< Psalms 78 >

1 Understanding for Asaph. Attend, O my people, to my law: incline your ears to the words of my mouth.
Utenzi wa Asafu. Enyi watu wangu, sikieni mafundisho yangu, sikilizeni maneno ya kinywa changu.
2 I will open my mouth in parables: I will utter propositions from the beginning.
Nitafungua kinywa changu kwa mafumbo, nitazungumza mambo yaliyofichika, mambo ya kale:
3 How great things have we heard and known, and our fathers have told us.
yale ambayo tuliyasikia na kuyajua, yale ambayo baba zetu walituambia.
4 They have not been hidden from their children, in another generation. Declaring the praises of the Lord, and his powers, and his wonders which he hath done.
Hatutayaficha kwa watoto wao; tutakiambia kizazi kijacho matendo yastahiliyo sifa ya Bwana, uweza wake, na maajabu aliyoyafanya.
5 And he set up a testimony in Jacob: and made a law in Israel. How great things he commanded our fathers, that they should make the same known to their children:
Aliagiza amri kwa Yakobo na akaweka sheria katika Israeli, ambazo aliwaamuru baba zetu wawafundishe watoto wao,
6 That another generation might know them. The children that should be born and should rise up, and declare them to their children.
ili kizazi kijacho kizijue, pamoja na watoto ambao watazaliwa, nao pia wapate kuwaeleza watoto wao.
7 That they may put their hope in God and may not forget the works of God: and may seek his commandments.
Ndipo wangeweka tumaini lao kwa Mungu, nao wasingesahau matendo yake, bali wangalizishika amri zake.
8 That they may not become like their fathers, a perverse and exasperating generation. A generation that set not their heart aright: and whose spirit was not faithful to God.
Ili wasifanane na baba zao, waliokuwa kizazi cha ukaidi na uasi, ambao roho zao hazikuwa na uaminifu kwake, ambao roho zao hazikumwamini.
9 The sons of Ephraim who bend and shoot with the bow: they have turned back in the day of battle.
Watu wa Efraimu, ingawa walijifunga pinde, walikimbia siku ya vita.
10 They kept not the covenant of God: and in his law they would not walk.
Hawakulishika agano la Mungu na walikataa kuishi kwa sheria yake.
11 And they forgot his benefits, and his wonders that he had shewn them.
Walisahau aliyokuwa ameyatenda, maajabu aliyokuwa amewaonyesha.
12 Wonderful things did he do in the sight of their fathers, in the land of Egypt, in the field of Tanis.
Alitenda miujiza machoni mwa baba zao, huko Soani, katika nchi ya Misri.
13 He divided the sea and brought them through: and he made the waters to stand as in a vessel.
Aliigawanya bahari akawapitisha, alifanya maji yasimame imara kama ukuta.
14 And he conducted them with a cloud by day: and all the night with a light of fire.
Aliwaongoza kwa wingu mchana na kwa nuru kutoka kwenye moto usiku kucha.
15 He struck the rock in the wilderness: and gave them to drink, as out of the great deep.
Alipasua miamba jangwani na akawapa maji tele kama bahari,
16 He brought forth water out of the rock: and made streams run down as rivers.
alitoa vijito kutoka kwenye jabali lililochongoka, akayafanya maji yatiririke kama mito.
17 And they added yet more sin against him: they provoked the most High to wrath in the place without water.
Lakini waliendelea kutenda dhambi dhidi yake, wakiasi jangwani dhidi ya Aliye Juu Sana.
18 And they tempted God in their hearts, by asking meat for their desires.
Kwa makusudi walimjaribu Mungu, wakidai vyakula walivyovitamani.
19 And they spoke ill of God: they said: Can God furnish a table in the wilderness?
Walinena dhidi ya Mungu, wakisema, “Je, Mungu aweza kuandaa meza jangwani?
20 Because he struck the rock, and the waters gushed out, and the streams overflowed. Can he also give bread, or provide a table for his people?
Alipopiga mwamba, maji yalitoka kwa nguvu, vijito vikatiririka maji mengi. Lakini je, aweza kutupa chakula pia? Je, anaweza kuwapa watu wake nyama?”
21 Therefore the Lord heard, and was angry: and a fire was kindled against Jacob, and wrath came up against Israel.
Bwana alipowasikia, alikasirika sana, moto wake ukawa dhidi ya Yakobo, na ghadhabu yake ikawaka dhidi ya Israeli,
22 Because they believed not in God: and trusted not in his salvation.
kwa kuwa hawakumwamini Mungu, wala kuutumainia ukombozi wake.
