< Psalms 36 >

1 Unto the end, for the servant of God, David himself. The unjust hath said within himself, that he would sin: there is no fear of God before his eyes.
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi mtumishi wa Bwana. Kuna neno moyoni mwangu kuhusu hali ya dhambi ya mwovu. Hakuna hofu ya Mungu mbele ya macho yake.
2 For in his sight he hath done deceitfully, that his iniquity may be found unto hatred.
Kwa kuwa machoni pake mwenyewe hujisifu mno hata hawezi kugundua au kuichukia dhambi yake.
3 The words of his mouth are iniquity and guile: he would not understand that he might do well.
Maneno ya kinywa chake ni maovu na ya udanganyifu, ameacha kuwa mwenye hekima na kutenda mema.
4 He hath devised iniquity on his bed, he hath set himself on every way that is not good: but evil he hath not hated.
Hata kitandani mwake hupanga hila mbaya, hujitia katika njia ya dhambi na hakatai lililo baya.
5 O Lord, thy mercy is in heaven, and thy truth reacheth, even to the clouds.
Upendo wako, Ee Bwana, unafika hadi mbinguni, uaminifu wako hadi kwenye anga.
6 Thy justice is as the mountains of God, thy judgments are a great deep. Men and beasts thou wilt preserve, O Lord:
Haki yako ni kama milima mikubwa, hukumu zako ni kama kilindi kikuu. Ee Bwana, wewe huwahifadhi mwanadamu na mnyama.
7 O how hast thou multiplied thy mercy, O God! But the children of men shall put their trust under the covert of thy wings.
Upendo wako usiokoma ni wa thamani mno! Watu wakuu na wadogo hujificha uvulini wa mbawa zako.
8 They shall be inebriated with the plenty of thy house; and thou shalt make them drink of the torrent of thy pleasure.
Wanajifurahisha katika wingi nyumbani mwako, nawe utawanywesha katika mto wa furaha zako.
9 For with thee is the fountain of life; and in thy light we shall see light.
Kuwa pamoja nawe ni kijito cha uzima, katika nuru yako twaona nuru.
10 Extend thy mercy to them that know thee, and thy justice to them that are right in heart.
Dumisha upendo wako kwa wale wanaokujua wewe, haki yako kwa wale walio wanyofu wa moyo.
11 Let not the foot of pride come to me, and let not the hand of the sinner move me.
Mguu wa mwenye kiburi usije dhidi yangu, wala mkono wa mwovu usinifukuze.
12 There the workers of iniquity are fallen, they are cast out, and could not stand.
Angalia jinsi watenda mabaya walivyoanguka: wametupwa chini, hawawezi kuinuka!

< Psalms 36 >