< Psalms 68 >

1 Unto the end, a psalm of a canticle for David himself. Let God arise, and let his enemies be scattered: and let them that hate him flee from before his face.
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Wimbo. Mungu na ainuke, watesi wake watawanyike, adui zake na wakimbie mbele zake.
2 As smoke vanisheth, so let them vanish away: as wax melteth before the fire, so let the wicked perish at the presence of God.
Kama vile moshi upeperushwavyo na upepo, vivyo hivyo uwapeperushe mbali, kama vile nta iyeyukavyo kwenye moto, vivyo hivyo waovu na waangamie mbele za Mungu.
3 And let the just feast, and rejoice before God: and be delighted with gladness.
Bali wenye haki na wafurahi, washangilie mbele za Mungu, wafurahi na kushangilia.
4 Sing ye to God, sing a psalm to his name, make a way for him who ascendeth upon the west: the Lord is his name. Rejoice ye before him: but the wicked shall be troubled at his presence,
Mwimbieni Mungu, liimbieni sifa jina lake, mtukuzeni yeye aendeshwaye juu ya mawingu: jina lake ni Bwana, furahini mbele zake.
5 Who is the father of orphans, and the judge of widows. God in his holy place:
Baba wa yatima, mtetezi wa wajane, ni Mungu katika makao yake matakatifu.
6 God who maketh men of one manner to dwell in a house: Who bringeth out them that were bound in strength; in like manner them that provoke, that dwell in sepulchres.
Mungu huwaweka wapweke katika jamaa, huwaongoza wafungwa wakiimba, bali waasi huishi katika nchi kame.
7 O God, when thou didst go forth in the sight of thy people, when thou didst pass through the desert:
Ee Mungu, ulipowatangulia watu wako, ulipopita nyikani,
8 The earth was moved, and the heavens dropped at the presence of the God of Sina, at the presence of the God of Israel.
dunia ilitikisika, mbingu zikanyesha mvua, mbele za Mungu, Yule wa Sinai, mbele za Mungu, Mungu wa Israeli.
9 Thou shalt set aside for thy inheritance a free rain, O God: and it was weakened, but thou hast made it perfect.
Ee Mungu, ulinyesha mvua nyingi na kuiburudisha ardhi iliyokuwa imechoka.
10 In it shall thy animals dwell; in thy sweetness, O God, thou hast provided for the poor.
Ee Mungu, watu wako waliishi huko, nawe kwa wingi wa utajiri wako uliwapa maskini mahitaji yao.
11 The Lord shall give the word to them that preach good tidings with great power.
Bwana alitangaza neno, waliolitangaza neno hilo walikuwa kundi kubwa:
12 The king of powers is of the beloved, of the beloved; and the beauty of the house shall divide spoils.
“Wafalme na majeshi walikimbia upesi, watu waliobaki kambini waligawana nyara.
13 If you sleep among the midst of lots, you shall be as the wings of a dove covered with silver, and the hinder parts of her back with the paleness of gold.
Hata ulalapo katikati ya mioto ya kambini, mabawa ya njiwa wangu yamefunikwa kwa fedha, manyoya yake kwa dhahabu ingʼaayo.”
14 When he that is in heaven appointeth kings over her, they shall be whited with snow in Selmon.
Wakati Mwenyezi alipowatawanya wafalme katika nchi, ilikuwa kama theluji iliyoanguka juu ya Salmoni.
15 The mountain of God is a fat mountain. A curdled mountain, a fat mountain.
Milima ya Bashani ni milima iliyotukuka, milima ya Bashani ina vilele vilivyochongoka.
16 Why suspect, ye curdled mountains? A mountain in which God is well pleased to dwell: for there the Lord shall dwell unto the end.
Enyi milima yenye vilele vilivyochongoka, kwa nini mnakazia macho kwa wivu, katika mlima Mungu anaochagua kutawala, ambako Bwana mwenyewe ataishi milele?
17 The chariot of God is attended by ten thousands; thousands of them that rejoice: the Lord is among them in Sina, in the holy place.
Magari ya Mungu ni makumi ya maelfu, na maelfu ya maelfu; Bwana amekuja kutoka Sinai hadi katika patakatifu pake.