23 And he had commanded the clouds from above, and had opened the doors of heaven.
Hata hivyo alitoa amri kwa anga zilizo juu na kufungua milango ya mbingu,
24 And had rained down manna upon them to eat, and had given them the bread of heaven.
akawanyeshea mana ili watu wale; aliwapa nafaka ya mbinguni.
25 Man ate the bread of angels: he sent them provisions in abundance.
Watu walikula mkate wa malaika, akawatumia chakula chote ambacho wangeliweza kula.
26 He removed the south wind from heaven: and by his power brought in the southwest wind.
Aliachia upepo wa mashariki kutoka kwenye mbingu na kuuongoza upepo wa kusini kwa uwezo wake.
27 And he rained upon them flesh as dust: and feathered fowls like as the sand of the sea.
Aliwanyeshea nyama kama mavumbi, ndege warukao kama mchanga wa pwani.
28 And they fell in the midst of their camp, round about their pavilions.
Aliwafanya washuke ndani ya kambi yao, kuzunguka mahema yao yote.
29 So they did eat, and were filled exceedingly, and he gave them their desire:
Walikula na kusaza, kwa maana alikuwa amewapa kile walichotamani.
30 They were not defrauded of that which they craved. As yet their meat was in their mouth:
Kabla hawajamaliza kula walichokitamani, hata kilipokuwa kingali bado vinywani mwao,
31 And the wrath of God came upon them. And he slew the fat ones amongst them, and brought down the chosen men of Israel.
hasira ya Mungu ikawaka juu yao, akawaua wale waliokuwa na nguvu zaidi miongoni mwao, akiwaangusha vijana wa Israeli.
32 In all these things they sinned still: and they believed not for his wondrous works.
Licha ya haya yote, waliendelea kutenda dhambi, licha ya maajabu yake, hawakuamini.
33 And their days were consumed in vanity, and their years in haste.
Kwa hiyo akamaliza siku zao katika ubatili na miaka yao katika vitisho.
34 When he slew them, then they sought him: and they returned, and came to him early in the morning.
Kila mara Mungu alipowaua baadhi yao, waliosalia walimtafuta, walimgeukia tena kwa shauku.
35 And they remembered that God was their helper: and the most high God their redeemer.
Walikumbuka kwamba Mungu alikuwa Mwamba wao, kwamba Mungu Aliye Juu Sana alikuwa Mkombozi wao.
36 And they loved him with their mouth: and with their tongue they lied unto him:
Lakini walimdanganya kwa vinywa vyao, wakisema uongo kwa ndimi zao,
37 But their heart was not right with him: nor were they counted faithful in his covenant.
mioyo yao haikuwa thabiti kwake, wala hawakuwa waaminifu katika agano lake.
38 But he is merciful, and will forgive their sins: and will not destroy them. And many a time did he turn away his anger: and did not kindle all his wrath.
Hata hivyo alikuwa na huruma, alisamehe maovu yao na hakuwaangamiza. Mara kwa mara alizuia hasira yake, wala hakuchochea ghadhabu yake yote.
39 And he remembered that they are flesh: a wind that goeth and returneth not.
Alikumbuka kwamba wao walikuwa nyama tu, upepo upitao ambao haurudi.
40 How often did they provoke him in the desert: and move him to wrath in the place without water?
Mara ngapi walimwasi jangwani na kumhuzunisha nyikani!
41 And they turned back and tempted God: and grieved the holy one of Israel.
Walimjaribu Mungu mara kwa mara, wakamkasirisha yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.
42 They remembered not his hand, in the day that he redeemed them from the hand of him that afflicted them:
Hawakukumbuka uwezo wake, siku aliyowakomboa kutoka kwa mtesi,
43 How he wrought his signs in Egypt, and his wonders in the field of Tanis.
siku aliyoonyesha ishara zake za ajabu huko Misri, maajabu yake huko Soani.
44 And he turned their rivers into blood, and their showers that they might, not drink.
Aligeuza mito yao kuwa damu, hawakuweza kunywa maji kutoka vijito vyao.
45 He sent amongst them divers sores of flies, which devoured them: and frogs which destroyed them.
Aliwapelekea makundi ya mainzi yakawala, na vyura wakawaharibu.
46 And he gave up their fruits to the blast, and their labours to the locust.
Aliruhusu tunutu kuharibu mimea yao, mazao yao kwa nzige.
47 And he destroyed their vineyards with hail, and their mulberry trees with hoarfrost.
Aliharibu mizabibu yao kwa mvua ya mawe na mikuyu yao kwa mvua iliyochangamana na theluji.
48 And he gave up their cattle to the hail, and their stock to the fire.
Aliwaachia mifugo yao mvua ya mawe, akayapiga makundi ya wanyama wao kwa radi.
49 And he sent upon them the wrath of his indignation: indignation and wrath and trouble, which he sent by evil angels.
Aliwafungulia hasira yake kali, ghadhabu yake, hasira na uadui, na kundi la malaika wa kuharibu.
