< Proverbs 9 >

1 Wisdom hath built herself a house, she hath hewn her out seven pillars.
Hekima amejenga nyumba yake; amechonga nguzo saba kutoka katika miamba.
2 She hath slain her victims, mingled her wine, and set forth her table.
Ameandaa wanyama wake kwa chakula cha usiku; ameichanganya divai yake; na kuandaa meza yake.
3 She hath sent her maids to invite to the tower, and to the walls of the city:
Amewatuma watumishi wake kupeleka mialiko na kutoka mahali pa juu sana kwenye mji anaita:
4 Whosoever is a little one, let him come to me. And to the unwise she said:
“Wale wasiofunzwa waje hapa!” anawaambia wale wasionaufahamu.
5 Come, eat my bread, and drink the wine which I have mingled for you.
Njoo, ule chakula, na unywe divai nimeshaichanganya.
6 Forsake childishness, and live, and walk by the ways of prudence.
Acheni njia zenu za kijinga, na mkaishi; tembeeni katika njia ya ufahamu.
7 He that teacheth a scorner, doth an injury to himself: and he that rebuketh a wicked man, getteth himself a blot.
Yeyote amrekebishaye mwenye dhihaka hukaribisha matusi na yeyote anayemshutumu mtu mbaya atapata madhara.
8 Rebuke not a scorner lest he hate thee. Rebuke a wise man, and he will love thee.
Usimshutumu mwenye dhihaka, ama atakuchukia; mshutumu mtu mwenye busara, naye atakupenda.
9 Give an occasion to a wise man, and wisdom shall be added to him. Teach a just man, and he shall make haste to receive it.
Mpe mafundisho mtu mwenye busara, naye atakuwa na busara zaidi; mfundishe mtu mwenye haki, naye ataongeza elimu.
10 The fear of the Lord is the beginning of wisdom: and the knowledge of the holy is prudence.
Hofu ya Mungu ni chanzo cha hekima na maarifa ya Mtakatifu ni ufahamu.
11 For by me shall thy days be multiplied, and years of life shall be added to thee.
Maana kwa njia yangu siku zako zitazidishwa na uzima wako utaongezewa miaka.
12 If thou be wise, thou shalt be so to thyself: and if a scorner, thou alone shalt bear the evil.
Kama unahekima, unahekima kwako mwenyewe, lakini ukidharau, utaibeba peke yako.
13 A foolish woman and clamorous, and full of allurements, and knowing nothing at all,
Mwanamke mpumbavu anakelele nyingi- hajafunzwa wala haelewi chochote.
14 Sat at the door of her house, upon a seat, in a high place of the city,
Anakaa kwenye mlango wa nyumba yake, kwenye kiti cha sehemu ya juu sana ya mji.
15 To call them that pass by the way, and go on their journey:
Anawaita kwa sauti wanaopita karibu, watu wale wanaotembea wima katika njia zao.
16 He that is a little one, let him turn to me. And to the fool she said:
Wale ambao hamjafunzwa njoni hapa ndani!” anawaambia wale wasio na akili. “
17 Stolen waters are sweeter, and hid den bread is more pleasant.
Maji ya kuiba ni matamu na mkate unaoliwa kwa siri unapendeza.”
18 And he did not know that giants are there, and that her guests are in the depths of hell. (Sheol h7585)
Lakini hajui kwamba wafu wapo pale, wageni wake wapo kwenye vina vya kuzimu. (Sheol h7585)

< Proverbs 9 >