< Proverbs 9 >

1 Wisdom hath built herself a house, she hath hewn her out seven pillars.
Hekima amejenga nyumba yake; amechonga nguzo zake saba.
2 She hath slain her victims, mingled her wine, and set forth her table.
Ameandaa nyama na kuchanganya divai yake; pia ameandaa meza yake.
3 She hath sent her maids to invite to the tower, and to the walls of the city:
Amewatuma watumishi wake wa kike, naye huita kutoka mahali pa juu sana pa mji.
4 Whosoever is a little one, let him come to me. And to the unwise she said:
Anawaambia wale wasio na akili, “Wote ambao ni wajinga na waje hapa!
5 Come, eat my bread, and drink the wine which I have mingled for you.
Njooni, mle chakula changu na mnywe divai niliyoichanganya.
6 Forsake childishness, and live, and walk by the ways of prudence.
Acheni njia zenu za ujinga nanyi mtaishi; tembeeni katika njia ya ufahamu.
7 He that teacheth a scorner, doth an injury to himself: and he that rebuketh a wicked man, getteth himself a blot.
“Yeyote anayemkosoa mwenye mzaha hukaribisha matukano; yeyote anayekemea mtu mwovu hupatwa na matusi.
8 Rebuke not a scorner lest he hate thee. Rebuke a wise man, and he will love thee.
Usimkemee mwenye mzaha la sivyo atakuchukia; mkemee mwenye hekima naye atakupenda.
9 Give an occasion to a wise man, and wisdom shall be added to him. Teach a just man, and he shall make haste to receive it.
Mfundishe mtu mwenye hekima naye atakuwa na hekima zaidi; mfundishe mtu mwadilifu naye atazidi kufundishika.
10 The fear of the Lord is the beginning of wisdom: and the knowledge of the holy is prudence.
“Kumcha Bwana ndicho chanzo cha hekima, na kumjua Aliye Mtakatifu ni ufahamu.
11 For by me shall thy days be multiplied, and years of life shall be added to thee.
Kwa maana kwa msaada wangu siku zako zitakuwa nyingi, na miaka itaongezwa katika maisha yako.
12 If thou be wise, thou shalt be so to thyself: and if a scorner, thou alone shalt bear the evil.
Kama wewe una hekima, hekima yako itakupa tuzo; kama wewe ni mtu wa mzaha, wewe mwenyewe ndiwe utateseka.”
13 A foolish woman and clamorous, and full of allurements, and knowing nothing at all,
Mwanamke aitwaye Mpumbavu ana kelele; hana adabu na hana maarifa.
14 Sat at the door of her house, upon a seat, in a high place of the city,
Huketi kwenye mlango wa nyumba yake, juu ya kiti katika mahali pa juu sana pa mji,
15 To call them that pass by the way, and go on their journey:
akiita wale wapitao karibu, waendao moja kwa moja kwenye njia yao.
16 He that is a little one, let him turn to me. And to the fool she said:
Anawaambia wale wasio na akili, “Wote ambao ni wajinga na waje hapa ndani!”
17 Stolen waters are sweeter, and hid den bread is more pleasant.
“Maji yaliyoibiwa ni matamu; chakula kinacholiwa sirini ni kitamu!”
18 And he did not know that giants are there, and that her guests are in the depths of hell. (Sheol h7585)
Lakini hawajui hata kidogo kuwa wafu wako humo, kwamba wageni wake huyo mwanamke wako katika vilindi vya kuzimu. (Sheol h7585)

< Proverbs 9 >