18 Thou hast ascended on high, thou hast led captivity captive; thou hast received gifts in men. Yea for those also that do not believe, the dwelling of the Lord God.
Ulipopanda juu, uliteka mateka, ukapokea vipawa kutoka kwa wanadamu, hata kutoka kwa wale walioasi, ili wewe, Ee Bwana Mungu, upate kuishi huko.
19 Blessed be the Lord day by day: the God of our salvation will make our journey prosperous to us.
Sifa apewe Bwana, Mungu Mwokozi wetu, ambaye siku kwa siku hutuchukulia mizigo yetu.
20 Our God is the God of salvation: and of the Lord, of the Lord are the issues from death.
Mungu wetu ni Mungu aokoaye, Bwana Mwenyezi hutuokoa na kifo.
21 But God shall break the heads of his enemies: the hairy crown of them that walk on in their sins.
Hakika Mungu ataponda vichwa vya adui zake, vichwa vya hao waendao katika njia za dhambi.
22 The Lord said: I will turn them from Basan, I will turn them into the depth of the sea:
Bwana alisema, “Nitawarudisha kutoka Bashani; nitawarudisha kutoka vilindi vya bahari,
23 That thy foot may be dipped in the blood of thy enemies; the tongue of thy dogs be red with the same.
ili uweze kuchovya miguu yako katika damu ya adui zako, huku ndimi za mbwa wako zikiwa na fungu lake.”
24 They have seen thy goings, O God, the goings of my God: of my king who is in his sanctuary.
Ee Mungu, maandamano yako yameonekana, maandamano ya Mungu wangu, Mfalme wangu, yakielekea patakatifu pake.
25 Princes went before joined with singers, in the midst of young damsels playing on timbrels.
Mbele wako waimbaji, baada yao wapiga vinanda, pamoja nao wako wanawali wakipiga matari.
26 In the churches bless ye God the Lord, from the fountains of Israel.
Msifuni Mungu katika kusanyiko kubwa, msifuni Bwana katika kusanyiko la Israeli.
27 There is Benjamin a youth, in ecstasy of mind. The princes of Juda are their leaders: the princes of Zabulon, the princes of Nephthali.
Liko kabila dogo la Benyamini likiwaongoza, wakifuatwa na kundi kubwa la watawala wa Yuda, hatimaye watawala wa Zabuloni na Naftali.
28 Command thy strength, O God: confirm, O God, what thou hast wrought in us.
Ee Mungu, amuru uwezo wako, Ee Mungu tuonyeshe nguvu zako, kama ulivyofanya hapo awali.
29 From thy temple in Jerusalem, kings shall offer presents to thee.
Kwa sababu ya Hekalu lako Yerusalemu wafalme watakuletea zawadi.
30 Rebuke the wild beasts of the reeds, the congregation of bulls with the kine of the people; who seek to exclude them who are tried with silver. Scatter thou the nations that delight in wars:
Mkemee mnyama aliyeko kwenye manyasi, kundi la mafahali katikati ya ndama za mataifa. Na walete minara ya madini ya fedha wakinyenyekea. Tawanya mataifa yapendayo vita.
31 Ambassadors shall come out of Egypt: Ethiopia shall soon stretch out her hands to God.
Wajumbe watakuja kutoka Misri, Kushi atajisalimisha kwa Mungu.
32 Sing to God, ye kingdoms of the earth: sing ye to the Lord: Sing ye to God,
Mwimbieni Mungu, enyi falme za dunia, mwimbieni Bwana sifa,
33 Who mounteth above the heaven of heavens, to the east. Behold he will give to his voice the voice of power:
mwimbieni sifa yeye apandaye mbingu za kale zilizo juu, yeye angurumaye kwa sauti kuu.
34 Give ye glory to God for Israel, his magnificence, and his power is in the clouds.
Tangazeni uwezo wa Mungu, ambaye fahari yake iko juu ya Israeli, ambaye uwezo wake uko katika anga.
35 God is wonderful in his saints: the God of Israel is he who will give power and strength to his people. Blessed be God.
Ee Mungu, wewe unatisha katika mahali patakatifu pako, Mungu wa Israeli huwapa watu wake uwezo na nguvu. Mungu Asifiwe!

< Psalms 68 >