< Psalms 19 >
1 Unto the end. A psalm for David. The heavens shew forth the glory of God, and the firmament declareth the work of his hands.
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Mbingu zinatangaza utukufu wa Mungu, anga zahubiri kazi ya mikono yake.
2 Day to day uttereth speech, and night to night sheweth knowledge.
Siku baada ya siku zinatoa habari, usiku baada ya usiku zinatangaza maarifa.
3 There are no speeches nor languages, where their voices are not heard.
Hakuna msemo wala lugha, ambapo sauti zao hazisikiki.
4 Their sound hath gone forth into all the earth: and their words unto the ends of the world.
Sauti yao imeenea duniani pote, nayo maneno yao yameenea hadi miisho ya ulimwengu. Katika mbingu amepiga hema kwa ajili ya jua,
5 He hath set his tabernacle in the sun: and he, as a bridegroom coming out of his bride chamber, Hath rejoiced as a giant to run the way:
linafanana na bwana arusi akitoka chumbani mwake, kama shujaa afurahiavyo kukamilisha kushindana kwake.
6 His going out is from the end of heaven, And his circuit even to the end thereof: and there is no one that can hide himself from his heat.
Huchomoza upande mmoja wa mbingu, na kufanya mzunguko wake hadi upande mwingine. Hakuna kilichojificha joto lake.
7 The law of the Lord is unspotted, converting souls: the testimony of the Lord is faithful, giving wisdom to little ones.
Sheria ya Bwana ni kamilifu, ikihuisha nafsi. Shuhuda za Bwana ni za kuaminika, zikimpa mjinga hekima.
8 The justices of the Lord are right, rejoicing hearts: the commandment of the Lord is lightsome, enlightening the eyes.
Maagizo ya Bwana ni kamili, nayo hufurahisha moyo. Amri za Bwana huangaza, zatia nuru machoni.
9 The fear of the Lord is holy, enduring for ever and ever: the judgments of the Lord are true, justified in themselves.
Kumcha Bwana ni utakatifu, nako kwadumu milele. Amri za Bwana ni za hakika, nazo zina haki.
10 More to be desired than gold and many precious stones: and sweeter than honey and the honeycomb.
Ni za thamani kuliko dhahabu, kuliko dhahabu iliyo safi sana, ni tamu kuliko asali, kuliko asali kutoka kwenye sega.
11 For thy servant keepeth them, and in keeping them there is a great reward.
Kwa hizo mtumishi wako anaonywa, katika kuzishika kuna thawabu kubwa.
12 Who can understand sins? from my secret ones cleanse me, O Lord:
Ni nani awezaye kutambua makosa yake? Nisamehe makosa yangu nisiyoyajua.
13 And from those of others spare thy servant. If they shall have no dominion over me, then shall I be without spot: and I shall be cleansed from the greatest sin.
Mlinde mtumishi wako na dhambi za makusudi, nazo zisinitawale. Ndipo nitakapokuwa sina lawama, wala sitakuwa na hatia ya kosa kubwa.
14 And the words of my mouth shall be such as may please: and the meditation of my heart always in thy sight. O Lord, my helper, and my redeemer.
Maneno ya kinywa changu na mawazo ya moyo wangu, yapate kibali mbele zako, Ee Bwana, Mwamba wangu na Mkombozi wangu.