< Psalms 83 >

1 A canticle of a psalm for Asaph. O God, who shall be like to thee? hold not thy peace, neither be thou still, O God.
Ee Mungu, usikae kimya! usitupuuze na kustarehe, Ee Mungu.
2 For lo, thy enemies have made a noise: and they that hate thee have lifted up the head.
Tazama, adui zako wanafanya vurugu, na wale wakuchukiao wameinua vichwa vyao.
3 They have taken a malicious counsel against thy people, and have consulted against thy saints.
Wanafanya hila juu ya watu wako na kwa pamoja kupanga njama dhidi ya wale uwalindao. Wamesema,
4 They have said: Come and let us destroy them, so that they be not a nation: and let the name of Israel be remembered no more.
“Njoni na tuwaangamize wao kama taifa. Kisha jina la Israeli halitakumbukwa.”
5 For they have contrived with one consent: they have made a covenant together against thee,
Wamepanga njama pamoja wakiwa na mkakati mmoja; wamefanya muungano dhidi yako.
6 The tabernacles of the Edomites, and the Ismahelites: Moab, and the Agarens,
Hii inajumuisha hema za Edomu na Waishmaeli, na watu wa Moabu na Wahagari, ambao wamepanga njama pamoja nao
7 Gebal, and Ammon and Amalec: the Philistines, with the inhabitants of Tyre.
Gebal, Amoni, Amaleki; pia inajumuisha Filisti na wenyeji wa Tiro.
8 Yea, and the Assyrian also is joined with them: they are come to the aid of the sons of Lot.
Ashuri pia ameshirikina nao; wanawasaidia wana wa Lutu. Serah
9 Do to them as thou didst to Madian and to Sisara: as to Jabin at the brook of Cisson.
Ufanye kwao kama ulivyofanya kwa Midiani, kama ulivyofanya kwa Sisera na kwa Yabini kwenye Mto Kishoni.
10 Who perished at Endor: and became as dung for the earth.
Waliangamizwa kule Endori na wakawa kama mbolea juu ya chi.
11 Make their princes like Oreb, and Zeb, and Zebee, and Salmana. All their princes,
Uvifanye vyeo vyao kama Oreb na Zeeb, na wakuu wao wote kama Zeba na Zalmuna.
12 Who have said: Let us possess the sanctuary of God for an inheritance.
Wao walisema, natujimilikishe malisho ya Mungu.”
13 O my God, make them like a wheel; and as stubble before the wind.
Ee Mungu wangu, uwafanye kama mavumbi ya kisulisuli, kama makapi mbele ya upepo,
14 As fire which burneth the wood: and as a flame burning mountains:
Kama moto uteketezao msitu, na kama miali ya moto iwakayo milimani.
15 So shalt thou pursue them with thy tempest: and shalt trouble them in thy wrath.
Uwafuatie kwa tufani yako, na kuwafadhaisha kwa dhoruba yako.
16 Fill their faces with shame; and they shall seek thy name, O Lord.
Uwajaze nyuso zao kwa aibu ili kwamba waweze kulitafuta jina lako, Yahwe.
17 Let them be ashamed and troubled for ever and ever: and let them be confounded and perish.
Nao waaibishwe na kufadhaishwa milele; waangamizwe katika aibu.
18 And let them know that the Lord is thy name: thou alone art the most High over all the earth.
Kisha watajua kwamba ni wewe pekee, Yahwe, Uliye Juu ya nchi yote.

< Psalms 83 >