< Psalms 80 >

1 Unto the end, for them that shall he changed, a testimony for Asaph, a psalm. Give ear, O thou that rulest Israel: thou that leadest Joseph like a sheep. Thou that sittest upon the cherubims, shine forth
Usikie, Mchungaji wa Israel, wewe uliye muongoza Yusufu kama kundi; wewe uketiye juu ya makerubi, utuangazie!
2 Before Ephraim, Benjamin, and Manasses. Stir up thy might, and come to save us.
Machoni pa Efraimu na Benjamini na Manase, uziinue nguvu zako; njoo na utuokoe.
3 Convert us, O God: and shew us thy face, and we shall be saved.
Mungu, uturejeshe sisi; uangaze uso wako juu yetu, nasi tutaokolewa.
4 O Lord God of hosts, how long wilt thou be angry against the prayer of thy servant?
Yahwe Mungu wa majeshi, mpaka lini utawakasirikia watu wako wanapoomba?
5 How long wilt thou feed us with the bread of tears: and give us for our drink tears in measure?
Umewalisha wa mkate wa machozi na umewapa machozi ili wanywe katika kiasi kikubwa.
6 Thou hast made us to be a contradiction to our neighbours: and our enemies have scoffed at us.
Umetufanya kitu kwa ajili ya majirani zetu kubishania, na maadui zetu hucheka kuhusu sisi kati yao.
7 O God of hosts, convert us: and shew thy face, and we shall be saved.
Mungu wa majeshi, uturejeshe sisi; nasi tutaokolewa.
8 Thou hast brought a vineyard out of Egypt: thou hast cast cut the Gentiles and planted it.
Wewe ulileta mzabibu kutoka Misri; ukawafukuza mataifa na ukaupanda.
9 Thou wast the guide of its journey in its sight: thou plantedst the roots thereof, and it filled the land.
Uliisafisha ardhi kwa ajil yake; nao ulipata mzizi na kuijaza nchi.
10 The shadow of it covered the hills: and the branches thereof the cedars of God.
Milima ilifunikwa kwa kivuli chake, mierezi ya Mungu kwa matawi yake.
11 It stretched forth its branches unto the sea, and its boughs unto the river.
Ilieneza matawi yake mbali kama bahari na mashina yake mpaka kwenye Mto Euphrates.
12 Why hast thou broken down the hedge thereof, so that all they who pass by the way do pluck it?
Kwa nini umezibomoa kuta zake hata wapitao karibu huyachuma matunda yake.
13 The boar out of the wood hath laid it waste: and a singular wild beast hath devoured it.
Ngurue wa msituni wanauharibu, na wanyama wa kondeni wanaula.
14 Turn again, O God of hosts, look down from heaven, and see, and visit this vineyard:
Urudi, Ee Mungu wa majeshi; kutoka mbinguni utazame chini na uuangalie na kuujali huu mzabibu.
15 And perfect the same which thy right hand hath planted: and upon the son of man whom thou hast confirmed for thyself.
Huu ni mzizi ambao mkono wako wa kuume umeupanda, mashina ambayo wewe uliyafanya yakue.
16 Things set on fire and dug down shall perish at the rebuke of thy countenance.
Yamekatwa na kuchomwa; yameangamia kwa sababu ya kukemea kwako.
17 Let thy hand be upon the man of thy right hand: and upon the son of man whom thou hast confirmed for thyself.
Mkono wako na uwe juu ya mtu aliye mkono wako wa kuume, kwa mwana wa mtu uliyemfanya imara kwa ajili yako mwenyewe.
18 And we depart not from thee, thou shalt quicken us: and we will call upon thy name.
Ndipo hatuta kuacha wewe; utuhuishe, nasi tutaliita jina lako.
19 O Lord God of hosts, convert us: and shew thy face, and we shall be saved.
Yahwe, Mungu wa majeshi, uturejeshe sisi; utuangazie nuru ya uso wako, nasi tutaokolewa.

< Psalms 80 >