< Psalms 73 >

1 A psalm for Asaph. How good is God to Israel, to them that are of a right heart!
Hakika Mungu ni mwema kwa Israeli, kwa wale walio na moyo safi.
2 But my feet were almost moved; my steps had well nigh slipped.
Lakini kwangu mimi, kidogo tu miguu yangu iteleze; miguu yangu karibu iteleze kutoka kwangu
3 Because I had a zeal on occasion of the wicked, seeing the prosperity of sinners.
kwa sababu niliwaonea wivu wenye kiburi nilipoona mafanikio ya waovu.
4 For there is no regard to their death, nor is there strength in their stripes.
Kwa maana hawana maumivu hadi kufa kwao, lakini wana nguvu na wameshiba.
5 They are not in the labour of men: neither shall they be scourged like other men.
Wako huru dhidi ya mizigo ya watu wengine; nao hawateswi kama watu wengine.
6 Therefore pride hath held them fast: they are covered with their iniquity and their wickedness.
Kiburi kinawapamba kama mkufu kwenye shingo zao; jeuri huwavika kama vazi.
7 Their iniquity hath come forth, as it were from fatness: they have passed into the affection of the heart.
Katika upofu wa jinsi hii dhambi huja; mawazo maovu hupita mioyoni mwao.
8 They have thought and spoken wickedness: they have spoken iniquity on high.
Wao hudhihaki na kuongea kwa namna ya uovu; kwa kiburi chao hutishia mateso.
9 They have set their mouth against heaven: and their tongue hath passed through the earth.
Wameweka vinywa vyao dhidi ya mbingu, na ndimi zao hutanga tanga duniani.
10 Therefore will my people return here and full days shall be found in them.
Kwa hiyo watu wake huwageukia na maji yaliyojaa hukaushwa.
11 And they said: How doth God know? and is there knowledge in the most High?
Nao husema, “Mungu anajuaje? Yako maarifa kwake yeye aliye juu?”
12 Behold these are sinners; and yet abounding in the world they have obtained riches.
Fahamu: watu hawa ni waovu; mara zote hawajali, wakifanyika matajiri na matajiri.
13 And I said: Then have I in vain justified my heart, and washed my hands among the innocent.
Hakika nimeutunza moyo wangu bure na nimenawa mikono yangu pasipo kukosa.
14 And I have been scourged all the day; and my chastisement hath been in the mornings.
Maana mchana kutwa nimeteswa na kuadhibiwa kila asubuhi.
15 If I said: I will speak thus; behold I should condemn the generation of thy children.
Kama ningesema, “Ningesema mambo haya,” kumbe nigewasaliti kizazi hiki cha watoto wenu.
16 I studied that I might know this thing, it is a labour in my sight:
Ingawa nilijaribu kuyaelewa mambo haya, yalikuwa ni magumu sana kwangu.
17 Until I go into the sanctuary of God, and understand concerning their last ends.
Ndipo nilipoingia patakatifu pa Mungu na kuelewa hatma yao.
18 But indeed for deceits thou hast put it to them: when they were lifted up thou hast cast them down.
Hakika wewe huwaweka penye utelezi; huwaangusha mpaka palipoharibika.
19 How are they brought to desolation? they have suddenly ceased to be: they have perished by reason of their iniquity.
Jinsi gani wamekuwa ukiwa kwa muda mfupi! Wamefika mwisho nao wamemaliza kwa utisho.
20 As the dream of them that awake, O Lord; so in thy city thou shalt bring their image to nothing.
Wao ni kama ndoto wakati wa mtu kuamka; Bwana, utakapo inuka, utazidharau ndoto zao.
21 For my heart hath been inflamed, and my reins have been changed:
Maana moyo wangu ulipata uchungu, nami nilijeruhiwa sana.
22 And I am brought to nothing, and I knew not.
Nilikuwa mjinga na sijui neno; nilikuwa kama mnyama tu mbele yako.
23 I am become as a beast before thee: and I am always with thee.
Lakini mimi nipo pamoja nawe daima; umenishika mkono wa kuume.
24 Thou hast held me by my right hand; and by thy will thou hast conducted me, and with thy glory thou hast received me.
Utaniongoza kwa shauri lako na baadaye utanipokea katika utukufu.
25 For what have I in heaven? and besides thee what do I desire upon earth?
Ni nani niliye naye mbinguni isipokuwa wewe? Hakuna nimtamaniye duniani isipokuwa wewe.
26 For thee my flesh and my heart hath fainted away: thou art the God of my heart, and the God that is my portion for ever.
Mwili wangu na moyo wangu huwa dhaifu, bali Mungu ndiye nguvu ya moyo wangu daima.
27 For behold they that go far from thee shall perish: thou hast destroyed all them that are disloyal to thee.
Wale walio mbali nawe wataangamia; utawaangamiza wote wasio waaminifu kwako.
28 But it is good for me to adhere to my God, to put my hope in the Lord God: That I may declare all thy praises, in the gates of the daughter of Sion.
Lakini mimi, linipasalo kufanya ni kumkaribia Mungu. Nimemfanya Bwana Yahwe kimbilio langu. Nami nitayatangaza matendo yako yote.

< Psalms 73 >