< Psalms 46 >
1 Unto the end, for the sons of Core, for the hidden. Our God is our refuge and strength: a helper in troubles, which have found us exceedingly.
Mungu kwetu ni kimbilio la usalama na nguvu, upatikanao tele wakati wa mateso.
2 Therefore we will not fear, when the earth shall be troubled; and the mountains shall be removed into the heart of the sea.
Hivyo hatutaogopa, hata kama dunia italazimika kubadilika, hata kama milima italazimika kutetemeka na kuangukia kwenye mtima wa bahari, hata kama maji yatavuma kwa kishindo kikuu,
3 Their waters roared and were troubled: the mountains were troubled with his strength.
hata kama milima itatetemeka kwa vurugu ya maji. (Selah)
4 The stream of the river maketh the city of God joyful: the most High hath sanctified his own tabernacle.
Kuna mto, mikondo yake huufanya mji wa Mungu kufurahi, mahali patakatifu pa hema ya Aliye Juu.
5 God is in the midst thereof, it shall not be moved: God will help it in the morning early.
Mungu yuko katikati yake; naye hatasogezwa; Mungu atamsaidia, naye atafanya hivyo asubuhi na mapema.
6 Nations were troubled, and kingdoms were bowed down: he uttered his voice, the earth trembled.
Mataifa yalikasirika na falme zikataharuki; yeye alipaza sauti yake, na nchi ikayeyuka.
7 The Lord of armies is with us: the God of Jacob is our protector.
Yahwe wa majeshi yuko pamoja nasi; Mungu wa Yakobo ni kimbilio letu la usalama. (Selah)
8 Come and behold ye the works of the Lord: what wonders he hath done upon earth,
Njoni, mtazame matendo ya Yahwe, uharibifu alioufanya juu ya nchi.
9 Making wars to cease even to the end of the earth. He shall destroy the bow, and break the weapons: and the shield he shall burn in the fire.
Anaisitisha vita kwenye nchi; yeye anauvunja upinde na kuikata vipande vipande mishale; anazichoma ngao.
10 Be still and see that I am God; I will be exalted among the nations, and I will be exalted in the earth.
Mkae kimya na mjue kuwa mimi ni Mungu; nitainuliwa juu ya nchi.
11 The Lord of armies is with us: the God of Jacob is our protector.
Mungu wa majeshi yuko pamoja nasi; Mungu wa Yakobo ni kimbilio letu la usalama. Serah