< Psalms 45 >
1 Unto the end, for them that shall be changed, for the sons of Core, for understanding. A canticle for the Beloved. My heart hath uttered a good word I speak my works to the king; My tongue is the pen of a scrivener that writeth swiftly.
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa utenzi wa “Yungiyungi.” Utenzi wa wana wa Kora. Wimbo wa arusi. Moyo wangu umesisimuliwa na jambo jema ninapomsimulia mfalme mabeti yangu; ulimi wangu ni kalamu ya mwandishi stadi.
2 Thou art beautiful above the sons of men: grace is poured abroad in thy lips; therefore hath God blessed thee for ever.
Wewe ni bora kuliko watu wengine wote na midomo yako imepakwa neema, kwa kuwa Mungu amekubariki milele.
3 Gird thy sword upon thy thigh, O thou most mighty.
Jifunge upanga wako pajani mwako, ee mwenye nguvu, jivike fahari na utukufu.
4 With thy comeliness and thy beauty set out, proceed prosperously, and reign. Because of truth and meekness and justice: and thy right hand shall conduct thee wonderfully.
Katika fahari yako, songa mbele kwa ushindi, kwa ajili ya kweli, unyenyekevu na haki, mkono wako wa kuume na uonyeshe matendo ya kutisha.
5 Thy arrows are sharp: under thee shall people fall, into the hearts of the king’s enemies.
Mishale yako mikali na ichome mioyo ya adui za mfalme, mataifa na yaanguke chini ya nyayo zako.
6 Thy throne, O God, is for ever and ever: the sceptre of thy kingdom is a sceptre of uprightness.
Ee Mungu, kiti chako cha enzi kitadumu milele na milele, fimbo ya utawala wa haki itakuwa fimbo ya utawala wa ufalme wako.
7 Thou hast loved justice, and hated iniquity: therefore God, thy God, hath anointed thee with the oil of gladness above thy fellows.
Unaipenda haki na kuchukia uovu; kwa hiyo Mungu, Mungu wako, amekuweka juu ya wenzako, kwa kukupaka mafuta ya furaha.
8 Myrrh and stacte and cassia perfume thy garments, from the ivory houses: out of which
Mavazi yako yote yana harufu nzuri ya manemane, udi na mdalasini; kutoka kwenye majumba ya kifalme yaliyopambwa kwa pembe za ndovu, sauti za vinanda vya nyuzi zinakufanya ufurahi.
9 The daughters of kings have delighted thee in thy glory. The queen stood on thy right hand, in gilded clothing; surrounded with variety.
Binti za wafalme ni miongoni mwa wanawake wako waheshimiwa; kuume kwako yupo bibi arusi malkia aliyevaa dhahabu ya Ofiri.
10 Hearken, O daughter, and see, and incline thy ear: and forget thy people and thy father’s house.
Sikiliza, ewe binti, fikiri na utege sikio: Sahau watu wako na nyumba ya baba yako.
11 And the king shall greatly desire thy beauty; for he is the Lord thy God, and him they shall adore.
Mfalme ameshangazwa na uzuri wako; mheshimu, kwa kuwa yeye ni bwana wako.
12 And the daughters of Tyre with gifts, yea, all the rich among the people, shall entreat thy countenance.
Binti wa Tiro atakuletea zawadi, watu wenye utajiri watatafuta upendeleo wako.
13 All the glory of the king’s daughter is within in golden borders,
Utukufu wote una binti mfalme katika chumba chake; vazi lake limefumwa kwa nyuzi za dhahabu.
14 Clothed round about with varieties. After her shall virgins be brought to the king: her neighbours shall be brought to thee.
Anaongozwa kwa mfalme, akiwa amevalia mavazi yaliyotariziwa, mabikira wenzake wanamfuata na wanaletwa kwako.
15 They shall be brought with gladness and rejoicing: they shall be brought into the temple of the king.
Wanaingizwa ndani kwa shangwe na furaha, na kuingia katika jumba la mfalme.
16 Instead of thy fathers, sons are born to thee: thou shalt make them princes over all the earth.
Wana wenu watachukua nafasi za baba zenu, mtawafanya wakuu katika nchi yote.
17 They shall remember thy name throughout all generations. Therefore shall people praise thee for ever; yea, for ever and ever.
Nitadumisha kumbukumbu lako katika vizazi vyote, kwa hiyo mataifa watakusifu milele na milele.