< Psalms 104 >

1 For David himself. Bless the Lord, O my soul: O Lord my God, thou art exceedingly great. Thou hast put on praise and beauty:
Ee nafsi yangu, umhimidi Bwana. Ee Bwana Mungu wangu, wewe ni mkuu sana, umejivika utukufu na enzi.
2 And art clothed with light as with a garment. Who stretchest out the heaven like a pavilion:
Amejifunika katika nuru kama vile kwa vazi, amezitandaza mbingu kama hema
3 Who coverest the higher rooms thereof with water. Who makest the clouds thy chariot: who walkest upon the wings of the winds.
na kuziweka nguzo za orofa yake juu ya maji. Huyafanya mawingu kuwa gari lake, na hupanda kwenye mbawa za upepo.
4 Who makest thy angels spirits: and thy ministers a burning fire.
Huzifanya pepo kuwa wajumbe wake, miali ya moto watumishi wake.
5 Who hast founded the earth upon its own bases: it shall not be moved for ever and ever.
Ameiweka dunia kwenye misingi yake, haiwezi kamwe kuondoshwa.
6 The deep like a garment is its clothing: above the mountains shall the waters stand.
Uliifunika kwa kilindi kama kwa vazi, maji yalisimama juu ya milima.
7 At thy rebuke they shall flee: at the voice of thy thunder they shall fear.
Lakini kwa kukemea kwako maji yalikimbia, kwa sauti ya radi yako yakatoroka,
8 The mountains ascend, and the plains descend into the place which thou hast founded for them.
yakapanda milima, yakateremka mabondeni, hadi mahali pale ulipoyakusudia.
9 Thou hast set a bound which they shall not pass over; neither shall they return to cover the earth.
Uliyawekea mpaka ambao hayawezi kuuvuka, kamwe hayataifunika dunia tena.
10 Thou sendest forth springs in the vales: between the midst of the hills the waters shall pass.
Huzifanya chemchemi zimwage maji mabondeni, hutiririka kati ya milima.
11 All the beasts of the field shall drink: the wild asses shall expect in their thirst.
Huwapa maji wanyama wote wa kondeni, punda-mwitu huzima kiu yao.
12 Over them the birds of the air shall dwell: from the midst of the rocks they shall give forth their voices.
Ndege wa angani hufanya viota kando ya maji, huimba katikati ya matawi.
13 Thou waterest the hills from thy upper rooms: the earth shall be filled with the fruit of thy works:
Huinyeshea milima kutoka orofa zake, dunia inatoshelezwa kwa matunda ya kazi yake.
14 Bringing forth grass for cattle, and herb for the service of men. That thou mayst bring bread out of the earth:
Huyafanya majani ya mifugo yaote, na mimea kwa watu kulima, wajipatie chakula kutoka ardhini:
15 And that wine may cheer the heart of man. That he may make the face cheerful with oil: and that bread may strengthen man’s heart.
divai ya kuufurahisha moyo wa mwanadamu, mafuta kwa ajili ya kungʼarisha uso wake, na mkate wa kutia mwili nguvu.
16 The trees of the field shall be filled, and the cedars of Libanus which he hath planted:
Miti ya Bwana inanyeshewa vizuri, mierezi ya Lebanoni aliyoipanda.
17 There the sparrows shall make their nests. The highest of them is the house of the heron.
Humo ndege hufanya viota vyao, korongo ana nyumba yake kwenye msunobari.
18 The high hills are a refuge for the harts, the rock for the irchins.
Milima mirefu ni makao ya mbuzi-mwitu, majabali ni kimbilio la pelele.
19 He hath made the moon for seasons: the sun knoweth his going down.
Mwezi hugawanya majira, na jua hutambua wakati wake wa kutua.
20 Thou hast appointed darkness, and it is night: in it shall all the beasts of the woods go about:
Unaleta giza, kunakuwa usiku, wanyama wote wa mwituni huzurura.
21 The young lions roaring after their prey, and seeking their meat from God.
Simba hunguruma kwa mawindo yao, na kutafuta chakula chao kutoka kwa Mungu.
22 The sun ariseth, and they are gathered together: and they shall lie down in their dens.
Jua huchomoza, nao huondoka, hurudi na kulala katika mapango yao.
23 Man shall go forth to his work, and to his labour until the evening.
Kisha mwanadamu huenda kazini mwake, katika kazi yake mpaka jioni.
24 How great are thy works, O Lord? thou hast made all things in wisdom: the earth is filled with thy riches.
Ee Bwana, jinsi matendo yako yalivyo mengi! Kwa hekima ulizifanya zote, dunia imejaa viumbe vyako.
25 So is this great sea, which stretcheth wide its arms: there are creeping things without number: Creatures little and great.
Pale kuna bahari, kubwa na yenye nafasi tele, imejaa viumbe visivyo na idadi, vitu vyenye uhai vikubwa na vidogo.
26 There the ships shall go. This sea dragon which thou hast formed to play therein.
Huko meli huenda na kurudi, pia Lewiathani, uliyemuumba acheze ndani yake.
27 All expect of thee that thou give them food in season.
Hawa wote wanakutazamia wewe, uwape chakula chao kwa wakati wake.
28 What thou givest to them they shall gather up: when thou openest thy hand, they shall all be filled with good.
Wakati unapowapa, wanakikusanya, unapofumbua mkono wako, wao wanashibishwa mema.
29 But if thou turnest away thy face, they shall be troubled: thou shalt take away their breath, and they shall fail, and shall return to their dust.
Unapoficha uso wako, wanapata hofu, unapoondoa pumzi yao, wanakufa na kurudi mavumbini.
30 Thou shalt send forth thy spirit, and they shall be created: and thou shalt renew the face of the earth.
Unapopeleka Roho wako, wanaumbwa, nawe huufanya upya uso wa dunia.
31 May the glory of the Lord endure for ever: the Lord shall rejoice in his works.
Utukufu wa Bwana na udumu milele, Bwana na azifurahie kazi zake:
32 He looketh upon the earth, and maketh it tremble: he toucheth the mountains, and they smoke.
yeye aitazamaye dunia, nayo ikatetemeka, aigusaye milima, nayo ikatoa moshi.
33 I will sing to the Lord as long as I live: I will sing praise to my God while I have my being.
Nitamwimbia Bwana maisha yangu yote; nitaimba sifa kwa Mungu wangu muda wote ninaoishi.
34 Let my speech be acceptable to him: but I will take delight in the Lord.
Kutafakari kwangu na kumpendeze yeye, ninapofurahi katika Bwana.
35 Let sinners be consumed out of the earth, and the unjust, so that they be no more: O my soul, bless thou the Lord.
Lakini wenye dhambi na watoweke katika dunia na waovu wasiwepo tena. Ee nafsi yangu, msifu Bwana. Msifuni Bwana.

< Psalms 104 >