< Numbers 3 >
1 These are the generations of Aaron and Moses in the day that the Lord spoke to Moses in mount Sinai.
Sasa hii ndiyo historia ya uzao wa Haruni na Musa wakati BWANA aliposema na Musa kwenye mlima Sinai.
2 And these the names of the sons of Aaron: his firstborn Nadab, then Abiu, and Eleazar, and Ithamar.
Majina ya watoto wa Haruni walikuwa Nadabu ambaye ndiyo mtoto wa kwanza, na Abihu, na Eliezeri, na Ithamari.
3 These the names of the sons of Aaron the priests that were anointed, and whose hands were filled and consecrated, to do the functions of priesthood.
Haya ndiyo majina ya wana wa Haruni, makuhani waliokuwa wamepakwa mafuta na kuwekwa wakfu kutumika kama makuhani.
4 Now Nadab and Abiu died, without children, when they offered strange fire before the Lord, in the desert of Sinai: and Eleazar and Ithamar performed the priestly office in the presence of Aaron their father.
Lakini Nadabu na Abihu walikufa mbele ya BWANA walipomtolea moto usiokubalika walipokuwa katika nyika ya Sinai. Nadabu na Abihu hawakuwa na watoto, kwa hiyo Eliazari na Ithamari walitumika kama makuhani pamoja na baba yao.
5 And the Lord spoke to Moses, saying:
BWANA alinena na Musa, akamwambia,
6 Bring the tribe of Levi, and make them stand in the sight of Aaron the priest to minister to him, and let them watch,
“Walete kabila ya Lawi na uwaweke kwa Haruni kuhani ili wamsaidie
7 And observe whatsoever appertaineth to the service of the multitude before the tabernacle of the testimony,
Nao lazima wafanye majukumu badala ya Haruni na jumuiya yote mbele ya hema ya kukutania. Lazima watumike hemani.
8 And let them keep the vessels of the tabernacle, serving in the ministry thereof.
Watayatunza mapambo ya hema ya kukutania, na watawatumikia makabila ya Israel kwa huduma ya hemani.
9 And thou shalt give the Levites for a gift,
Uwaweke Walawi kwa Haruni na watoto wake. Nimewatoa kikamilifu ili wamsaidie kuwatumikia watu wa Israel.
10 To Aaron and to his sons, to whom they are delivered by the children of Israel. But thou shalt appoint Aaron and his sons over the service of priesthood. The stranger that approacheth to minister, shall be put to death.
Umchague Haruni na watoto wake kuwa makuhani, lakini mgeni yeyote atakayekaribia lazima auawe.”
11 And the Lord spoke to Moses, saying:
BWANA alinena na Musa. akamwambia,
12 I have taken the Levites from the children of Israel, for every firstborn that openeth the womb among the children of Israel, and the Levites shall be mine.
“Tazama, nimewachagua Walawi katika watu wa Israel. Nimefanya hivyo badala ya kuchukua mzaliwa wa kwanza wa kiume wa wana wa Israel. Hawa Walawi ni wangu.
13 For every firstborn is mine: since I struck the firstborn in the land of Egypt: I have sanctified to myself whatsoever is firstborn in Israel both of man and beast, they are mine: I am the Lord.
Na hata wazaliwa wa kwanza ni mali yangu. Katika siku ambyo niliwavamia wazaliwa wote wa kwanza wa nchi ya Misri, Niliwatenga wazaliwa wa kwanza wa Israeli kwa ajili yangu, watu na wanyama pia. Ni mali yangu. Mimi ndimi BWANA.”
14 And the Lord spoke to Moses in the desert of Sinai, saying:
BWANA alinena na Musa katika nyika ya Sinai. Akasema,
15 Number the sons of Levi by the houses of their fathers and their families, every male from one month and upward.
“Wahesabu uzao wa Lawi katika kila familia, katika nyumba za koo zao. Hesabu kila mume kuanzia mwezi mmoja au zaidi.”
16 Moses numbered them as the Lord had commanded.
Musa aliwahesabu, kufuata maelekezo ya BWANA, kama alivyoamriwa kufanya.
17 And there were found sons of Levi by their names, Gerson and Caath and Merari.
Majina ya watoto waLawi yalikuwa Gerishoni, Kohathi, na Merari.
18 The sons of Gerson: Lebni and Semei.
Ukoo uliotokana na watoto wa Gerishoni walikuwa ni Libni na Shimei.
