< Proverbs 29 >

1 The man that with a stiff neck despiseth him that reproveth him, shall suddenly be destroyed: and health shall not follow him.
Mtu anayeendelea kuwa na shingo ngumu baada ya maonyo mengi, ataangamia ghafula, wala hapati dawa.
2 When just men increase, the people shall rejoice: when the wicked shall bear rule, the people shall mourn.
Wenye haki wanapostawi, watu hufurahi; waovu watawalapo, watu hulia kwa huzuni.
3 A man that loveth wisdom, rejoiceth his father: but he that maintaineth bar lots, shall squander away his substance.
Mtu apendaye hekima huleta furaha kwa baba yake, bali aambatanaye na makahaba hutapanya mali yake.
4 A just king setteth up the land: a covetous man shall destroy it.
Kwa haki mfalme huipa nchi uthabiti, bali mfalme aliye na tamaa ya rushwa huiangamiza.
5 A man that speaketh to his friend with flattering and dissembling words, spreadeth a net for his feet.
Yeyote amsifuye jirani yake isivyostahili, anautandaza wavu kuitega miguu yake.
6 A snare shall entangle the wicked man when he sinneth: and the just shall praise and rejoice.
Mtu mbaya hutegwa na dhambi yake mwenyewe bali mwenye haki huweza kuimba na kufurahi.
7 The just taketh notice of the cause of the poor: the wicked is void of knowledge.
Mwenye haki hujali haki kwa ajili ya maskini, bali mwovu hajishughulishi na hilo.
8 Corrupt men bring a city to ruin: but wise men turn away wrath.
Wenye mzaha huuchochea mji, bali watu wenye hekima hugeuzia mbali hasira.
9 If a wise man contend with a fool, whether he be angry or laugh, he shall find no rest.
Kama mwenye hekima akienda mahakamani na mpumbavu, mpumbavu hukasirika na kudhihaki, wala hakuna amani.
10 Bloodthirsty men hate the upright: but just men seek his soul.
Watu wamwagao damu humchukia mtu mwadilifu na hutafuta kumuua mtu mnyofu.
11 A fool uttereth all his mind: a wise man deferreth, and keepeth it till afterwards.
Mpumbavu huonyesha hasira yake yote, bali mwenye hekima hujizuia.
12 A prince that gladly heareth lying words, hath all his servants wicked.
Kama mtawala akisikiliza uongo, maafisa wake wote huwa waovu.
13 The poor man and the creditor have met one another: the Lord is the enlightener of them both.
Mtu maskini na mtu anayeonea wanafanana kwa jambo hili: Bwana hutia nuru macho yao wote wawili.
14 The king that judgeth the poor in truth, his throne shall be established for ever.
Kama mfalme akiwaamua maskini kwa haki, kiti chake cha enzi kitakuwa thabiti siku zote.
15 The rod and reproof give wisdom: but the child that is left to his own will bringeth his mother to shame.
Fimbo ya maonyo hutia hekima, bali mtoto aliyeachiwa bila maonyo humwaibisha mama yake.
16 When the wicked are multiplied, crimes shall be multiplied: but the just shall see their downfall.
Wakati waovu wanapostawi, pia dhambi vivyo hivyo, lakini wenye haki wataliona anguko lao.
17 Instruct thy son, and he shall refresh thee, and shall give delight to thy soul.
Mrudi mwanao, naye atakupa amani, atakufurahisha nafsi yako.
18 When prophecy shall fail, the people shall be scattered abroad: but he that keepeth the law is blessed.
Mahali pasipo na ufunuo, watu kujizuia, bali ana heri mtu yule aishikaye sheria.
19 A slave will not be corrected by words: because he understandeth what thou sayest, and will not answer.
Mtumishi hawezi kuonywa kwa maneno matupu, ajapoelewa, hataitikia.
20 Hast thou seen a man hasty to speak? folly is rather to be looked for, than his amendment.
Je, unamwona mtu azungumzaye kwa haraka? Kuna matumaini zaidi kwa mpumbavu kuliko yeye.
21 He that nourisheth his servant delicately from his childhood, afterwards shall find him stubborn.
Kama mtu akimdekeza mtumishi wake tangu ujanani, atamletea sikitiko mwishoni.
22 A passionate man provoketh quarrels: and he that is easily stirred up to wrath, shall be more prone to sin.
Mtu mwenye hasira huchochea ugomvi, naye mtu mwenye hasira ya haraka hutenda dhambi nyingi.
23 Humiliation followeth the proud: and glory shall uphold the humble of spirit.
Kiburi cha mtu humshusha, bali mtu mwenye roho ya unyenyekevu hupata heshima.
24 He that is partaker with a thief, hateth his own soul: he heareth one putting him to his oath, and discovereth not.
Anayekubaliana na mwizi ni adui wa nafsi yake mwenyewe; huapishwa lakini hathubutu kushuhudia.
25 He that feareth man, shall quickly fall: he that trusteth in the Lord, shall be set on high.
Kuwaogopa watu huwa ni mtego, bali yeyote amtumainiaye Bwana atakuwa salama.
26 Many seek the face of the prince: but the judgment of every one cometh forth from the Lord.
Wengi hutafuta kusikilizwa na mtawala, bali mtu hupata haki kutoka kwa Bwana.
27 The just abhor the wicked man: and the wicked loathe them that are in the right way. The son that keepeth the word, shall be free from destruction.
Mwenye haki huwachukia sana wasio waaminifu; waovu huwachukia sana wenye haki.

< Proverbs 29 >