< Psalms 111 >

1 I will praise thee, O Lord, with my whole heart; in the council of the just: and in the congregation.
Msifuni Bwana. Nitamtukuza Bwana kwa moyo wangu wote, katika baraza la wanyofu na katika kusanyiko.
2 Great are the works of the Lord: sought out according to all his wills.
Kazi za Bwana ni kuu, wote wanaopendezwa nazo huzitafakari.
3 His work is praise and magnificence: and his justice continueth for ever and ever.
Kazi zake zimejaa fahari na utukufu, haki yake hudumu daima.
4 He hath made a remembrance of his wonderful works, being a merciful and gracious Lord:
Amefanya maajabu yake yakumbukwe, Bwana ni mwenye neema na huruma.
5 He hath given food to them that fear him. He will be mindful for ever of his covenant:
Huwapa chakula wale wanaomcha, hulikumbuka agano lake milele.
6 He will shew forth to his people the power of his works.
Amewaonyesha watu wake uwezo wa kazi zake, akiwapa nchi za mataifa mengine.
7 That he may give them the inheritance of the Gentiles: the works of his hands are truth and judgment.
Kazi za mikono yake ni za uaminifu na haki, mausia yake yote ni ya kuaminika.
8 All his commandments are faithful: confirmed for ever and ever, made in truth and equity.
Zinadumu milele na milele, zikifanyika kwa uaminifu na unyofu.
9 He hath sent redemption to his people: he hath commanded his covenant for ever. Holy and terrible is his name:
Aliwapa watu wake ukombozi, aliamuru agano lake milele: jina lake ni takatifu na la kuogopwa.
10 The fear of the Lord is the beginning of wisdom. A good understanding to all that do it: his praise continueth for ever and ever.
Kumcha Bwana ndicho chanzo cha hekima, wote wanaozifuata amri zake wana busara. Sifa zake zadumu milele.

< Psalms 111 >