50 He made a way for a path to his anger: he spared not their souls from death, and their cattle he shut up in death.
Aliitengenezea njia hasira yake, hakuwaepusha na kifo, bali aliwaachia tauni.
51 And he killed all the firstborn in the land of Egypt: the firstfruits of all their labour in the tabernacles of Cham.
Aliwapiga wazaliwa wote wa kwanza wa Misri, matunda ya kwanza ya ujana katika mahema ya Hamu.
52 And he took away his own people as sheep: and guided them in the wilderness like a flock.
Lakini aliwatoa watu wake kama kundi, akawaongoza kama kondoo kupitia jangwani.
53 And he brought them out in hope, and they feared not: band the sea overwhelmed their enemies.
Aliwaongoza salama, wala hawakuogopa, bali bahari iliwameza adui zao.
54 And he brought them into the mountain of his sanctuary: the mountain which his right hand had purchased. And he cast out the Gentiles before them: and by lot divided to them their land by a line of distribution.
Hivyo akawaleta hadi kwenye mpaka wa nchi yake takatifu, hadi nchi ya vilima ambayo mkono wake wa kuume ulikuwa umeitwaa.
55 And he made the tribes of Israel to dwell in their tabernacles.
Aliyafukuza mataifa mbele yao, na kuwagawia nchi zao kama urithi, aliwakalisha makabila ya Israeli katika makao yao.
56 Yet they tempted, and provoked the most high God: and they kept not his testimonies.
Lakini wao walimjaribu Mungu, na kuasi dhidi ya Yeye Aliye Juu Sana, wala hawakuzishika sheria zake.
57 And they turned away, and kept not the covenant: even like their fathers they were turned aside as a crooked bow.
Kama baba zao, hawakuwa thabiti wala waaminifu, wakawa wasioweza kutegemewa kama upinde wenye kasoro.
58 They provoked him to anger on their hills: and moved him to jealousy with their graven things.
Wakamkasirisha Mungu kwa mahali pao pa juu pa kuabudia miungu, wakachochea wivu wake kwa sanamu zao.
59 God heard, and despised them, and he reduced Israel exceedingly as it were to nothing.
Wakati Mungu alipowasikia, alikasirika sana, akamkataa Israeli kabisa.
60 And he put away the tabernacle of Silo, his tabernacle where he dwelt among men.
Akaiacha hema ya Shilo, hema aliyokuwa ameiweka katikati ya wanadamu.
61 And he delivered their strength into captivity: and their beauty into the hands of the enemy.
Akalipeleka Sanduku la nguvu zake utumwani, utukufu wake mikononi mwa adui.
62 And he shut up his people under the sword: and he despised his inheritance.
Aliachia watu wake wauawe kwa upanga, akaukasirikia sana urithi wake.
63 Fire consumed their young men: and their maidens were not lamented.
Moto uliwaangamiza vijana wao, na wanawali wao hawakuimbiwa nyimbo za arusi,
64 Their priests fell by the sword: and their widows did not mourn.
makuhani wao waliuawa kwa upanga, wala wajane wao hawakuweza kulia.
65 And the Lord was awaked as one out of sleep, and like a mighty man that hath been surfeited with wine.
Ndipo Bwana alipoamka kama vile kuamka usingizini, kama vile mtu aamkavyo kutoka kwenye bumbuazi la mvinyo.
66 And he smote his enemies on the hinder parts: he put them to an everlasting reproach.
Aliwapiga na kuwashinda adui zake, akawatia katika aibu ya milele.
67 And he rejected the tabernacle of Joseph: and chose not the tribe of Ephraim:
Ndipo alipozikataa hema za Yosefu, hakulichagua kabila la Efraimu,
68 But he chose the tribe of Juda, mount Sion which he loved.
lakini alilichagua kabila la Yuda, Mlima Sayuni, ambao aliupenda.
69 And he built his sanctuary as of unicorns, in the land which he founded for ever.
Alijenga patakatifu pake kama vilele, kama dunia ambayo aliimarisha milele.
70 And he chose his servant David, and took him from the hocks of sheep: he brought him from following the ewes great with young,
Akamchagua Daudi mtumishi wake na kumtoa kwenye mazizi ya kondoo.
71 To feed Jacob his servant, and Israel his inheritance.
Kutoka kuchunga kondoo alimleta kuwa mchungaji wa watu wake Yakobo, wa Israeli urithi wake.
72 And he fed them in the innocence of his heart: and conducted them by the skillfulness of his hands.
Naye Daudi aliwachunga kwa uadilifu wa moyo, kwa mikono ya ustadi aliwaongoza.

< Psalms 78 >