< Romans 2 >
1 Wherefore thou art inexcusable, O man, whosoever thou art that judgest. For wherein thou judgest another, thou condemnest thyself. For thou dost the same things which thou judgest.
Kwa hiyo huna udhuru wowote, wewe utoaye hukumu kwa mwingine, kwa maana katika jambo lolote unalowahukumu wengine, unajihukumu wewe mwenyewe kwa sababu wewe unayehukumu unafanya mambo hayo hayo.
2 For we know that the judgment of God is, according to truth, against them that do such things.
Basi tunajua kwamba hukumu ya Mungu dhidi ya wale wafanyao mambo kama hayo ni ya kweli.
3 And thinkest thou this, O man, that judgest them who do such things, and dost the same, that thou shalt escape the judgment of God?
Hivyo wewe mwanadamu, utoapo hukumu juu yao na bado unafanya mambo yale yale, unadhani utaepuka hukumu ya Mungu?
4 Or despisest thou the riches of his goodness, and patience, and longsuffering? Knowest thou not, that the benignity of God leadeth thee to penance?
Au waudharau wingi wa wema, ustahimili na uvumilivu wake, bila kujua kuwa wema wa Mungu wakuelekeza kwenye toba?
5 But according to thy hardness and impenitent heart, thou treasurest up to thyself wrath, against the day of wrath, and revelation of the just judgment of God.
Lakini kwa sababu ya ukaidi wenu na mioyo yenu isiyotaka kutubu, mnajiwekea akiba ya ghadhabu dhidi yenu wenyewe kwa siku ile ya ghadhabu ya Mungu, wakati hukumu yake ya haki itakapodhihirishwa.
6 Who will render to every man according to his works.
Kwa maana Mungu atamlipa kila mtu sawasawa na matendo yake.
7 To them indeed, who according to patience in good work, seek glory and honour and incorruption, eternal life: (aiōnios )
Wale ambao kwa kuvumilia katika kutenda mema hutafuta utukufu, heshima na maisha yasiyoharibika, Mungu atawapa uzima wa milele. (aiōnios )
8 But to them that are contentious, and who obey not the truth, but give credit to iniquity, wrath and indignation.
Lakini kwa wale watafutao mambo yao wenyewe na wale wanaokataa kweli na kuzifuata njia mbaya, kutakuwa na ghadhabu na hasira ya Mungu.
9 Tribulation and anguish upon every soul of man that worketh evil, of the Jew first, and also of the Greek.
Kutakuwa na taabu na dhiki kwa kila mmoja atendaye maovu, Myahudi kwanza na mtu wa Mataifa pia,
10 But glory, and honour, and peace to every one that worketh good, to the Jew first, and also to the Greek.
bali utukufu, heshima na amani kwa ajili ya kila mmoja atendaye mema, kwa Myahudi kwanza, kisha kwa mtu wa Mataifa.
11 For there is no respect of persons with God.
Kwa maana Mungu hana upendeleo.
12 For whosoever have sinned without the law, shall perish without the law; and whosoever have sinned in the law, shall be judged by the law.
Watu wote waliotenda dhambi pasipo sheria wataangamia pasipo sheria, nao wote wale waliotenda dhambi chini ya sheria watahukumiwa kwa sheria.
13 For not the hearers of the law are just before God, but the doers of the law shall be justified.
Kwa maana si wale wanaoisikia sheria ambao ni wenye haki mbele za Mungu, bali ni wale wanaoitii sheria ndio watakaohesabiwa haki.
14 For when the Gentiles, who have not the law, do by nature those things that are of the law; these having not the law are a law to themselves:
(Naam, wakati wa watu wa Mataifa, ambao hawana sheria, wanapofanya kwa asili mambo yatakiwayo na sheria, wao ni sheria kwa nafsi zao wenyewe, hata ingawa hawana sheria.
