuwa mashuhuri katika Bethelehem.
12 And that the house may be, as the house of Phares, whom Thamar bore unto Juda, of the seed which the Lord shall give thee of this young woman.
Na nyumba yako kama nyumba ya Peres, ambaye Tamari alimzalia yuda, kupitia uzao ambao Yahweh atakupatia pamoja na msichana huyu.”
13 Booz therefore took Ruth, and married her: and went in unto her, and the Lord gave her to conceive and to bear a son.
Hivyo Boazi alimchukua Ruth, na akawa mke wake. Boazi alilala naye, na Yahweh alimruhusu kupata mimba, na alizaa mtoto wa kiume.
14 And the women said to Noemi: Blessed be the Lord, who hath not suffered thy family to want a successor, that his name should be preserved in Israel.
Wanamke huyu akamwambia Naomi, “Yahweh abarikiwe, ambaye hajakuacha bila ndugu wa karibu, yaani mtoto huyu. Jina lake na liwe maarufu katika Israeli.
15 And thou shouldst have one to comfort thy soul, and cherish thy old age. For he is born of thy daughter in law: who loveth thee: and is much better to thee, than if thou hadst seven sons.
Na awe kwako mrutubishaji wa maisha na mwenye ruzuku uzeeni mwako, kwa kuwa mtoto wako mkwe, ambaye anakupenda, ambaye ni bora kwako kuliko watoto wa kiume saba, amemzaa.
16 And Noemi taking the child laid it in her bosom, and she carried it, and was a nurse unto it.
Kisha naomi akamchukua mtoto, akamlaza kifuani pake, na kumhudumia.
17 And the women her neighbours, congratulating with her and saying: There is a son born to Noemi: called his name Obed: he is the father of Isai, the father of David.
Na majirani wa yule mwanamke, wakampa jina, wakisema, “Mtoto amezaliwa kwa Naomi.” Wakawita Obedi. Ambaye alikuja kuwa baba yake na Jese, ambaye alikuja kuwa baba yake na Daudi.
18 These are the generations of Phares: Phares begot Esron,
Hiki kilikuwa ni kizazi cha Peresi: Peres alimzaa Hezroni,
19 Esron begot Aram, Aram begot Aminadab,
Hezroni akamzaa Ram, Ram akamzaa Aminadabu,
20 Aminadab begot Nahasson, Nahasson begot Salmon,
Aminadabu akamzaa Nashon, Nashon akamzaa Salmon,
21 Salmon begot Booz, Booz begot Obed,
Salmon akamzaa Boazi, Boazi akamzaa Obed,
22 Obed begot Isai, Isai begot David.
Obedi akamzaa Jese, na Jese akamzaa Daudi.