19 The sons of Caath: Amram, and Jesaar, Hebron and Oziel:
Ukoo uliotokana na watoto Kohathi walikuwa ni Amramu na, Izihari, Hebroni, na Uzieli.
20 The sons of Merari: Moholi and Musi.
Ukoo uliotokana na watoto wa Merari walikuwa ni Mahili na Mushi. Hizi ndizo koo za Walawi, zilizoorodheshwa ukoo kwa ukoo.
21 Of Gerson were two families, the Lebnites, and the Semeites:
Koo za Walibini na Washimei zilitokana na Wagerishoni. Hizi ndizo koo za Wagerishoni.
22 Of which were numbered, people of the male sex from one month and upward, seven thousand five hundred.
Wanaume wote wenye umri wa mwezi mmoja au zaidi walihesabiwa na kufikia idadi ya 7, 500.
23 These shall pitch behind the tabernacle on the west,
Koo za Wagerishoni watapanga upande wa magharibi wa hema.
24 Under their prince Eliasaph the son of Lael.
Eliasafu mwana wa Laeli ataongoza koo za uzao wa Wagerishoni.
25 And their charge shall be in the tabernacle of the covenant:
Familia ya Gerishoni watalilinda hema la kukutania pamoja na hiyo masikani. Watalilinda hema, kifuniko chake, na lile pazia la lango la hema ya kukutania.
26 The tabernacle itself and the cover thereof, the hanging that is drawn before the doors of the tabernacle of the covenant, and the curtains of the court: the hanging also that is hanged in the entry of the court of the tabernacle, and whatsoever belongeth to the rite of the altar, the cords of the tabernacle, and all the furniture thereof.
Wataulinda ua, lile pazia la kwenye lango—ua unaozunguka mahali patakatifu na madhabahu. Watazilinda kamba za hema ya kukutania na vyote vilivyomo.
27 Of the kindred of Caath come the families of the Amramites and Jesaarites and Hebronites and Ozielites. These are the families of the Caathites reckoned up by their names:
Koo zifuatazo zinatokana na Kohathi: ukoo wa Waamrami, ukoo wa Waizihari ukoo wa Wahebroni, na ukoo wa Wauzieli. Koo hizi zinatokana na Wakohathi.
28 All of the male sex from one month and upward, eight thousand six hundred: they shall have the guard of the sanctuary,
Wanaume 8, 600 wenye umri wa mwezi mmoja au zaidi walihesabiwa ili kulinda vitu vya BWANA.
29 And shall camp on the south side.
Familia ya uzao wa Kohathi watapanga upande wa kusini wa Hema.
30 And their prince shall be Elisaphan the son of Oziel:
Elizafani mwana wa Uzieli ndiye atakayeongoza ukoo wa Wakohathi.
31 And they shall keep the ark, and the table and the candlestick, the altars, and the vessels of the sanctuary, wherewith they minister, and the veil, and all the furniture of this kind.
Watalilinda sanduku, meza, vikalishio vya taa, madhabahu, vitu vitakatifu ambvyo hutumika katika huduma yao, pazia, na kazi zote zinazoambatana na hema.
32 And the prince of the princes of the Levites, Eleazar, the son of Aaron the priest, shall be over them that watch for the guard of the sanctuary.
Eliazari mwana wa Haruni kuhani atawaongoza wanaume wanaowaongoza Walawi. Atawasimamia wanaume wanaongoza eneo takatifu.
33 And of Merari are the families of the Moholites, and Musites, reckoned up by their names:
Koo mbili zimetoka kwa Merari: Ukoo wa Mahili na ukoo wa Mushi. Koo hizi zimetokana na Merari,
34 All of the male kind from one month and upward, six thousand two hundred.
Wanaume 6, 200 wenye umri wa mwezi mmoja na zaidi walihesabiwa.
35 Their prince Suriel the son of Abihaiel: they shall camp on the north side.
Zurieli mwana wa Abihaili ataongoza ukoo wa Merari. Hawa watapanga upande wa kaskazini mwa hema.
36 Under their custody shall be the boards of the tabernacle, and the bars, and the pillars and their sockets, and all things that pertain to this kind of service:
Uzao wa Merari utatunza mbao za hema, mataruma, nguzo, makalishio, viifaa vya ujenzi na vitu vyote vinavyohusika,
37 And the pillars of the court round about with their sockets, and the pins with their cords.
na nguzo za ua zinazozunguka hema, makalishio, vigingi na kamba zake.
