< Proverbs 20 >
1 Wine is a luxurious thing, and drunkenness riotous: whosoever is delighted therewith shell not be wise.
Divai ni dhihaka na kinywaji kikali ni mgomvi; anayepotea kwa kunywa hana busara.
2 As the roaring of a lion, so also is the dread of a king: he that provoketh him, sinneth against his own soul.
Kumwogopa mfalme ni kama kumwogopa simba kijana aungurumaye, yeyote anayemkasirisha hutoa fidia ya maish yake.
3 It is an honour for a man to separate himself from quarrels: but all fools are meddling with reproaches.
Ni heshima kwa mtu yeyote kujiepusha na mafarakano, bali kila mpumbavu hurukia kwenye mabishano.
4 Because of the cold the sluggard would not plough: he shall beg therefore in the summer, and it shall not be given him.
Mtu mvivu halimi majira ya kipupwe; hutafuta mazao wakati wa mavuno lakini hapati kitu.
5 Counsel in the heart of a man is like deep water: but a wise man will draw it out.
Makusudi ndani ya moyo wa mtu ni kama maji yenye kina, bali mtu mwenye ufahamu huyateka.
6 Many men are called merciful: but who shall find a faithful man?
Mara nyingi mtu husema yeye ni mwaminifu, lakini ni nani awezaye kumpata yule mwaminifu?
7 The just that walketh in his simplicity, shall leave behind him blessed children.
Mtu atendaye haki hutembea katika uaminifu wake na wana wake wanaofuata baada yake wanafuraha.
8 The king, that sitteth on the throne of judgment, scattereth away all evil with his look.
Mfalme anayeketi kwenye kiti cha hukumu akifanya kazi za kuhukumu hupembua kwa macho yake mabaya yote yaliyoko mbele yake.
9 Who can say: My heart is clean, I am pure from sin?
Nani anayeweza kusema, “Nimeuweka safi moyo wangu; nipo huru na dhambi zangu”?
10 Diverse weights and diverse measures, both are abominable before God.
Mizani tofauti na vipimo visivyosawa - Yehova huvichukia vyote.
11 By his inclinations a child is known, if his works be clean and right.
Hata kijana hujulikana kwa matendo yake, kwa mwenendo wake kama ni safi na uadilifu.
12 The hearing ear, and the seeing eye, the Lord hath made them both.
Masikio yanayosikia na macho yanayoona- Yehova aliyafanya yote.
13 Love not sleep, lest poverty oppress thee: open thy eyes, and be filled with bread.
Usipende usingizi au utakuwa masikini; fumbua macho yako na utakuwa na vyakula tele.
14 It is nought, it is nought, saith every buyer: and when he is gone away, then he will boast.
“Mbaya! Mbaya!” anasema mnunuzi, lakini akiondoka anajisifu.
15 There is gold, and a multitude of jewels: but the lips of knowledge are a precious vessel.
Ipo dhahabu na mawe ya thamani, lakini midomo yenye maarifa ni kito cha thamani.
16 Take away the garment of him that is surety for a stranger, and take a pledge from him for strangers.
Chukua vazi kama mmiliki wake ataweka fedha kama dhamana kwa deni la mgeni, na lichukue kama anaweka dhamana kwa uzinifu.
17 The bread of lying is sweet to a man: but afterwards his mouth shall be filled with gravel.
Mkate uliopatikana kwa ulaghai unaladha tamu, lakini baadaye kinywa chake kitajaa kokoto.
18 Designs are strengthened by counsels: and wars are to be managed by governments.
Mipango huimarishwa kwa ushauri na kwa mwongozo wa busara utapigana vita.
19 Meddle not with him that revealeth secrets, and walketh deceitfully, and openeth wide his lips.
Mmbea hufunua siri na kwa hiyo hupaswi kushirikiana na watu ambao huongea sana.
20 He that curseth his father, and mother, his lamp shall be put out in the midst of darkness.
Kama mtu atamlaani baba yake au mama yake, taa yake itapulizwa katikati ya giza.
21 The inheritance gotten hastily in the beginning, in the end shall be without a blessing.
Urithi uliopatikana mwanzoni kwa haraka utakuwa na mema kidogo mwishoni.
22 Say not: I will return evil: wait for the Lord and he will deliver thee.
Usiseme “Mimi nitakulipiza kwa kosa hili” Msubiri Yehova na yeye atakuokoa.
23 Diverse weights are an abomination before the Lord: a deceitful balance is not good.
Yehova huchukia mizani isiyo sawa na vipimo vya udanganyifu si vizuri.
24 The steps of man are guided by the Lord: but who is the man that can understand his own way?
Hatua za mtu huongozwa na Yehova; namna gani basi ataifahamu njia yake?
25 It is ruin to a man to devour holy ones, and after vows to retract.
Ni mtego kwa mtu kusema kwa pupa, “Kitu hiki ni kitakatifu” na kuanza kufikiri juu yake kwamba kina maana gani baada ya kufanya kiapo.
26 A wise king scattereth the wicked, and bringeth over them the wheel.
Mfalme mwenye busara huwapepeta waovu na huligeuza juu yao gurudumu la kupuria.
27 The spirit of a man is the lamp of the Lord, which searcheth all the hidden things of the bowels.
Roho ya mtu ni taa ya Yehova, hutafiti sehemu zake zote za ndani kabisa.
28 Mercy and truth preserve the king, and his throne is strengthened by clemency.
Agano la uaminifu na udhamini humhifadhi mfalme; kiti chake cha enzi hufanywa thabiti kwa upendo.
29 The joy of young men is their strength: and the dignity of old men, their grey hairs.
Utukufu wa watu vijana ni nguvu zao na fahari ya watu wazee ni mvi zao.
30 The blueness of a wound shall wipe away evils: and stripes in the more inward parts of the belly.
Mapigo yanayoleta kidonda huusafisha ubaya na vichapo hufanya sehemu za ndani kabisa kuwa safi.