< Psalms 96 >

1 A canticle for David himself, when the house was built after the captivity. Sing ye to the Lord a new canticle: sing to the Lord, all the earth.
Mwimbieni Bwana wimbo mpya; mwimbieni Bwana dunia yote.
2 Sing ye to the Lord and bless his name: shew forth his salvation from day to day.
Mwimbieni Bwana, lisifuni jina lake; tangazeni wokovu wake siku baada ya siku.
3 Declare his glory among the Gentiles: his wonders among all people.
Tangazeni utukufu wake katikati ya mataifa, matendo yake ya ajabu miongoni mwa mataifa yote.
4 For the Lord is great, and exceedingly to be praised: he is to be feared above all gods.
Kwa kuwa Bwana ni mkuu mwenye kustahili kusifiwa kuliko wote; yeye ni wa kuogopwa kuliko miungu yote.
5 For all the gods of the Gentiles are devils: but the Lord made the heavens.
Kwa maana miungu yote ya mataifa ni sanamu, lakini Bwana aliziumba mbingu.
6 Praise and beauty are before him: holiness and majesty in his sanctuary.
Fahari na enzi viko mbele yake; nguvu na utukufu vimo patakatifu pake.
7 Bring ye to the Lord, O ye kindreds of the Gentiles, bring ye to the Lord glory and honour:
Mpeni Bwana, enyi jamaa za mataifa, mpeni Bwana utukufu na nguvu.
8 Bring to the Lord glory unto his name. Bring up sacrifices, and come into his courts:
Mpeni Bwana utukufu unaostahili jina lake; leteni sadaka na mje katika nyua zake.
9 Adore ye the Lord in his holy court. Let all the earth be moved at his presence.
Mwabuduni Bwana katika uzuri wa utakatifu wake; dunia yote na itetemeke mbele zake.
10 Say ye among the Gentiles, the Lord hath reigned. For he hath corrected the world, which shall not be moved: he will judge the people with justice.
Katikati ya mataifa semeni, “Bwana anatawala.” Ulimwengu ameuweka imara, hauwezi kusogezwa; atawahukumu watu kwa uadilifu.
11 Let the heavens rejoice, and let the earth be glad, let the sea be moved, and the fulness thereof:
Mbingu na zishangilie, nchi na ifurahi; bahari na ivume, na vyote vilivyomo ndani yake;
12 The fields and all things that are in them shall be joyful. Then shall all the trees of the woods rejoice
mashamba na yashangilie, pamoja na vyote vilivyomo ndani yake. Kisha miti yote ya msituni itaimba kwa furaha;
13 Before the face of the Lord, because he cometh: because he cometh to judge the earth. He shall judge the world with justice, and the people with his truth.
itaimba mbele za Bwana kwa maana anakuja, anakuja kuihukumu dunia. Ataihukumu dunia kwa haki, na mataifa katika kweli yake.

< Psalms 96 >