38 Before the tabernacle of the covenant, that is to say on the east side, shall Moses and Aaron camp, with their sons, having the custody of the sanctuary, in the midst of the children of Israel. What stranger soever cometh unto it, shall be put to death.
Musa na Haruni na watoto wake watapanga upande wa mashariki wa masikani, mbele ya hema ya kukutania kuelekea mawio ya jua. Wao wataajibika na majukumu ya mahali patakatifu na majukumu ya wana wa Israeli. Mgeni atakayekaribia mahali patakatifu auawe.
39 All the Levites, that Moses and Aaron numbered according to the precept of the Lord, by their families, of the male kind from one month and upward, were twenty-two thousand.
Musa na Haruni wakawahesabu wanaume wote wa ukoo wa Walawi walikuwa na umri wa mwezi mmoja na zaidi, kama vile BWANA alivyokuwa ameagiza. Walihesabu wanaume ishirini na mbili elfu.
40 And the Lord said to Moses: Number the firstborn of the male sex of the children of Israel, from one month and upward, and thou shalt take the sum of them.
BWANA alisema na Musa, “Wahesabu wanaume wote ambo ni wazaliwa wa kwanza wa Israeli ambao wana umri wa mwezi mmoja na zaidi. Orodhesha majina yao.
41 And thou shalt take the Levites to me for all the firstborn of the children of Israel, I am the Lord: and their cattle for all the firstborn of the cattle of the children of Israel:
Unitwalie walawi kwa ajili yangu badala ya wazaliwa wa kwanza wa Israeli, Mimi ndimi BWANA. Na utwae wanyama wa Walawi badala ya wazaliwa wa kwanza wa wanyama wa uzao wa Israeli,”
42 Moses reckoned up, as the Lord had commanded, the firstborn of the children of Israel:
Musa akawahesabu wazaliwa wa kwanza wote wa Israeli kama BWANA alivyomwagiza kufanya.
43 And the males by their names, from one month and upward, were twenty-two thousand two hundred and seventy-three.
Aliwahesabu wazaliwa wote wa kwanza kwa mjina, wenye umri wa mwezi mmoja na zaidi. Alihesabu wanaume 22, 273.
44 And the Lord spoke to Moses, saving:
Tena BWANA alinena na Musa. Akasema,
45 Take the Levites for the firstborn of the children of Israel, and the cattle of the Levites for their cattle, and the Levites shall be mine. I am the Lord.
“Watwae Walawi badala ya wazaliwa wote wa kwanza wa wana wa Israeli. Na utwae wanyama wa Walawi badala ya wanyama wa Waisreli wengine. Walawi ni mali yangu. Mimi ndimi BWANA.
46 But for the price of the two hundred and seventy-three, of the firstborn of the children of Israel, that exceed the number of the Levites,
Unikusanyie shekeli tano za wokovu kwa kila hao 273 za hao wazaliwa wa kwanza wa Israeli za hao wanaozidi idadi ya Walawi.
47 Thou shalt take five sides for every head, according to the weight of the sanctuary. A sicle hath twenty obols.
Utazitumia hizo shekeli tano kwa kipimo cha mahali patakatifu. Shekeli moja ni sawa na gera ishirini.
48 And then shalt give the money to Aaron and his sons, the price of them that are above.
Utawalipa hizo shekeli za wokovu kwa Haruni na wanawe.”
49 Moses therefore took the money of them that were above, and whom they had redeemed from the Levites,
Kwa hiyo Musa akakusanya shakeli za wokovu kutoka kwa wale waliozidi idadi ya wale waliookolewa na Walawi.
50 For the firstborn of the children of Israel, one thousand three hundred and sixty-five sicles, according to the weight of the sanctuary,
Musa akakusanya zile fedha kutoka kwa hao wazaliwa wa kwanza wa wana wa Israeli. Alikusanya jumla ya shekeli 1, 365, zenye kipimo sawa na mahali patakatifu. Musa akamlipa Haruni na wanawe hizo shekeli za wokovu.
51 And gave it to Aaron and his sons, according to the word that the Lord had commanded him.
Musa akafanya kila kitu alichoagizwa na neno la BWANA kama BWANA alivyomwagiza.