< Psalms 109 >

1 Unto the end, a psalm for David.
Zaburi ya Daudi. Mungu ninaye msifu, usinyamaze kimya.
2 O God, be not thou silent in thy praise: for the mouth of the wicked and the mouth of the deceitful man is opened against me.
Kwa maana waovu na wadanganyifu wananishambulia; wanazungumza uongo dhidi yangu.
3 They have spoken against with deceitful tongues; and they have compassed me about with words of hatred; and have fought against me without cause.
Wananizunguka na kusema mambo ya chuki, na wananishambulia bila sababu.
4 Instead of making me a return of love, they detracted me: but I gave myself to prayer.
Wananilipa kashfa badala ya upendo, lakini mimi ninawaombea.
5 And they repaid me evil for good: and hatred for my love.
Wananilipa uovu badala ya mema, na wanachukia upendo wangu.
6 Set thou the sinner over him: and may the devil stand at his right hand.
Teua mtu mwovu aliye adui zaidi kama watu hawa; teua mshitaki asimame mkono wake wa kuume.
7 When he is judged, may he go out condemned; and may his prayer be turned to sin.
Na atakapohukumiwa, aonekane na hatia; maombi yake yachukuliwe kuwa ni dhambi.
8 May his days be few: and his bishopric let another take.
Siku zake na ziwe chahe; mamlaka yake na yachukuliwe na mtu mwingine.
9 May his children be fatherless, and his wife a widow.
Watoto wake wawe yatima, na mke wake awe mjane.
10 Let his children be carried about vagabonds, and beg; and let them be cast out of their dwellings.
Watoto wake wenye kutanga tanga na kuombaomba, wakiondoka katika nyumba zao zilizo haribika na kuomba chakula au pesa kwa wapita njia.
11 May the userer search all his substance: and let strangers plunder his labours.
Mdai na achukue vitu vyake vyote amilikivyo; wageni wateke mapato ya kazi yake.
12 May there be none to help him: nor none to pity his fatherless offspring.
Asiwepo mtu yeyote wa kumfanyia wema; mtu yeyote asiwahurumie yatima wake.
13 May his posterity be cut off; in one generation may his name be blotted out.
Watoto wake waangamizwe; majina yao na yafutwe katika kizazi kijacho.
14 May the iniquity of his fathers be remembered in the sight of the Lord: and let not the sin of his mother be blotted out.
Uovu wa baba zake utajwe kwa Yahwe; na dhambi ya mama yake isisahaulike.
15 May they be before the lord continually, and let the memory of them perish from the earth:
Hatia zao na ziwe mbele ya Yahwe siku zote; Yahwe na aiondoe kumbukumbu yao duniani.
16 Because he remembered not to show mercy,
Yahwe na afanye hivi kwa sababu mtu huyu kamwe hakusumbuka kuonesha uaminifu wa agano wowote, lakini badala yake aliwasumbua wanyonge, wahitaji, na kuwaua walio vunjika moyo.
17 But persecuted the poor man and the beggar; and the broken in heart, to put him to death.
Alipenda kulaani; na imrudie juu yake. Alichukia kubariki; baraka zozote na zisije kwake.
18 And he loved cursing, and it shall come unto him: and he would not have blessing, and it shall be far from him. And he put on cursing, like a garment: and it went in like water into his entrails, and like oil in his bones.
Alijivika kulaani kana kwamba ni vazi lake, na laana yake iliingia ndani yake kama maji, na kama mafuta mifupani mwake.
19 May it be unto him like a garment which covereth him; and like a girdle with which he is girded continually.
Laana zake na ziwe kwake kama vazi avaalo kujifunika mwenyewe, na kama mkanda avaao kila siku.
20 This is the work of them who detract me before the Lord; and who speak evils against my soul.
Na haya yawe malipo ya mshitaki wangu kutoka kwa Yahwe, ya wale wasemao mambo maovu juu yangu.
21 But thou, O Lord, do with for thy names sake: because thy mercy is sweet. Do thou deliver me.
Yahwe Bwana wangu, unishughulikie kwa wema kwa ajili ya jina lako. Kwa sababu uaminifu wa agano lako ni mwema, uniokoe.
22 For I am poor and needy, and my heart is troubled within me.
Kwa maana ni mnyonge na muhitaji, na moyo wangu umejeruhiwa ndani yangu.
23 I am taken away like the shadow when it declineth: and I am shaken off as locusts.
Ninatoweka kama kivuli cha jioni; ninapeperushwa kama nzige.
24 My knees are weakened through fasting: and my flesh is changed for oil.
Magoti yangu ni dhaifu kutokana na kufunga; ninakuwa mwembamba na mifupa.
25 And I am become a reproach to them: they saw me and they shaked their heads,
Nimedharauliwa na washitaki wangu; wanionapo; hutikisa vichwa vyao.
26 Help me, O Lord my God; save me according to thy mercy.
Nisaidie, Yahwe Mungu wangu; uniokoe kwa uaminifu wa agano lako.
27 And let them know that this is thy hand: and that thou, O Lord, hast done it.
Nao wajue kuwa wewe umefanya haya, kwamba wewe, Yahwe, umetenda haya.
28 They will curse and thou will bless: let them that rise up against me be confounded: but thy servant shall rejoice.
Ingawa wananilaani, tafadhali unibariki; wanishambuliapo, waaibishwe, lakini mtumishi wako afurahi.
29 Let them that detract me be clothed with shame: and let them be covered with the their confusion as with a double cloak.
Washitaki wangu na wavishwe kwa aibu; wavae aibu yao kama vazi.
30 I will give great thanks to the Lord with my mouth: and in the midst of many I will praise him.
Kwa kinywa changu ninatoa shukrani kuu kwa Yahwe; nitamsifu yeye katikati ya kusanyiko.
31 Because he hath stood at the right hand of the poor, to save my soul from persecutors.
Maana nitasimama mkono wa kuume wa mhitaji, ili nimuokoe dhidi ya wale wanao muhukumu.

< Psalms 109 >