< Psalms 87 >

1 For the sons of Core, a psalm of a canticle. The foundations thereof are in the holy mountains:
Zaburi ya wana wa Kora. Wimbo. Ameuweka msingi wake katika mlima mtakatifu;
2 The Lord loveth the gates of Sion above all the tabernacles of Jacob.
Bwana anayapenda malango ya Sayuni kuliko makao yote ya Yakobo.
3 Glorious things are said of thee, O city of God.
Mambo matukufu yanasemwa juu yako, ee mji wa Mungu:
4 I will be mindful of Rahab and of Babylon knowing me. Behold the foreigners, and Tyre, and the people of the Ethiopians, these were there.
“Nitaweka kumbukumbu ya Rahabu na Babeli miongoni mwa wale wanaonikubali mimi: Ufilisti pia na Tiro, pamoja na Kushi, nami nitasema, ‘Huyu alizaliwa Sayuni.’”
5 Shall not Sion say: This man and that man is born in her? and the Highest himself hath founded her.
Kuhusu Sayuni itasemwa hivi, “Huyu na yule walizaliwa humo, naye Aliye Juu Sana mwenyewe atamwimarisha.”
6 The Lord shall tell in his writings of peoples and of princes, of them that have been in her.
Bwana ataandika katika orodha ya mataifa: “Huyu alizaliwa Sayuni.”
7 The dwelling in thee is as it were of all rejoicing.
Watakapokuwa wanapiga vinanda wataimba, “Chemchemi zangu zote ziko kwako.”

< Psalms 87 >