< Psalms 75 >

1 Unto the end, corrupt not, a psalm of a canticle for Asaph. We will praise thee, O God: we will praise, and we will call upon thy name. We will relate thy wondrous works:
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Usiharibu!” Zaburi ya Asafu. Wimbo. Ee Mungu, tunakushukuru, tunakushukuru wewe, kwa kuwa jina lako li karibu; watu husimulia matendo yako ya ajabu.
2 When I shall take a time, I will judge justices.
Unasema, “Ninachagua wakati maalum; ni mimi nihukumuye kwa haki.
3 The earth is melted, and all that dwell therein: I have established the pillars thereof.
Wakati dunia na watu wake wote inapotetemeka, ni mimi ninayezishikilia nguzo zake imara.
4 I said to the wicked: Do not act wickedly: and to the sinners: Lift not up the horn.
Kwa wale wenye majivuno ninasema, ‘Msijisifu tena,’ kwa wale waovu, ‘Msiinue pembe zenu.
5 Lift not up your horn on high: speak not iniquity against God.
Msiinue pembe zenu dhidi ya mbingu; msiseme kwa shingo zilizonyooshwa.’”
6 For neither from the east, nor from the west, nor from the desert hills:
Hakuna yeyote atokaye mashariki wala magharibi au kutoka jangwani awezaye kumkweza mwanadamu.
7 For God is the judge. One he putteth down, and another he lifteth up:
Bali Mungu ndiye ahukumuye: Humshusha huyu na kumkweza mwingine.
8 For in the hand of the Lord there is a cup of strong wine full of mixture. And he hath poured it out from this to that: but the dregs thereof are not emptied: all the sinners of the earth shall drink.
Mkononi mwa Bwana kuna kikombe kilichojaa mvinyo unaotoka povu uliochanganywa na vikolezo; huumimina, nao waovu wote wa dunia hunywa mpaka tone la mwisho.
9 But I will declare for ever: I will sing to the God of Jacob.
Bali mimi, nitatangaza hili milele; nitaimba sifa kwa Mungu wa Yakobo.
10 And I will break all the horns of sinners: but the horns of the just shall be exalted.
Nitazikatilia mbali pembe za waovu wote, bali pembe za wenye haki zitainuliwa juu.

< Psalms 75 >