< Psalms 129 >

1 Often have they fought against me from my youth, let Israel now say.
Wimbo wa kwenda juu. Wamenionea mno tangu ujana wangu; Israeli na aseme sasa:
2 Often have they fought against me from my youth: but they could not prevail over me.
wamenionea mno tangu ujana wangu, lakini bado hawajanishinda.
3 The wicked have wrought upon my back: they have lengthened their iniquity.
Wakulima wamelima mgongo wangu, na kufanya mifereji yao mirefu.
4 The Lord who is just will cut the necks of sinners:
Lakini Bwana ni mwenye haki; amenifungua toka kamba za waovu.
5 Let them all be confounded and turned back that hate Sion.
Wale wote waichukiao Sayuni na warudishwe nyuma kwa aibu.
6 Let them be as grass on the tops of houses: which withered before it be plucked up:
Wawe kama majani juu ya paa, ambayo hunyauka kabla hayajakua;
7 Wherewith the mower filleth not his hand: nor he that gathereth sheaves his bosom.
kwa hayo mvunaji hawezi kujaza vitanga vyake, wala akusanyaye kujaza mikono yake.
8 And they that have passed by have not said: The blessing of the Lord be upon you: we have blessed you in the name of the Lord.
Wale wapitao karibu na wasiseme, “Baraka ya Bwana iwe juu yako; tunakubariki katika jina la Bwana.”

< Psalms 129 >