< Psalms 17 >

1 The prayer of David. Hear, O Lord, my justice: attend to my supplication. Give ear unto my prayer, which proceedeth not from deceitful lips.
Maombi ya Daudi. Sikia ombi langu kwa ajili ya haki, Yawhe; uusikilize mwito wangu wa msaada. Uyasikilize maombi yangu yatokayo katika midomo isiyo na udanganyifu.
2 Let my judgment come forth from thy countenance: let thy eyes behold the things that are equitable.
Uthibitisho wangu na uje kutoka uweponi mwako; macho yako na yaone kile kilicho sahihi!
3 Thou hast proved my heart, and visited it by night, thou hast tried me by fire: and iniquity hath not been found in me.
Kama utaujaribu moyo wangu, kama utakuja kwangu wakati wa usiku, wewe utanitakasa na hautapata mipango yeyote ya uovu; mdomo wangu hautavunja sheria.
4 That my mouth may not speak the works of men: for the sake of the words of thy lips, I have kept hard ways.
Kama kwa matendo ya binadamu, ni katika neno la midomo yako ya kuwa nimejiepusha na njia za wahalifu.
5 Perfect thou my goings in thy paths: that my footsteps be not moved.
Mwenendo wangu umeshikila kwa umakini mwenendo wako; miguu yangu haija teleza.
6 I have cried to thee, for thou, O God, hast heard me: O incline thy ear unto me, and hear my words.
Nakuita wewe, kwa kuwa unanijibu, Mungu; geizia sikio lako kwangu na usikilize ninapo ongea.
7 Shew forth thy wonderful mercies; thou who savest them that trust in thee.
Onyesha uaminifu wa agano lako katika namna ya ajabu, wewe uokoaye kwa mkono wa haki yako wale wanao kukimbilia wewe kutoka kwa adui zao.
8 From them that resist thy right hand keep me, as the apple of thy eye. Protect me under the shadow of thy wings.
Unilinde kama mboni ya jicho lako; unifiche katika kivuli cha mbawa zako
9 From the face of the wicked who have afflicted me. My enemies have surrounded my soul:
kutoka katika uwepo wa waovu ambao wananitusi, adui zangu wanizungukao.
10 They have shut up their fat: their mouth hath spoken proudly.
Wao hawana huruma kwa yeyote; midomo yao huongea kwa majivuno.
11 They have cast me forth and now they have surrounded me: they have set their eyes bowing down to the earth.
Wao wame zizunguka hatua zangu. Wamekaza macho yao wanishambulie mpaka ardhini.
12 They have taken me, as a lion prepared for the prey; and as a young lion dwelling in secret places.
Wao ni kama mfano wa hasira ya simba mawindoni. Ni kama simba kijana anapotokea mafichoni.
13 Arise, O Lord, disappoint him and supplant him; deliver my soul from the wicked one: thy sword
Inuka, Yahwe! Uwashambulie! Uwaangushe chini kwenye nyuso zao! Uyaokoe maisha yangu kutokana na waovu kwa upanga wako!
14 From the enemies of thy hand. O Lord, divide them from the few of the earth in their life: their belly is filled from thy hidden stores. They are full of children: and they have left to their little ones the rest of their substance.
Uniokoe kutoka kwa watu hawa kwa mkono wako, Yahwe, kutoka kwa watu wa dunia hii ambao utajiri wao ni maisha haya pekee! Wewe utayajaza matumbo ya wale uwathaminio na utajiri; watakuwa na watoto wengi na wataacha utajiri wao kwa watoto wao.
15 But as for me, I will appear before thy sight in justice: I shall be satisfied when thy glory shall appear.
Bali mimi, nitauona uso wako katika haki; Nitashuhudiwa, pale nitakapo amka, na macho yako.

< Psalms 17 >