< Proverbs 12 >

1 He that loveth correction, loveth knowledge: but he that hateth reproof is foolish.
Yeyote apendaye kuadibishwa hupenda maarifa, bali yeye achukiaye kuonywa ni mpumbavu.
2 He that is good, shall draw grace from the Lord: but he that trusteth in his own devices doth wickedly.
Mtu mwema hupata kibali kutoka kwa Bwana, bali Bwana humhukumu mwenye hila.
3 Men shall not be strengthened by wickedness: and the root of the just shall not be moved.
Mtu hathibitiki kutokana na uovu, bali mwenye haki hataondolewa.
4 A diligent woman is a crown to her husband: and she that doth things worthy of confusion, is a rottenness in his bones.
Mke mwenye tabia nzuri ni taji ya mumewe, bali aaibishaye ni kama uozo katika mifupa ya mumewe.
5 The thoughts of the just are judgments: and the counsels of the wicked are deceitful.
Mipango ya mtu mwadilifu ni ya haki, bali ushauri wa mwovu ni udanganyifu.
6 The words of the wicked lie in wait for blood: the mouth of the just shall deliver them.
Maneno ya waovu huotea kumwaga damu, bali maneno ya waadilifu huwaokoa.
7 Turn the wicked, and they shall not be: but the house of the just shall stand firm.
Watu waovu huondolewa na kutoweka, bali nyumba ya mwenye haki husimama imara.
8 A man shall be known by his learning: but he that is vain and foolish, shall be exposed to contempt.
Mtu husifiwa kulingana na hekima yake, bali watu wenye akili zilizopotoka hudharauliwa.
9 Better is the poor man that provideth for himself, than he that is glorious and wanteth bread.
Heri mtu wa hali ya chini mwenye mtumishi, kuliko kujifanya mtu wa hali ya juu nawe huna chakula.
10 The just regardeth the lives of his beasts: but the bowels of the wicked are cruel.
Mtu mwenye haki hujali mahitaji ya mnyama wake, bali matendo ya huruma ya mwovu ni ukatili.
11 He that tilleth his land shall be satisfied with bread: but he that pursueth idleness is very foolish. He that is delighted in passing his time over wine, leaveth a reproach in his strong holds.
Yeye alimaye shamba lake atakuwa na chakula tele, bali yeye afuataye mambo ya upuzi hana akili.
12 The desire of the wicked is the fortification of evil men: but the root of the just shall prosper.
Waovu hutamani mateka ya watu wabaya, bali shina la mwenye haki hustawi.
13 For the sins of the lips ruin draweth nigh to the evil mall: but the just shall escape out of distress.
Mtu mwovu hunaswa kwa mazungumzo yake ya dhambi, bali mwenye haki huepuka taabu.
14 By the fruit of his own mouth shall a man be filled with good things, and according to the works of his hands it shall be repaid him.
Kutokana na tunda la midomo yake mtu hujazwa na mambo mema, hakika kama ilivyo kazi ya mikono yake humtunza.
15 The way of a fool is right in his own eyes: but he that is wise hearkeneth unto counsels.
Njia ya mpumbavu huonekana sawa machoni pake mwenyewe, bali mtu mwenye hekima husikiliza ushauri.
16 A fool immediately sheweth his anger: but he that dissembleth injuries is wise.
Mpumbavu huonyesha kuudhika kwake mara moja, bali mtu wa busara hupuuza matukano.
17 He that speaketh that which he knoweth, sheweth forth justice: but he that lieth, is a deceitful witness.
Shahidi wa kweli hutoa ushuhuda wa kuaminika, bali shahidi wa uongo husema uongo.
18 There is that promiseth, and is pricked as it were with a sword of conscience: but the tongue of the wise is health.
Maneno ya kipumbavu huchoma kama upanga, bali ulimi wa mwenye hekima huleta uponyaji.
19 The lip of truth shall be steadfast for ever: but he that is a hasty witness, frameth a lying tongue.
Midomo isemayo kweli hudumu milele, bali ulimi wa uongo hudumu kwa muda mfupi tu.
20 Deceit is in the heart of them that think evil things: but joy followeth them that take counsels of peace.
Upo udanganyifu katika mioyo ya wale ambao hupanga mabaya, bali kuna furaha kwa wale wanaoleta amani.
21 Whatsoever shall befall the just man. it shall not make him sad: but the wicked shall be filled with mischief.
Hakuna dhara linalompata mwenye haki, bali waovu wana taabu nyingi.
22 Lying lips are an abomination to the Lord: but they that deal faithfully please him.
Bwana anachukia sana midomo idanganyayo, bali hufurahia watu ambao ni wa kweli.
23 A cautious man concealeth knowledge: and the heart of fools publisheth folly.
Mtu mwenye busara hujihifadhia maarifa yeye mwenyewe, bali moyo wa wapumbavu hububujika upumbavu.
24 The hand of the valiant shall bear rule: but that which is slothful, shall be under tribute.
Mikono yenye bidii itatawala, bali uvivu huishia katika kazi za utumwa.
25 Grief in the heart of a man shall bring him low, but with a good word he shall be made glad.
Moyo wa wasiwasi humlemea mtu, bali neno la huruma humfurahisha.
26 He that neglecteth a loss for the sake of a friend, is just: but the way of the wicked shall deceive them.
Mtu mwenye haki ni mwangalifu katika urafiki, bali njia ya waovu huwapotosha.
27 The deceitful man shall not find gain: but the substance of a just man shall be precious gold.
Mtu mvivu haoki mawindo yake, bali mtu mwenye bidii ana mali za thamani.
28 In the path of justice is life: but the by-way leadeth to death.
Katika njia ya haki kuna uzima; katika mapito hayo kuna maisha ya milele.

< Proverbs 12 >