15 Who shew the work of the law written in their hearts, their conscience bearing witness to them, and their thoughts between themselves accusing, or also defending one another,
Wao wanaonyesha kwamba lile linalotakiwa na sheria limeandikwa kwenye mioyo yao, ambayo pia dhamiri zao zikiwashuhudia, nayo mawazo yao yenye kupingana yatawashtaki au kuwatetea.)
16 In the day when God shall judge the secrets of men by Jesus Christ, according to my gospel.
Hili litatukia siku hiyo Mungu atakapozihukumu siri za wanadamu kwa njia ya Yesu Kristo, kama isemavyo Injili yangu.
17 But if thou art called a Jew and restest in the law, and makest thy boast of God,
Tazama, wewe ukiwa unaitwa Myahudi na kuitegemea sheria na kujisifia uhusiano wako na Mungu,
18 And knowest his will, and approvest the more profitable things, being instructed by the law,
kama unajua mapenzi ya Mungu na kukubali lililo bora kwa sababu umefundishwa na hiyo sheria,
19 Art confident that thou thyself art a guide of the blind, a light of them that are in darkness,
kama unatambua kuwa wewe ni kiongozi wa vipofu, na mwanga kwa wale walio gizani,
20 An instructor of the foolish, a teacher of infants, having the form of knowledge and of truth in the law.
mkufunzi wa wajinga na mwalimu wa watoto wachanga, kwa kuwa una maarifa ya kweli katika hiyo sheria,
21 Thou therefore that teachest another, teachest not thyself: thou that preachest that men should not steal, stealest:
basi wewe, uwafundishaye wengine, mbona hujifunzi mwenyewe? Wewe uhubiriye kwamba mtu asiibe, wewe mwenyewe waiba?
22 Thou that sayest, men should not commit adultery, committest adultery: thou that abhorrest idols, committest sacrilege:
Wewe usemaye mtu asizini, wewe mwenyewe wazini? Wewe uchukiaye miungu ya sanamu, wafanya jambo la kumchukiza katika mahekalu?
23 Thou that makest thy boast of the law, by transgression of the law dishonourest God.
Wewe ujivuniaye sheria, wamwaibisha Mungu kwa kuvunja sheria?
24 (For the name of God through you is blasphemed among the Gentiles, as it is written.)
Kama ilivyoandikwa, “Kwa ajili yenu ninyi, Jina la Mungu linatukanwa miongoni mwa watu wa Mataifa.”
25 Circumcision profiteth indeed, if thou keep the law; but if thou be a transgressor of the law, thy circumcision is made uncircumcision.
Kutahiriwa kuna thamani ikiwa unatii sheria, lakini kama unavunja sheria, kutahiriwa kwako kumekuwa kutokutahiriwa.
26 If, then, the uncircumcised keep the justices of the law, shall not this uncircumcision be counted for circumcision?
Hivyo, ikiwa wale wasiotahiriwa wanatimiza mambo ambayo sheria inataka, je, kutokutahiriwa kwao hakutahesabiwa kuwa sawa na kutahiriwa?
27 And shall not that which by nature is uncircumcision, if it fulfill the law, judge thee, who by the letter and circumcision art a transgressor of the law?
Ndipo wale ambao hawakutahiriwa kimwili lakini wanaitii sheria watawahukumu ninyi, ambao ingawa mmetahiriwa na kuijua sana sheria ya Mungu iliyoandikwa, lakini mwaivunja.
28 For it is not he is a Jew, who is so outwardly; nor is that circumcision which is outwardly in the flesh:
Kwa maana mtu si Myahudi kwa vile alivyo kwa nje, wala tohara ya kweli si kitu cha nje au cha kimwili.
29 But he is a Jew, that is one inwardly; and the circumcision is that of the heart, in the spirit, not in the letter; whose praise is not of men, but of God.
Lakini mtu ni Myahudi alivyo ndani, nayo tohara ya kweli ni jambo la moyoni, ni la Roho, wala si la sheria iliyoandikwa. Mtu wa namna hiyo hapokei sifa kutoka kwa wanadamu bali kwa Mungu.