< Proverbs 6 >

1 My son, if thou be surety for thy friend, thou hast engaged fast thy hand to a stranger.
Mwanangu, kama utaweka pesa zako kuwa dhamana kwa mkopo wa jirani yako; kama ukitoa ahadi yako katika mkopo wa mtu usiyemjua,
2 Thou art ensnared with the words of thy mouth, and caught with thy own words.
basi umejiwekea mtego mwenyewe na umenaswa kwa maneno ya kinywa chako.
3 Do therefore, my son, what I say, and deliver thyself: because thou art fallen into the hand of thy neighbour. Run about, make haste, stir up thy friend:
Mwanagu, ukinaswa kwa maneno yako mwenyewe, fanya haya ili kujiokoa, kwa kuwa umeangukia kwenye mikono ya jirani yako; nenda unyenyekee na ufanye shauri mbele ya jirani yako.
4 Give not sleep to thy eyes, neither let thy eyelids slumber.
Usiruhusu usingizi katika macho yako wala kope za macho yako kusinzia.
5 Deliver thyself as a doe from the hand, and as a bird from the hand of the fowler.
Jiokoe mwenyewe kama swala kutoka katika mkono wa mwindaji, kama ndege kutoka katika mkono wa mwinda ndege.
6 Go to the ant, O sluggard, and consider her ways, and learn wisdom:
Wewe mtu mvivu, mwangalie mchwa, zitafakari njia zake ili kupata busara.
7 Which, although she hath no guide, nor master, nor captain,
Hana akida, afisa au mtawala,
8 Provideth her meat for herself in the summer, and gathereth her food in the harvest.
lakini huandaa chakula chake wakati wa joto na wakati wa mavuno huweka hazina ili kula baadaye.
9 How long wilt thou sleep, O sluggard? when wilt thou rise out of thy sleep?
Ewe mtu mvivu, utalala hata lini? Wakati gani utainuka usingizini?”
10 Thou wilt sleep a little, thou wilt slumber a little, thou wilt fold thy hands a little to sleep:
Lala kidogo, sizia kidogo, kunja mikono kupumzika kidogo” -
11 And want shall come upon thee, as a traveller, and poverty as a man armed. But if thou be diligent, thy harvest shall come as a fountain, and want shall flee far from thee.
ndipo umasikini wako utakapokujia kama mporaji na uhitaji wako kama askari wa vita.
12 A man that is an apostate, an unprofitable man, walketh with a perverse mouth,
Mtu asiyefaa-mtu mwovu- huishi kwa kauli za udanganyifu wake,
13 He winketh with the eyes, presseth with the foot, speaketh with the finger.
akipepesa macho yake, akiashilia kwa miguu yake na kusonta kwa videle vyake.
14 With a wicked heart he deviseth evil, and at all times he soweth discord.
Hufanya njama za uovu kwa hila ya moyo wake; daima huchochea faraka.
15 To such a one his destruction shall presently come, and he shall suddenly be destroyed, and shall no longer have any remedy.
Kwa hiyo msiba wake utamkumba kwa ghafula, punde atavunjika vibaya wala hatapona.
16 Six things there are, which the Lord hateth, and the seventh his soul detesteth:
Kuna vitu sita ambavyo Yehova huvichukia, saba ambavyo ni chukizo kwake.
17 Haughty eyes, a lying tongue, hands that shed innocent blood,
Macho ya mtu mwenye kiburi, ulimi wa uongo, mikono inayomwaga damu ya watu maasumu,
18 A heart that deviseth wicked plots, feet that are swift to run into mischief,
moyo unaobuni njama mbaya, miguu inayokimbilia maovu upesi,
19 A deceitful witness that uttereth lies, and him that soweth discord among brethren.
shahidi asemaye uongo na apandaye faraka kati ya ndugu.
20 My son, beep the commandments of thy father, and forsake not the law of thy mother.
Mwanangu, itii amri ya baba yako na wala usiyaache mafundisho ya mama yako.
21 Bind them in thy heart continually, and put them about thy neck.
Uyafunge katika moyo wako siku zote; yafunge kwenye shingo yako.
22 When thou walkest, let them go with thee: when thou sleepest, let them keep thee; and when thou awakest, talk with them.
utembeapo, yatakuongoza; ulalapo yatakulinda, na uamkapo yatakufundisha.
23 Because the commandment is a lamp, and the law a light, and reproofs of instruction are the way of life:
Maana amri ni taa, na mafundisho ni nuru; kinga za kuadilisha za njia ya uzima.
24 That they may keep thee from the evil woman, and from the flattering tongue of the stranger.
Yanakulinda dhidi ya mwanamke malaya, dhidi ya maneno laini ya uzinzi.
25 Let not thy heart covet her beauty, be not caught with her winks:
Moyoni mwako usiutamani uzuri wake wala usitekwe katika kope zake.
26 For the price of a harlot is scarce one loaf: but the woman catcheth the precious soul of a man.
Kulala na malaya inaweza kugharimu bei ya kipande cha mkate, lakini mke wa mtu mwingine inagharimu uzima wako wote.
27 Can a man hide fire in his bosom, and his garments not burn?
Je mtu anaweza kubeba moto katika kifua chake bila kuuguza mavazi yake?
28 Or can he walk upon hot coals, and his feet not be burnt?
Je mtu anaweza kutembea juu ya makaa bila kuchomwa miguu yake?
29 So he that goeth in to his neighbour’s wife, shall not be clean when he shall touch her.
Ndivyo alivyo mtu alalaye na mke wa jirani yake; yule alalaye na huyo mke hatakosa adhabu.
30 The fault is not so great when a man hath stolen: for he stealeth to fill his hungry soul:
Watu hawawezi kumdharau mwizi kama anaiba ili kukidhi hitaji lake la njaa.
31 And if he be taken he shall restore sevenfold, and shall give up all the substance of his house.
Walakini akimatwa, atalipa mara saba ya kile alichoiba; lazima atoe kila kitu cha thamani katika nyumba yake.
32 But he that is an adulterer, for the folly of his heart shall destroy his own soul:
Mtu anayefanya uzinzi hana akili; hufanya hiyo kwa uharibifu wake mwenyewe.
33 He gathereth to himself shame and dishonour, and his reproach shall not be blotted out:
Anasitahili aibu na majeraha na fedheha yake haiwezi kuondolewa.
34 Because the jealousy and rage of the husband will not spare in the day of revenge,
Maana vivu humghadhibisha mtu; hatakuwa na huruma wakati wa kulipa kisasi chake.
35 Nor will he yield to any man’s prayers, nor will he accept for satisfaction ever so many gifts.
Ujapompa zawadi nyingi, hatakubali mbadala wa kusuruhishwa wala kulipwa.

< Proverbs 6 >